Picha zinatisha; Huu ni ugonjwa gani?

Mmh, dunian kuna magonjwa mengi aisee, pole kama ndo weye unaumwaa
 
Mkuu hivi lile dawa zito kama asali likiingia matakoni si unakufa kabisa[emoji16] [emoji16] [emoji16] [emoji16] [emoji16]

Mkuu;
Kipi bora, kupona au kukatika dyudyu?? Ukishikwa kisawia huogopi dawa.
 
hujawaona ndugu yangu... Kila dizaini... Wazee vijana.... Weupe weusi... Wacha mungu vicheche... Wapole wakali n. K.... Wewe tu na roho yako.
Unahudumia mtu kama unahudumia reli ya kiwango cha kati haijalishi ni mweupe, mweusi, mzee, kijana, mcha mungu, kicheche, mpole, mkali n.k...
Halafu mara gonjwa hilo...
 
Unahudumia mtu kama unahudumia reli ya kiwango cha kati haijalishi ni mweupe, mweusi, mzee, kijana, mcha mungu, kicheche, mpole, mkali n.k...
Halafu mara gonjwa hilo...
Umeambiwa hayo ni maradhi ya zinaa mkuu? Sio maradhi ya ngono ...au ushakua kada wa chama
 
Na kwa kifupi ukitumia choo cha kukaa ambacho anakitumia huyo mgonjwa lazima ukupate hata yale maji maji yake akikuingia tu ni soo
Mkuu hapa nakuelewa sana. Na nikiongea hapa simaanishi kusikia. Nimetest hiyo kitu acha kabisa. Na niliipatia guest. Kwenye kamji kamoja kenye guest houses nyingi sana hapo bongo. Nilienda kwenye shughuli za kitaifa kurudi home sikumaliza week. Ikaanza muwasho, kipele, vipele, na mwisho madonda. Mwanzo vinaanza na kupona vyenyewe. With time vinakuwa haviponi kabisa. Asikuambie mtu. Madaktari hapa watanielewa. Na waliopitia experience. Na hapa natoa ushuhuda bila chenga. Nilicheza na hiyo ugonjwa almost two years. Ugonjwa ulianzia kweye penile ukahamia kwenye scrotal sacs. Na kwa ugonjwa huu boxer haifai. Hata kama mwanaume utavaa chupi kwa nidhamu kabisa, uweze kubeba scrotal sacs vizuri. Otherwise hutembei. Ni maisha huwezi kuyatamani. Hakuna sindano mbaya sikuchoma. Hakuna dawa mbaya ya kutibu viral na bacterial deseases sikunywa. Kuna sindano inaitwa Penadur injection niliichoma sanaa! Kwa wanoijua. Madaktari walifika mahali wakasurrender. Wakanipima ngoma mara 5 haikuonekana. Wakapima more than 60 diseases hawakuona. Hapa namaanisha hata hiyo syphillis na Herpes na ndugu zake hawakuonekana. It was realy terrible. Wakaniambia kaombewe ndio kilichobaki. Hahaaa. Ila ya Mungu mengi. Hata nilivyopona sikujua kilichoniponyesha nini. So tuache mzaha. Magonjwa haya ni hatari sana na hakika kuna umuhimu wa kuwahi hospitali mapema tuonapo dalili.

Kwa kifupi niliusoma ugonjwa nikaujua. Niliimaliza Google. Asikuambie mtu. Nilikata tamaa na maisha nikawa nasubiri kufa. Haya Magonjwa tuyasome tu humu ila yasikupate ukayachelewesha. Utavaa pedi hata kama mwanaume. Lazima uione jehanam ukiwa duniani. Nimeeleza kirefu kwa hisia sababu iliniuma nilipata ugonjwa wa zinaa bila kufanya zinaa. Tunaziamini hotel kubwa nzuri za pesa nyingi na kudhani zina afya sana . Si kweli. Afya zetu zinatunzwa na sisi wenyewe. Haijalishi umelala hotel ya hadhi kiasi gani. Kwangu mm kitanda wala washroom usiyoiswafi wewe si ya kuamini 100%. Toka wakati huo, nikisafiri nasafiri na taulo langu shuka zangu medicated soaps na detol ya maji na sabuni. Unaweza ona iliniumiza kiasi gani hata sasa siamini hotel yoyote. Mnaweza kuuliza kwani nilijuaje niliupata ugonjwa hotelini. Niliondoka nyumbani nikiwa mzima. Nimekaa hapo hotelini week 3. Nikarudi home in a week time nikaanza kuumwa. Hata hivyo kuna wakati nilitilia shaka chumba Nilicholala. Details nyingine siwezi kutoa hapa. Anyways, mnisamehe kwa maelezo mengi. Mada imenikumbusha mateso na maumivu ambayo sikuwahi kuyapata. But this is my true experience.
 
Asaidiwe dawa atumie dawa gani? Huenda hapo ni mme na msichana wake aka demu wake
 
Cku hizi hayo magonjwa hayapo, yakitokea 2 watu wanaanza medical
 
Pole sana Mkuu, na hongera kwa kupona....Nimependa ushuhuda wako wengi tutajifunza kupitia wewe.!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…