Sahihi kabisa. Moja ni jizi sugu (CWT). Hili linakula kimasihara tu 2% ya basic salary ya mshahara wa mwalimu aliyeko serikalini kila mwezi. Na hili jizi kwa miaka nenda limekuwa likilindwa na serikali ya ccm!
Kajizi kengine ni hako ka Chakuhawata. Haka ni kajizi kapya kabisa! Mana kameingia rasmi kwenye ulaji mwaka huu wa 2023 kama sijakosea. Na walau haka kajizi kapya kanapendwa na walimu walio wengi, kwa sababu kenyewe kanaiba 5000/= tu kila mwezi kwenye basic salary ya mwalimu mnyonge wa nchi hii.