SI KWELI Picha ya Freeman Mbowe akiwa na Rais Samia waliyopiga Ikulu inaonesha asali nyuma

SI KWELI Picha ya Freeman Mbowe akiwa na Rais Samia waliyopiga Ikulu inaonesha asali nyuma

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Source #1
View Source #1
MADAI
Kumekuwepo na picha inayozunguka mtandaoni ikimuonesha mwenyekiti wa CHADEMA Mhe. Freeman Mbowe akizungumza na Rais Samia huku mandhari ya nyuma ya picha hiyo kukiwa na chombo chenye asali ndani yake.

Ukweli wa picha hii upoje?

D74A8180-BF60-4A22-B98B-ABAE861FF69A.jpeg


Picha inayodaiwa kuwa na chombo chenye asali


5463E756-A803-4A9B-9FE4-AF4CC2044470.jpeg

Picha halisi iliyotolewa na Ikulu
 
Tunachokijua
Picha ya tukio hili ilichukuliwa Disemba 31, 2022, wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Freeman Mbowe pamoja na Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara Ndugu. Abdulrahman Kinana wakati akipokea taarifa ya Maendeleo ya mazungumzo ya mchakato wa maridhiano ya kisiasa, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Kwa kutazama picha ya pili iliyowekwa kwenye mitandao rasmi ya kijamii ya Ikulu, hakuna chombo chenye asali kama mtoa mada alivyoelezea hivyo madai haya siyo ya kweli.
Kwa nini picha ya pamoja muda wa kuagana wanakaa mbali mbali. Ata kushikana mikono au viuno sioni
 
MADAI
Kumekuwepo na picha inayozunguka mtandaoni ikimuonesha mwenyekiti wa CHADEMA Mhe. Freeman Mbowe akizungumza na Rais Samia huku mandhari ya nyuma ya picha hiyo kukiwa na chombo chenye asali ndani yake...
Kwa hili la Jamii check JF imejiongezea heshima nyingine[emoji1545][emoji818][emoji817]
 
Tunamshukuru Kwa kufafanua na kutolea maelezo ya hizo picha kuhusu asali.

Sikubahatika kuiona hiyo picha awali lakini yeyote aliyefanya hivyo lengo itakua ni kufikisha ujumbe wa Ile dhana ya kulamba asali ambayo nayenyewe kimsingi hua sio hii asali tunayoifaham. Neno asali na picha ya asali vinawakilisha kitu kingine kabisa.
 
Back
Top Bottom