fidel castro wapili
JF-Expert Member
- Mar 18, 2017
- 3,497
- 2,911
Amiin.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Shukran mzee wanguRelief...
Kibeku ni ungo uliozeeka umechoka hauwezi kupeta chichote.
Mungu FUNDI, amempiga upofu huyu jamaa kwa kushirikiana na Mkapa kudhulumu haki ya Wazanzibari kuishi.PICHA HII INAWEZA KUKUTOA MACHOZI
Dr. Salmin Amour aliyekuwa Rais wa Zanzibar alipotembelewa na Dr. Hussein Mwinyi nyumbani kwake.
Dr. Salmin kanyanyua mikono anamwelekea Allah kwa dua na dua siku zote ni kuomba kheri.
Dr. Salmin hivi sasa ni kipofu.
Haoni.
Amenyanyua mikono yake kamwelekea Allah anamuombea dua kijana wake ambae kama yeye miaka 25 iliyopita anasimama kugombea nafasi ya urais wa Zanzibar katika hali ile ile ngumu na ya hatari kwa usalama wa visiwa wakati alipokuwa anamkabili Maalim Seif katika nafasi hiyo hiyo ambayo Dr. Hussein Mwinyi anaitaka na dhidi ya mtu huyo huyo na katika hali ya hatari ile ile iliyokabili Zanzibar mwaka wa 1995.
Msomaji wangu nakutaka radhi kwa sentensi ndefu nimeifanya hivyo kwa kusudi ili usivute pumzi wala kumeza mate katika msisitizo ulio ndani ya sentensi hii.
Dr. Salmin Amour alikuwa anaitwa Komando yaani mpiganaji hodari anaemudu kuzitumia silaha zote za kivita kwa ufanisi mkubwa mpiganaji ambae kifua chake kipana na mwenye misuli iliyotuna inayotisha adui.
Dr. Salmin Komando hotuba zake zilikuwa kali za kuogofya.
Leo hii sipendi kuzisikiliza hotuba za Komando kwani zinanitia simanzi kubwa wala sipendi kumwangalia popote picha zake zinapoletwa.
Hakika Kibeku alikuwa Ungo.
Wewe kijitu ukizisikia hotuba hizi lazima utatetemeka kwani wewe una nini cha kumtisha Komando?
Mabingwa wa kutengeneza filamu wa Hollywood wametengeneza movie, "David," kisa cha Mtume Daud.
Kuna kipande na Allah kakieleza kisa hiki ndani ya Qur'an pale Daud alipotoka kwenda kumkabili Jalut katika mapigano huku wote wakiangaliwa na majeshi yao.
Kisa Maarufu.
Hollywood katika ubingwa wao kipande hiki cha Daud anakwenda kupigana na Jalut wame-dramatise na kukuza kila kitu.
Kipande hiki kitakutoa machozi ukiwa utakiangalia huku unaileta ile dua ya Daud aliyokuwa anaisoma wakati anakwenda kupigana na Jalut akiwa hana silaha ila dua aliyofunzwa na Allah.
Jalut kasimama mbele yake mrefu zaidi ya futi sita na kasheheni silaha nzito na deraya mwili mzima.
Maalim Seif alimshinda Komando katika uchaguzi ule na inasemekana Maalim ameshinda kila uchaguzi yaani kawashinda marais wote wa Zanzibar aliopambananao.
Dr. Salmin anaomba dua bila shaka ya kutafuta nusra Allah avinusuru visiwa na wananchi wake na shari iliyokuwa ishasimama ikisubiri cheche ndogo kulipuka.
Dr. Salim anajua kinachomkabili Dr. Hussein Mwinyi kwani yeye kapita njia hiyo na anaijua vizuri kabisa.
Bila shaka katika dua hii yake Komando anamuomba Allah asijaalie Dr. Hussein Mwinyi akakalia kiti cha urais wa Zanzibar baada ya Wazanzibari kuuliwa.
Sote tunawajibu wa kunyonyua mikono yetu kuomba dua Allah ainusuru Zanzibar na shari ambayo tayari iko mlangoni.
Amin.View attachment 1566596
Huwezi kudhulumu haki za maelfu ya Watu kuishi kisha Mwenyezi mungu akuache tu, malipo ni hapa hapa duniani. Mjulisheni na baba yenu jiwe pia.Inawezekana kabisa hata asingekua rais, Salmin angepitia hichohicho anachopitia sasa, siri ya maisha yetu anayo mwenyezi Mungu
Sisi sote ni binadamu hakuna aliyekamilika maisha yanaweza badilika muda wowote tusihukumu tusije kuhukumiwa, wala tusimpangie Mungu
Kuna mijitu afriti inayofikiri kumuenzi baba wa taifa ni kuendelea kuwanyanyasa raia wasio na hatia Zanzibar, na tayari imeishaanza vitisho!Kwa kweli wazanzibar wamepitia mengi,umefika wakati wapewe nafasi ya kuchagua viongozi na serikali wanayoitaka hiyo ni haki yao.Uchaguzi siku zote una changamoto nyingi pande zote mbili bara na visiwani,Ingawa CCM inaonekana itaendelea kutawala lakini shauku na njaa ya mabadiriko kwenye hii nchi ni wazi.Mabadiriko yatakuja sababu ni kanuni za kimaisha vitu kubadirika ila hatujui yatakujaje na lini,ingawa dalili zipo nyingi.
Mi pia naombea amani kwa nchi yote na Zanzibar kupata utawala wanaotaka na viongozi waliowachagua.
Mnamlaumu bure mzeeHuwezi kudhulumu haki za maelfu ya Watu kuishi kisha Mwenyezi mungu akuache tu, malipo ni hapa hapa duniani. Mjulisheni na baba yenu jiwe pia.
Kila binadam atazeeka na kunyauka hiyo ni inshu ya biological. Hata maalim kazeeka sana.
Alikuwa na maneno sanamzee alisema urais sio asali kila mtu alambe[emoji23]
Mkumbusheni Dr Mwinyi, tunajua yeye ni Swala 5. Aendelee kumuogopa Mungu na akumbuke kuwa Urais unapita tu, na maisha tunapita hapa duniani. Asitamani uraisi utakao kuwa na damu na machozi ya watu wasio na hatia.Kila la heri DR. Hussein,
Hakika Mungu yuko pamoja nawe,
Dr Mwinyi tunamjua, ni muadilifu, mpole, huruma, mtu wa watu na mwenye hofu ya Mungu. Lakini uchaguzi ni suala la watu kuwa wanampenda nani zaidi. Asikubali kuingia mkenge wa kuwaumiza watu lwa matakwa ya kutawalaKila binadam atazeeka na kunyauka hiyo ni inshu ya biological. Hata maalim kazeeka sana.
Shukrani kwa bandiko lako hili, Mkuu, Mohamed Said . Mimi sina mengi zaidi nilivutiwa na sentensi yako hii, hivyo nikalazimika kwenda kutafuta baadhi ya hotuba za 'Komando' huko Youtube. Na huko nimepataLeo hii sipendi kuzisikiliza hotuba za Komando kwani zinanitia simanzi kubwa wala sipendi kumwangalia popote picha zake zinapoletwa.
Tujitegemee,Shukrani kwa bandiko lako hili, Mkuu, Mohamed Said . Mimi sina mengi zaidi nilivutiwa na sentensi yako hii, hivyo nikalazimika kwenda kutafuta baadhi ya hotuba za 'Komando' huko Youtube. Na huko nimepata
Baada ya kuitazama mpaka mwisho, nimeshangazwa kwa nini, Mkuu, atiwe simanzi na hotuba kama hizi? Ukipata nafasi, unaweza kunifafanulia hili kwa ajili ya kuboresha uwelewa wangu na wa wengine wenye mtazamo kama wa kwangu.
Natanguliza shukrani.