Picha:Rais Kikwete afuturisha wasanii ikulu

Status
Not open for further replies.
huyu rais yenyu watu wa tz, haiko serious. yeye badala ya kufanya vitu yenye itawaletea maendelo, yeye yuko kwa kutembea na kucheka kwa picha

kwendaaaa nyie kwa kuwa hamkutani nae ndo unaona wivu
 
Ya habib..amin.
Ya shabiby..amin.
Ya hood..amin.
Ya abood..amin.
Ya dar xpres..amin.
Ya idd azan...mmmmmh!
Mapunda hao...acha wapewe deal.
 
Kumbe JK bado yupo katika Kampeni?Lakini sishangai kwani JK amekuwa busy na Kampeni badala ya kuongoza kwa muhula wote wa kwanza.Nikadhani baada ya Uchaguzi wa 2010 sasa ataanza kutuongoza nahisi nilikosea kumbe mwenzetu Kampeni hazijaisha?
Sasa hivi hayupo katika kuongoza bali anafikiri itakuwaje kwa maana kuna uwezekano wa kukabidhi nchi kwa upinzani. Pia si unajua? Chukua Chako Mapema!
 
Nasubiri viroja mwaka wa meisho ule kama 2015 au 2017!tutasikia na kuona mengi sana!
 
Ebwaana ehhh p funk alikuwepo da imekakaa poa ila kina fetty wa clouds nao wasanii hivi
 
sina tatizo na ufuturishaji au dina whatever u cal it! Ila priority kwa makundi! Ningefurah kama angewaandalia vijana waliongoza kwenye semester/term iliyopita! Au walimu wao! Au madaktari etc! Ila ndo hivyo tena taifa lishakuwa la mateja na ndio tunaowapa kipaumbele!
 
Ukistaajabu ya Mussa utaona ya Farao,Wakubwa wanamambo,Mageniuz ndo waliwazaaa
"Vox populi,Vox dei"
 
Jamaa na PUNDA wake anawapa moyo wasikate tamaa kwa kilichowatokea binti kiziwi, Ngwea,Masogange e.t.c... hilo tabasamu la GK ndo limenimaliza kabisa.
 

Hao uliowataja wakípewa sembe kupeleka sauzi wataenda!??
 

Rais Kikwete akiwa akiwa katika picha ya pamoja na Msanii wa Filamu na Bongofleva,Hemed Suleiman.

Rais Kikwete akiwa katika picha ya kumbukumbu na mmoja wa Watangazaji machachari wa Clouds FM,TV,Mbwiga Mbwiguke.


Rais Kikwete akiwa akiwa katika picha ya pamoja na Msanii Mkongwe wa Bongofleva,Gwamaka Kaihula a.k.a King Crazy G K.


Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Msanii wa bongofleva na muigizaji wa Filamu hapa nchini,atambulikae kwa jina la kisanii Zuwena Mohamed a.k.a. Shilole.
Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Wasanii wa Bongofleva,Ally Kiba na mdogo wake Abdull Kiba.


Mke wa Rais,Mama Salma Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wasanii wa muziki wa Bongofleva mara baada ya kufturu.Kutoka kushoto,Snura,Keisha,Mwasiti,aliyechuchumaa ni Shilole,Dj Fetty ,Mwanahawa Abdul a.k.a Quee Doreen.

Wasanii wa muziki wa kizazi kipya pichani shoto Mwasiti Almas na kulia Zuwena Mohamed a.k.a Shilole wakiwa sambamba na Mtangazaji wa Clouds FM,Dj Fetty wakipakua ftari kufuatia mualiko wa Rais Kikwete kwenye viwanja vya Ikulu,jijini Dar jana.


Wasanii wa muziki wa kizazi kipya a.k.a Bongofleva wakipata ftari kwenye viwanja vya Ikulu jijini Dar jana kufuatia mualiko wa Rais Kikwete.

Rais Kikwete akisalimiana na msanii wa bongofleva,Lawrence Malima a.k.a Marlow,kulia kwake ni Ally Kiba pamoja na Abdul Kiba na kushoto ni Mtangazaji wa East Africa Radio,Samisango


Rais Kikwete akisalimiana na msanii wamuziki wa kizazi kipya,Chege Chigunda na kulia kwake ni msanii wa bongofleva,Cassim Mganga,wakati wa kupata ftari jana jioni kwenye viwanja vya Ikulu jijini Dar.


Rais Kikwete akiwasabahi baadhi ya wasanii wa muziki wa kizazi kipya,mara baada ya kupata ftari mapema jana jioni kwenye viwanja vya Ikulu jijini Dar,Rais Kikwete aliwaalika wasanii mbalimbali kupata ftari ya pamoja Ikulu jana jioni.
 
Rais wenu kwa showoff si mchezo ana charactor zote za utalii
 
Iman ya kufunga afu unajua baadae utafidia mavyakula ya maana kiasi hichi huwa inanichanganya sana.

Anyways,,Ila nadhani pia hii sio gharama ya serikali.
 
Wanajamvi naomba kufahamishwa yafuatayo:

i. Hii inafanyika kwa gharama za nani? Je,ni fedha binafsi za Jk na Familia yake au ni kodi za wananchi?

ii. Nini maana halisi ya "Kufuturu" na "Kufuturisha" kwa Mwislamu safi na miiko yake?

iii. Je, "Bongo Flava" ndio kipaumbele cha Taifa??
 
Mbona nasikia wasanii ni watuhumiwa kama PUNDA WA UNGA?????
 
Ndicho anachoweza.... Huwezi kna anafuturisha wasomi, na wajenga nchi

halafu kufiturisha imeondoa sana hata maana ya ramadhan... Imeku ufujaji wa aina fulani
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…