KWELI Picha ya Lionel Messi na Yamal akiwa mtoto

KWELI Picha ya Lionel Messi na Yamal akiwa mtoto

Taarifa hii imethibitika kuwa ya kweli baada ya kufanya tathmini ya kina
Source #1
View Source #1
Source #2
View Source #2
Kuna picha inasambaa ikimuonesha Messi akiwa anamuogesha Yamal wakati Yamal akiwa mtoto. Naomba kufahamu ukweli wa ile picha na ilikuwaje Messi akakatuna na Wazazi wa Yamal enzi hizo.

Mesi Lamine.jpg
 
Tunachokijua
Lamine Yamal Nasraoui Ebana ni mchezaji wa timu ya taifa ya Uhispania aliyezaliwa Julai 13, 2007. Yamal alijiunga na klabu ya Barcelona akiwa na umri wa miaka 7 kutoka klabu ya mtaani kwake CF La Torreta.

Baada ya kufanya vizuri kwenye michuano ya EURO 2024 inayoendelea Ujerumani, Lamine Yamal amezua mjadala kwenye mitandao ya kijamii kuhusu ubora wake na jinsi anavyoweza kutawala soka miaka michache ijayo.

Picha za Yamal akiwa na Lionel Messi
Usiku wa Julai 9, 2024 zilianza kusambaa picha mbili za Lamine Yamal, moja akiwa amebebwa na Lionel Messi na nyingine akiwa amekaa kwenye beseni akiogeshwa na mchezaji huyo nguli wa soka duniani.

Aidha, mmojawapo wa watumiaji wa Mtandao wa X (Ayubu Madenge), Julai 10, 2024 alichapisha ujumbe wenye ufafanuzi wa mojawapo ya picha hizo ikisema "Barcelona ilikuwa na Utaratibu wa kupiga picha na watoto kwa ajili ya Calender ya UNICEF. Mwaka 2007, Messi akiwa na Miaka 20 akapangiwa kupiga picha na mtoto mchanga wa Miezi 4 ambaye ni Lamine Yamal. Wakati huo hakuna alijua kuwa Yamal angekuja kuwa mchezaji hodari namna hii"

screenshot-2024-07-10-100059-png.3038317

Chanzo: Ayubu madenge (Mtandao wa X)

Picha hizi ni halisi?
Ufuatiliaji wa JamiiCheck umebaini kuwa picha hizi ni halisi, zilichukuliwa miezi michache baada ya kuzaliwa kwa Yamal mwaka 2007, wakati huo Messi akiwa na umri wa miaka 20.

Kwa mujibu wa mpiga picha aliyeshiriki kwenye tukio hilo, Joan Monfort, nguli wa soka duniani Lionel Messi alipiga picha na watoto wa familia kadhaa kwenye mradi wa hisani uliokuwa unasimamiwa na Shirila la UNICEF. Anafafanua kuwa zoezi hilo halikuwa rahisi maana Messi ni mtu siyezungumza sana, pia ana aibu.

Aidha, Julai 5, 2024, baba yake Lamine kwenye ukurasa wake rasmi wa mtandao wa Instagram alichapisha picha ikimuonesha Lamine akiwa kwenye beseni la bluu huku mama yake pamoja na Messi wakiwa wamemshika wakimuogesha. Picha hii iliambatana na maneno yanayosema 'The beginning of two legends'

screenshot-2024-07-10-124650-png.3038352

Chanzo: Instagram
Hoja nyingine inayothibitisha uhalali wa picha hii ni kupitia chapisho la Lamine Yamal aliloweka kwenye akaunti yake rasmi ya Mtandao wa X Julai 10, 2024, likiwa na picha akiwa amebebwa na Messi ikiambatana na maneno 'Reborn'.
Wadau hamjamboni nyote?

Picha halisi zinaongea

Ni habari za kweli mtoto lamine akiwa na miezi 6 mikononi mwa Lionel Messi.

Wazazi wa lamine wakiishi Barcelona na maisha ya hadhi ya chini walishinda bahati nasibu ya UNICEF na kupata nafasi ya kupiga picha na Lionel Messi.

Picha hiyo na kitendo hicho cha kuogeshwa na Messi ndiyo ikawa baraka kuu Kwa mtoto wao ambaye akiwa na miaka 16 TU alifunga bao muhimu lililoipeleka Hispania fainali ya Euro24
1720594294919.jpg
1720594292163.jpg
 
Screenshot_20240710-195349_Instagram.jpg
Picha inayomuonesha LIONEL MESSI akimuogesha mtoto anaedaiwa kuwa LAMINE YAMAL ni halisi.

Lamine Yamal, inasemekana asili yake ni Morocco 🇲🇦 Morocco mpo vizuri sana, moja ya timu ninayoshabikia, The Atlas

Ukija Ulaya ni Spain 🇪🇸

In South Amerikan ni Argentina 🇦🇷
 
Back
Top Bottom