Pinda, Muungano, na Hatima ya Zanzibar

Pinda, Muungano, na Hatima ya Zanzibar

Kwa wale ambao wanajua undani wa Muungano, uliosukwa na kusukika, hatimaye nchi mbili tofauti, Zanzibar na Tanganyika, zikaungana na kuwa nchi moja, Tanzania, mnamo mwaka 1964, mtajua wazi kwamba Muungano huu ulikuwa na lengo moja tu: KUILINDA ZANZIBAR dhidi ya hatari za mashambulizi ya kuvamiwa tena, na kuwa chini ya Falme za Kisultani.

Muungano huu haukuwa na faida kwa Tanganyika, kwani, hata tukiangalia Uchumi wa Zanzibar, pamoja na rasilmali zake zote, hakukuwa na (zaidi ya karafuu) zao hata moja ambalo lingeweza kusaidia kipato cha Serikali ya Muungano. Na kweli, Zanzibar, toka "iungane" na Tanganyika, imekuwa ikifaidi ruzuku kutoka Serikali ya Muungano.

Mengi (yaliyofichwa) yaliandikwa kwenye Mkataba wa Muungano, ambao mpaka leo unafanywa kuwa SIRI. Watanzania tujiulize. Hivi, kwenye "maslahi ya taifa", sisi wote tukiwa ndio wenye TAIFA, kuna SIRI ambayo hatupaswi kuijua? Hiyo SIRI imewekwa kwa manufaa ya NANI haswa?

Nawakumbuka wale WAJINGA waliotaka tuwe na Serikali tatu; Serikali ya Muungano, Serikali ya Tanganyika, na Serikali ya Zanzibar. Watu wa ajabu sana wale! Wa ajabu kweli kweli! Hivi, ka-nchi kadogo kama haka, kawe na Serikali tatu, itawezekana kweli? Yaani, tuwe na Rais wa Jamhuri ya Muungano, Rais wa Tanganyika, na Rais wa Zanzibar? Halafu tuwe na Bunge la Muungano, Bunge la Tanganyika na Bunge la Zanzibar? Halafu tuwe na Baraza la Mawaziri la Muungano, la Tanganyika, na la Zanzibar? Halafu tuwe na Wabunge, wa Muungano, wa Tanganyika, na wa Zanzibar? Itawezekana kweli, kama si ujuha, upumbavu na UHUNI?

UHUNI? Ndio! Ni UHUNI kudai Serikali tatu! Uhuni mkubwa uliokithiri na kuvuka mipaka yote ya ustaarabu.

Nchi ya watu, takriban milioni 40, ambao asilimia 70 ya watu wake ni maskini, wanaoishi vijijini. Watu hao hao, uwalipishe ushuru na kodi lukuki, kukidhi haja za Serikali tatu? Kama si uhuni, sijui ni nini?

Tuzungumzie hali halisi iliyopo kwa sasa.

Serikali mbili... nchi moja! Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Nnini maana ya Muungano? Kwa nini kuwe na Serikali mbili, ndani ya NCHI MOJA? Ndani ya Muungano kuna Watanzania, hakuna Watanganyika wala Wazanzibar. Nje ya Muungano kuna Watanganyika na Wazanzibari. Ndani ya Zanzibar, nje ya Muungano, kuna Wazazibara na Wazanzibari. Ndani ya Zanzibar, nje ya Muungano, kuna Waunguja na Wapemba! Mnayaona haya?

Serikali mbili... nchi moja! Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Haiitwi Jamhuri ile. Inaitwa Zanzibar, basi! Si Jamhuri! Anayesema inaitwa Jamhuri ya Zanzibar aje na waraka huo uliopitishwa kisheria. Kimsingi, ZANZIBAR SIO NCHI! Zanzibar ni MKOA, ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ndio maana tunasema Tanzania ina MIKOA ishirini na sita, mkoa wa mwisho ukiwa Zanzibar, ambao, ndani ya Jamhuri una Wilaya zake zinazotambulika!

Serikali mbili... nchi moja! Bunge la Muungano wa Jamhuri ya Tanzania. Baraza la Wawakilishi (na Wabunge?) la Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Baraza la Mawaziri la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Baraza la Mawaziri la Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wabunge wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

KICHEKESHO (au KILIO? Chagua moja!): Ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzanzania, kuna Wabunge wa Jamhuri na Wabunge wa Zanzibar. Wote wanapigiwa kura.... kwa hiyo, Majimbo ya Ubunge ya Zanzibar yanatambuliwa rasmi kwenye Bunge, ndio maana yanasimimamiwa (wakati wa Uchaguzi) na (hiki ni KICHEKESHO zaidi) Tume ya Uchaguzi Zanzibar. Yaani, Zanzibar ina Tume ya Uchaguzi, ambayo baadhi ya watendaji wake wako kwenye Tume ya Taifa (Jamhuri) ya Uchaguzi. Mpo hapo? Tume mbili, nchi moja. Majimbo yanatambulika na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Jamhuri), na pia yanatambulika huko Zanzibar. Lakini (KICHEKESHO ZAIDI) sijaona, sijasikia, Mbunge wa Jamhuri akaingia kwenye Baraza la Wawakilishi la Zanzibar kuiwakilisha Jamhuri! Hilo HALIPO! Ila, wao wanaingia kwenye Bunge la Jamhuri! Nadhani mmenielewa!

Haya. Turudie.

Rais wa Jamhuri. Rais wa Zanzibar.
Bunge la Jamhuri. Bunge la Zanzibar.
Baraza la Mawaziri la Jamhuri. Baraza la Zanzibar.
Wabunge wa Jamhuri. Wabunge na Wawakilishi wa Zanzibar.
Serikali ya Jamhuri. Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Jeshi la Polisi la Tanzania. Oh, hakuna Jeshi la Polisi la Zanzibar.
Jeshi la Wananchi la Tanzania. Oh, HAKUNA Jeshi la Wananchi la Zanzibar.
Jeshi la Kujenga Taifa la Jamhuri. Oh, LIPO Jeshi la Kujenga Uchumi la Zanzibar (JKU).
Oh, HAKUNA Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo cha Jamhuri. Oh, lakini KIPO Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo (KMKM) cha Zanzibar.

Tathimini yangu?

Muungano huu haufai. Ni bora tuwe na Serikali Moja! Yeyote yule aliyeko Zanzibar aweze kugombea nafasi yoyote ile kwenye Uongozi, ndani ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Sitaki, sioni haja ya kuwa na Serikali Mbili ndani ya Muungano. Hakuna faida wala haja. Serikali moja. Hakuna haja ya kuwa na Bunge la Jamhuri na Baraza la Wawakilishi. Ina maana kwamba kuna Sheria za Muungano na Sheria za Zanzibar? Sasa nini haswa faida na haja ya kuwa na Muungano?

Tuache unafiki, tuanze kuambizana ukweli.

Kama Zanzibar haitaki Muungano, basi, wapige kura ya maoni kujitoa. Wakijitoa, vikosi vya Jeshi la Polisi na Jeshi la Wananchi viondolewe mara moja huko Zanzibar. Vijana wetu warudi nyumbani! Kama hawataki Muungano, tunafuta mara moja ruzuku wanayoipata kwenye Bajeti yao. Mamlaka ya Mapato ya Tanzania ifunge virago vyake huko Zanzibar. Ukitaka kwenda Zanzibar, unagonga passport yako, unalipia VISA kama vile unakwenda nchi nyingine. Na wao pia, wakija Tanzania, walipie VISA. Wazanzibari wote waliopo Tanzania bara waombe na kulipia vibali vya makazi. Ndicho wanachokitaka?

Tuache unafiki, tuambizane ukweli.

Serikali Moja! Nchi Moja! Bendera Moja! Wimbo MMOJA wa Taifa.

Hakuna Bendera ya Jamhuri kisha kuna Bendera ya Zanzibar. Hakuna Wimbo wa Taifa kisha kuna Wimbo wa Taifa wa Zanzibar! ZANZIBAR SIO NCHI!

Namuunga mkono kwa dhati kabisa, Waziri Mkuu, Mhe. Pinda Peter Mizengo Kayanda, kwamba, SERIKALI IWE MOJA, kwani hii ni NCHI MOJA, inayojulikana kwa jina la, JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA!

IDUMU JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA!
MUNGU IBARIKI TANZANIA.
MUNGU WABARIKI WATANZANIA NA VIONGOZI WAKE!
MUNGU TULINDE WATANZANIA!
MUNGU TUEPUSHE NA UFISADI!

./Mwana wa Haki

P.S. Bado nitaendelea kusema. Mwenye kukerwa, aende kujirusha FERI! Au Bahari ya Hindi kama Magogoni hapatoshi!


Huna jipya au mapepe ya Gin&tonic bado yamo kichwani ?
 
Sasa kwanini CCM na serikali yake wanaushikilia Muungano? Z'bar wapewe Independence yao wanayoitaka.
 
huyu mgala anasema nini hajui alisemalo hajijui kama kavaa nguo au yuko uchi naona mataptapu yanamuendesha ovyo
 
Babylon

Kwa mtu ambaye amejiunga humu ndani Thursday, February 2009, kweli naona bado huelewi maana halisi ya forum hii.

Nimeongea kwa hoja. Tetea hoja yako, si kusema kwamba nina "Gin & Tonic" kichwani.

Suala la Muungano si la kukejeli kama unavyofikiria. Unanikejeli mimi, inakusaidia nini? Zungumza kwa hoja yako. Hapa ni pa kujadiliana, si kuhasimiana ndugu. Tutasonga mbele kwa mtaji huo?

./Mwana wa Haki
 
Nyinyi munaona kuwa kauli ya Mizengo Pinda ni ya maana sana naona munajipa taabu sana. Nawashangaa wengine kusema eti muungano huu ni mfano kwa dunia. Ni kweli ni mfano kwa dunia kwani hakuna hata nchi moja iliokubali kuwa na muungano kama huu. Hata sis wazanzibari ni watu ambao tunatawaliwa ki,mabavu. Kama mujusavyo, hatuna haki ya kuiseme nchi yetu. Nyinyi watu wabara ndio mulioshadidia muungano. Sisi wazanzibari hatuna haja kuambiwa na Pinda namna ya kujitawala. Wala musiwe na wasiwasi kuwa eti muungano ukivunjika tutapata hasara. La hasha, hasara kutakuwa nayo nyinyi kwasababu mumezoweya vya bure. Sisi wazanziabri asili yetu ni watenda kazi na tunweza kuendesha taifa letu bila nyinyi.HATUTAKI MUUNGANO>
 
rev_revised.jpg




In this picture, standing from left to right are: Muhammed Abdulla, Abdulla Mfarinyaki, Khamis Darwesh, Said Idi Bavuai, Abdullah Said Natepe, Hamid Ameir, Hafidh Suleiman, Pili Khamis, and Said wa Shoto. Seated from left to right are: Ramadhan Haji, John Okello, and Seif Bakari.
According to a list published in a book (Zanzibar Dola, Taifa na Nchi Huru) by Dr. Yussuf S. Salim of the Zanzibar Center of Human and Democratic Rights based in Denmark, those not seen in this picture are Yusuf Himid and Khamis Hemedi. Based on our recollection, Yusuf Himid became the first leader of the Nyuki Brigade, the Zanzibar's division of the Tanzania People's Defence Forces (TPDF). Upon his death in early 80's, Khamis Hemedi succeeded him in the same capacity.
The Committee of Fourteen was essentially composed of members of the Afro Shirazi Youth League (ASYL), the youth branch of the Afro Shirazi Party (ASP).


(Kutoka http://www.zanzinet.org/zanzibar/history/wanamapinduzi_new.html )


Katika hiyo kamati ya mapinduzi mmisheni alikuwa ni mmoja, John Okello. Itakuwaje aliweza kuwarubuni wenzake wote waliokuwa waislamu kuwafanyia maovu waislamu wenzao? Ingawa Okello alisema wazi kuwa anaamini kuwa alitumwa na Mungu wake kuwakomboa waafrika kutoka kwa waarabu, kwa nini hao wengine wasiungane na wenye dini wenzao waliokuwa waarabu kumpinga? Kilicho wazi ni kuwa ingawa alisukumwa na udini lakini kilichompa mafanikio ni weusi wake na sio umisheni wake. Waliomuunga mkono walifanya hivyo kutokana na kuweka mbele solidarity ya rangi ya ngozi juu ya dini. Solidarity iliyotakana na common history ya utumwa chini ya waarabu. Utumwa uliokomeshwa na wamisheni lakini uliendelezwa katika mfumo wa kitabaka kati ya waungwana na watwana. Watwana wakiwa wenye rangi nyeusi. Udhalimu ambao ulithibitishwa (kwa matazamo wao) katika chaguzi za mwaka 1961 na 1963 ambapo chama cha watu weusi, ASP, kilipokonywa ushindi pamoja na kupata kura nyingi kuliko ZNP/ZPPP! Mwaka 1961 watu zaidi ya 68 waliuawa baada ya uchaguzi. Okello alikuwa Katibu wa ASP Pemba, akitokea Kenya na si Tanganyika. Yeye aliona kuwa anaongoza vita dhidi ya waarabu, waliowatendedea dhulma weusi wenzake. Hakuongoza mapambano dhidi ya waislamu kama wengine wanavyotaka kupotosha! Angefanya hivyo, asingefanikiwa hasa ukizingatia idadi ya waislamu ukilinganisha na wamisheni huko Zanzibar na Pemba.



Vijana wa kiarabu waliokuja kuunga mkono mapinduzi walifanya hivyo kutokana na mwamko wao wa kisiasa wa mlengo wa kushoto na kuona mapinduzi kama sehemu ya class wars aliyoizungumzia Marx. Kudai kuwa udini, hususan umisheni, ndiyo uliokuwa nyuma ya mapinduzi ni kutowatendea haki wazalendo waliojiunga na John Okello. Ni wao, kwa sababu ya uzalendo wao, waliomtumia Okello na si vice versa. Ndio maana baada ya kumtumia walimtema bila kusita. Na mmoja aliosaidia katika kumuondoa alikuwa ni mmisheni mwenzake, Julius Kambarage Nyerere.


Nchi za magharabi zilihofia mapinduzi ya Zanziba si kwa sababu za kidini bali ki-itikadi. Mapinduzi yalitokea wakati vita baridi imepamba moto. Nikita S Khrushchev aliishaahidi kuzifunika nchi za magharibi. Ni miaka miwili tu kabla alijaribu kuweka missile Cuba. Ni miaka mitano tu kabla, Fidel Castro na Che waliisha itoa kamasi Marekani. Vita ya Vietnam ilikuwa inafukuta. Ni miaka mitatu tu baada ya Yuri Gagarin kwenda kwenye anga za juu na kurudi. Uwezekano kuwa watu wa mlengo wa kushoto wanashinda vita vya ki-itikadi ulikuwa mkubwa. masuala ya kidini hayakuwa na nafasi. Tusipende kuandika upya historia ili kujenga hoja katika imani zetu za wakati huu.



Vile vile, tunakosea tunapodhani kuwa sababu kubwa ya Muungano ilikuwa ni uoga wa kurudi kwa utawala wa kisultan. Karume aliwahofia zaidi vijana wakina Babu na Sheikh Kassim Hanga kuliko hao wakina Jamshid. Hawa walikuwa wana mapinduzi wa dhati na nchi za magharibi zilihofia Zanzibar kugeuzwa Cuba nyingine na si vinginevyo. Hii ilithibitishwa pale nchi ya Zanzibar na Pemba ilipokuwa ya kwanza DUNIANI kutambua Jamhuri ya Kidemokrasia ya Ujerumani na ya Korea Magharibi. Wakina Babu na Hanga hawakuwa waislamu wenye msimamo mkali bali wanamapinduzi wa kikomunisti. Karume alihofia kuwa hawa wanamapinduzi wangeweza kumtoa kwenye madaraka hasa ukizingatia kuwa walikuwa na mvuto zaidi yake. Na Nyerere nae hakuwa na imani na wakomunisti. Hasa baada ya Tanganyika Rifles ku-mutiny wakati huo huo wa Mapinduzi! Ikumbukwe kuwa askari walioongoza machafuko hayo walionekana kumkubali zaidi Oscar Kambona, ambae wakati ule alionekana kuwa ni mwanamapinduzi zaidi kuliko Julius. Ni hofu ya mapinduzi kutoka ndani ndiyo iliyopelekea Muungano. Jamshid aliomba msaada kutoka Tanganyika na Kenya na si Oman. Jamshid alikimbilia kwanza Tanganyika halafu Uingereza na si Oman. Waarabu hawakuwa na ubavu wakati ule. Na kila mmoja alijua hilo.


Amandla........
 
Last edited:
Pinda: Usifanye mizengwe ya kupindisha ukweli
ban.znz.jpg


Salim Said Salim

amka2.gif

BINADAMU si malaika. Kuna kipindi huteleza na kufanya makosa. Anapofanya hivyo binadamu wenzake wenye utu, wema na hisani hutakiwa kumuonea huruma mwenzao aliyeanguka kwani kila mmoja wao huenda siku moja naye akateleza.
Waswahili wanasema mwenzako akianguka msaidie kumuokota aweze kusimama, ili nawe utapoanguka upate kiumbe wa kukuokota.
Lakini pale unapoona mtu anajiangusha kwa makusudi, basi ni vyema ukamueleza waziwazi kuchoshwa kwako na kumuokota, kwa vile kuna kipindi nguvu za kufanya hivyo zitakusekana na utakapojitahidi misuli huenda ikagoma kufanya kile unachokitaka.
Hivi karibuni limekuwa ni jambo la kawaida au mara kwa mara kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kuteleza, kuanguka au kujiangusha labda akiamini kila mizegwe anaweza kufanya kwa kutoa kauli za ajabu ambazo mimi ninavyoziona hazina kichwa wala miguu.
Baadhi ya wakati hujiuliza hivyo kweli huyu Waziri Mkuu wetu ni Mtanzania? Au ndiyo anauruka ukweli kwa kuwa anatoka Rukwa? Au ndiyo ni katika jitihada zake za kupindisha mambo ili mizengwe ionekane kweli?
Nimekuwa karibu na viongozi wengi wa nchi hii, wa Bara na Visiwani, kwa miaka mingi, tangu Waziri Mkuu akiwa shule. Tumezungumza mengi na nimewasikia wakizungumza mengi, baadhi yao ya siri. Lakini kama yupo kiongozi anayenishangaza ni huyu Mizengo Pinda ambaye ninaona anafanya mizengwe na kupindisha mambo.
Hivi karibuni amejibu hoja za Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi waliokuwa wakisema hawataki tena kuona suala la mafuta kuwa la Muungano. Kauli hii haikumfurahisha na kuwaeleza waliotamka hayo kuwa wanafanya chokochoko.
Si hayo tu, Mizengo Pinda alifanya mizengwe ya aina yake na kutoa kauli ambayo hata siku moja sijawahi kuisikia kutoka kwa kiongozi yeyote wa juu wa nchi hii. Nayo ni kusema Muungano ukivunjika Zanzibar ndiyo itakayopata hasara. Wapi alipata ujabari wa kutoa kauli hii, sijui. Kama alifanya utafiti ni vema pia akatueleza.
Masikini Pinda anapindisha mambo. Suala hapa ni kwa Zanzibar kukataa mafuta kuwa suala la Muungano na kudai kuwa liliingizwa katika orodha ya mambo ya Muungano kinyemela. Kama madai haya ni sahihi au upotoshaji ni suala la mjadala na kujengewa hoja yenye maelezo ya kina.
Ni vema tukaambiwa kuwa Wawakilishi wa Zanzibar hawana haki kusema hayo kikatiba. Kama ndiyo hivyo Pinda aeleze kuwa Wazanzibari, pamoja na Wawakilishi wao hawana haki ya kutoa maamuzi juu ya masuala ya Muungano.
Anachoamini Pinda - sijui kapata wapi takwimu za kutoa kauli hiyo - kuwa Zanzibar ndiyo inayofaidika zaidi kwa kuwapo kwa Muungano na ukivunjika hasara kubwa itawaendea watu wa visiwani.
Naamini Pinda ndiye aliyepata hasara kwa vile hazijui hisia za Wazanzibari juu ya namna Muungano unavyoendeshwa. Kwa taarifa yake Wazanzibari hawakushirikishwa (hajashauriwa) ulipoundwa.
Kwa taarifa yake Wazanzibari wengi, bila kujali kama ni wanachama wa CCM au CUF, hawaridhiki na shughuli za Muungano zinavyoendeshwa. Wapo wanaoamini kwamba Muungano, hasa wa vyama vya ASP na TANU, ndiyo uliowaletea balaa kwa vile hata viongozi wana-CCM wa visiwani huona wanafaa kuongoza Zanzibar huwekwa upande na Bara kuwachagulia watu wa Visiwani viongozi wa kuongoza.
Ni vizuri kama Pinda hajui mambo yanavyopindishwa kufikia hali hii, apitie kumbukumbu za vikao vya CCM, hasa wakati wa kuelekea kwenye uchaguzi.
Suala la mafuta na hizo chokochoko za Muungano ambazo Pinda anazizungumzia hazitoi taswira yoyote ile nyingine isipokuwa uwepo wa mgogoro wa katiba. Wazanzibari wanataka suala hili liwe chini ya mamlaka yao kama ilivyo kwa dhahabu na almasi kwa Bara, na hili ndio ningelimtarajia Waziri Mkuu kulizungumzia na si kupindisha mambo.
Kama walichofanya Wawakilishi ni dhambi, kwa nini haikuwa dhambi kwa Bara kufanya madini yake si ya Muungano? Au Zanzibar haina haki kudai kumiliki mafuta yaliyopo kwenye ardhi na bahari yake?
Kutaka mafuta yawe chini ya mamlaka ya Zanzibar ni kutaka kuvunja Muungano, lakini kwa dhahabu na almasi kuwa ya Bara si kuvunja bali kuimarisha Muungano. Makubwa haya, labda kama kule Rukwa ndivyo wanavyoelewa mantiki ya aina hii.
Hili Pinda analazimika kulitolea maelezo na si kupindisha mambo na kutufanyia mizengwe kwa kutoa kauli za vitisho na kusimanga (kunyanyapaa) watu. Wazanzibari hawataki kuabudiwa, lakini wanataka kuheshimiwa. Wao ni wadau wa Muungano na wanayo haki ya kutoa mawazo na maamuzi.
Suala la nani anafaidika zaidi na Muungano ni zito, refu na pana. Jawabu lake halipatikani kwa mizengwe, propaganda, kwa kauli au kupindisha mambo. Ni suala linalohitaji utafiti wa kina.
Lilio muhimu ni kukubali kwamba Muungano sasa unapanda mwamba na ukifanyiwa mchezo utazama. Hii ni kwa sababu Wazanzibari wanaamini hisia zao na maamuzi yao hayatiliwi maanani na watu kama Mizengo Pinda. Badala yake wanasukumiwa makombora na kushutumiwa kuwa wachochezi kama vile hawana haki ya kutoa maoni au kufanya maamuzi juu ya mwenendo wa Muungano.
Wakati umefika kwa kila upande wa Muungano kuheshimu kauli na mawazo ya upande wa pili. Wazanzibari wamesema si mara moja wala mbili, hawataki suala la mafuta liwe la Muungano kama ilivyo kwa almasi na dhahabu na madini mengine.
Kwa nini ionekane kuwa nongwa na kufuru? Kama kuvunjika kwa Muungano kutakuwa na hasara zaidi kwa Zanzibar kwa nini tusianzie basi na hasara kuonekana kwa hili suala mafuta ili tuone hasara itayopata Zanzibar?
Tukitaka au tusitake huu Muungano una matatizo na hata Pinda akijaribu kuupindisha ukweli matataizo yataendelea kujitokeza. Njia pekee ya kupata ahueni ni kwanza kukubali ukweli kwamba upo mgogoro na sio kutoa kauli za kutishana.
Zama za kutishana zilishapita, sasa ni zama za ukweli na uwazi, Pinda hata atumie vitisho vya aina gani hawezi kulipindisha kwani wakati wa kufanya hivyo umepita.
Watanzania tuamke. Muungano wetu una matatizo na wakubwa wanaonekana hawataki kuyaona. Tuwafumbue macho na tuwatoe tongo zinazowaziba macho, kama si kwa mikono basi kwa kuwafanyia upasuaji.
Jahazi letu linakwenda mrama na tuliowapa unahodha wa kuliongoza katika safari yetu, ambayo sasa imekumbwa na dhoruba wanaonekana hawataki au hawana ustadi wa kulivusha jahazi hili salama katika dhoruba hii. Kidumu Chama Cha Mapinduzi, Idumu CUF. Idumu CHADEMA. Idumu NCCR-Mageuzi. Idumu TLP na vidumu vyama vingine vyote vya siasa. Wadumu wa Tanzania - waliopo Bara na wale wa Visiwani. Tanzania ni moja lakini ni sehemu mbili – Bara na Visiwani - fikra nyingi na vyama vingi vya siasa. Tuache kupindisha mambo na badala yake tujitahidi kuyaweka sawa kwa hekima na busara na sio vitisho kama vya Mizengo Pinda.
 
Rejea. Hata "Mapinduzi ya Zanzibar" ambamo SMZ inatokana, hawakuyafanya. Walisepa. Wakamwachia Tito Okello (Mganda) aliyejiita baadaye "field marshall" na genge lake, wakachapa kazi, wakamchimba mkwara Sultani mpaka akatema nchi. Jamaa hao wakakwea viboti, wakapiga makasia kurejea kisiwani, wakachukua "credit".

Talking, talking, talking cheap. Walete mswada kurekebisha vifungu vya katiba. Yaani wanapiga kelele ili Bara wawabadilishie vifungu.

Nimeshasema huko nyuma, kelele hizi ni gia za uchaguzi 2010. Ngoja upite. Kimyaa.

Wewe umezongwa na MOVIES? Hivyo kwa akili yako kubwa unaamini hilo? Unamaana huyo "Mr Bond" wako alipindua sinle handed? Wacha porojo Bana!
 
Ngekewa unafanya kosa kumuona Pinda peke yake ndiye mkosaji. Lugha za kibabe hazikuanza kwake. Maneno kama 'kutingisha kiberiti n.k' yote yalitokea visiwani. Hivi karibuni pamekuwa na ushindani wa kuweka visheria kandamizi za kuwabana wanaotoka bara huko visiwani. Sheria zinazohusu ajira, haki ya kumiliki ardhi n.k. zimewekwa katika hali ya kumfanya mtu wa bara aonekane sawa na mKenya na wengine. Mfano mwingine ni lugha ya kibabe inayotumika katika suala la mafuta. Mnachosema wenzetu ni kuwa, mmeishaamua basi. Hamna mjadala! Hii kweli ni haki katika nchi inayodai kuwa ni ya Muungano?

Mimi natofautiana na Pinda katika imani yake ya kuwa serikali moja ni suluhisho. Mimi nitawashangaa sana wazanzibari kama watakubali kugeuzwa kuwa mkoa katika nchi ya Tanzania. Tukilazimisha hilo ndio tutawakimbiza hata wale ambao wangependa Muungano. Nchi zote zilizolazimisha kufanya hivyo zimeishia pabaya ( Ethiopia, Yugoslavia, USSR n.k.).

Vile vile sidhani kuwa serikali tatu ni suluhisho. Kutokana na tofauti ya uchumi, ukubwa wa nchi, idadi ya watu, maendeleo kati ya Zanzibar na Bara, watu wa bara watashawishika kutochangia katika hiyo Federal government na hivyo kuipeleka kaburini. Mfano ni kifo cha Jumuia ya Afrika Mashariki.

Kwa mawazo yangu, mfumo uliopo sasa wa serikali mbili ndio pekee ambao unaweza kuwa sustainable. Lakini ili iwe hivyo, itabidi kuwa masuala yanayohesabika kama ya muungano yapunguzwe hadi yabakie yale ambayo ni basic ( k.m. Mambo ya nje, Ulinzi na Hazina). Hatuwezi kujiita nchii moja tukiwa na balozi tofauti, majeshi tofauti na sarafu tofauti. Hayo mengine ( madini, elimu, bandari, uvuvi, kilimo, afya n.k.) kila nchi ijisimamie. Kwa hali hii, nchi ya Zanzibar iwe na uwakilishi mdogo katika Bunge la Muungano maana masuala mengi yatahusu bara na si visiwani. Ila katika hayo masuala machache ya Muungano yaliyobaki, nchi zote mbili ziwe na uwakilishi kwenye hizo wizara. Uwakilishi huu si lazima uwe based kwenye idadi ya watu bali uipe kila nchi uwezo wa kukataa jambo ambalo halikubaliani nalo. Lakini ukweli kuwa Bara ndiyo mhimili mkuu wa masuala yote ya Muungano ni lazima utambulike. Bara ni lazima ikubali kubeba mzigo mkubwa wa kuendesha shughuli za serikali ya Muungano na Zanzibar lazima ikubali kuwa kwa kufanya hivi inastahili haki zaidi. Mfano ni nchi ya Greenland na Denmark. Sasa, kama hapo baadae nchi ya Zanzibar itaamua kujitoa pasiwe na pingamizi. Na hivyo hivyo kwa nchi ya Tanzania ikiamua kuwa haihitaji zanzibar. Muungano ni lazima ukubali uwezekano wa kutengana. Kwa kufanya hivyo kutaupa legitimacy maana utakuwa wa hiari na si wa kulazimishana.

Amandla........
 
Kwa wale ambao wanajua undani wa Muungano, uliosukwa na kusukika, hatimaye nchi mbili tofauti, Zanzibar na Tanganyika, zikaungana na kuwa nchi moja, Tanzania, mnamo mwaka 1964, mtajua wazi kwamba Muungano huu ulikuwa na lengo moja tu: KUILINDA ZANZIBAR dhidi ya hatari za mashambulizi ya kuvamiwa tena, na kuwa chini ya Falme za Kisultani.

Muungano huu haukuwa na faida kwa Tanganyika, kwani, hata tukiangalia Uchumi wa Zanzibar, pamoja na rasilmali zake zote, hakukuwa na (zaidi ya karafuu) zao hata moja ambalo lingeweza kusaidia kipato cha Serikali ya Muungano. Na kweli, Zanzibar, toka "iungane" na Tanganyika, imekuwa ikifaidi ruzuku kutoka Serikali ya Muungano.

Mengi (yaliyofichwa) yaliandikwa kwenye Mkataba wa Muungano, ambao mpaka leo unafanywa kuwa SIRI. Watanzania tujiulize. Hivi, kwenye "maslahi ya taifa", sisi wote tukiwa ndio wenye TAIFA, kuna SIRI ambayo hatupaswi kuijua? Hiyo SIRI imewekwa kwa manufaa ya NANI haswa?

Nawakumbuka wale WAJINGA waliotaka tuwe na Serikali tatu; Serikali ya Muungano, Serikali ya Tanganyika, na Serikali ya Zanzibar. Watu wa ajabu sana wale! Wa ajabu kweli kweli! Hivi, ka-nchi kadogo kama haka, kawe na Serikali tatu, itawezekana kweli? Yaani, tuwe na Rais wa Jamhuri ya Muungano, Rais wa Tanganyika, na Rais wa Zanzibar? Halafu tuwe na Bunge la Muungano, Bunge la Tanganyika na Bunge la Zanzibar? Halafu tuwe na Baraza la Mawaziri la Muungano, la Tanganyika, na la Zanzibar? Halafu tuwe na Wabunge, wa Muungano, wa Tanganyika, na wa Zanzibar? Itawezekana kweli, kama si ujuha, upumbavu na UHUNI?

UHUNI? Ndio! Ni UHUNI kudai Serikali tatu! Uhuni mkubwa uliokithiri na kuvuka mipaka yote ya ustaarabu.

Nchi ya watu, takriban milioni 40, ambao asilimia 70 ya watu wake ni maskini, wanaoishi vijijini. Watu hao hao, uwalipishe ushuru na kodi lukuki, kukidhi haja za Serikali tatu? Kama si uhuni, sijui ni nini?

Tuzungumzie hali halisi iliyopo kwa sasa.

Serikali mbili... nchi moja! Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Nnini maana ya Muungano? Kwa nini kuwe na Serikali mbili, ndani ya NCHI MOJA? Ndani ya Muungano kuna Watanzania, hakuna Watanganyika wala Wazanzibar. Nje ya Muungano kuna Watanganyika na Wazanzibari. Ndani ya Zanzibar, nje ya Muungano, kuna Wazazibara na Wazanzibari. Ndani ya Zanzibar, nje ya Muungano, kuna Waunguja na Wapemba! Mnayaona haya?

Serikali mbili... nchi moja! Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Haiitwi Jamhuri ile. Inaitwa Zanzibar, basi! Si Jamhuri! Anayesema inaitwa Jamhuri ya Zanzibar aje na waraka huo uliopitishwa kisheria. Kimsingi, ZANZIBAR SIO NCHI! Zanzibar ni MKOA, ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ndio maana tunasema Tanzania ina MIKOA ishirini na sita, mkoa wa mwisho ukiwa Zanzibar, ambao, ndani ya Jamhuri una Wilaya zake zinazotambulika!

Serikali mbili... nchi moja! Bunge la Muungano wa Jamhuri ya Tanzania. Baraza la Wawakilishi (na Wabunge?) la Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Baraza la Mawaziri la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Baraza la Mawaziri la Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wabunge wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

KICHEKESHO (au KILIO? Chagua moja!): Ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzanzania, kuna Wabunge wa Jamhuri na Wabunge wa Zanzibar. Wote wanapigiwa kura.... kwa hiyo, Majimbo ya Ubunge ya Zanzibar yanatambuliwa rasmi kwenye Bunge, ndio maana yanasimimamiwa (wakati wa Uchaguzi) na (hiki ni KICHEKESHO zaidi) Tume ya Uchaguzi Zanzibar. Yaani, Zanzibar ina Tume ya Uchaguzi, ambayo baadhi ya watendaji wake wako kwenye Tume ya Taifa (Jamhuri) ya Uchaguzi. Mpo hapo? Tume mbili, nchi moja. Majimbo yanatambulika na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Jamhuri), na pia yanatambulika huko Zanzibar. Lakini (KICHEKESHO ZAIDI) sijaona, sijasikia, Mbunge wa Jamhuri akaingia kwenye Baraza la Wawakilishi la Zanzibar kuiwakilisha Jamhuri! Hilo HALIPO! Ila, wao wanaingia kwenye Bunge la Jamhuri! Nadhani mmenielewa!

Haya. Turudie.

Rais wa Jamhuri. Rais wa Zanzibar.
Bunge la Jamhuri. Bunge la Zanzibar.
Baraza la Mawaziri la Jamhuri. Baraza la Zanzibar.
Wabunge wa Jamhuri. Wabunge na Wawakilishi wa Zanzibar.
Serikali ya Jamhuri. Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Jeshi la Polisi la Tanzania. Oh, hakuna Jeshi la Polisi la Zanzibar.
Jeshi la Wananchi la Tanzania. Oh, HAKUNA Jeshi la Wananchi la Zanzibar.
Jeshi la Kujenga Taifa la Jamhuri. Oh, LIPO Jeshi la Kujenga Uchumi la Zanzibar (JKU).
Oh, HAKUNA Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo cha Jamhuri. Oh, lakini KIPO Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo (KMKM) cha Zanzibar.

Tathimini yangu?

Muungano huu haufai. Ni bora tuwe na Serikali Moja! Yeyote yule aliyeko Zanzibar aweze kugombea nafasi yoyote ile kwenye Uongozi, ndani ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Sitaki, sioni haja ya kuwa na Serikali Mbili ndani ya Muungano. Hakuna faida wala haja. Serikali moja. Hakuna haja ya kuwa na Bunge la Jamhuri na Baraza la Wawakilishi. Ina maana kwamba kuna Sheria za Muungano na Sheria za Zanzibar? Sasa nini haswa faida na haja ya kuwa na Muungano?

Tuache unafiki, tuanze kuambizana ukweli.

Kama Zanzibar haitaki Muungano, basi, wapige kura ya maoni kujitoa. Wakijitoa, vikosi vya Jeshi la Polisi na Jeshi la Wananchi viondolewe mara moja huko Zanzibar. Vijana wetu warudi nyumbani! Kama hawataki Muungano, tunafuta mara moja ruzuku wanayoipata kwenye Bajeti yao. Mamlaka ya Mapato ya Tanzania ifunge virago vyake huko Zanzibar. Ukitaka kwenda Zanzibar, unagonga passport yako, unalipia VISA kama vile unakwenda nchi nyingine. Na wao pia, wakija Tanzania, walipie VISA. Wazanzibari wote waliopo Tanzania bara waombe na kulipia vibali vya makazi. Ndicho wanachokitaka?

Tuache unafiki, tuambizane ukweli.

Serikali Moja! Nchi Moja! Bendera Moja! Wimbo MMOJA wa Taifa.

Hakuna Bendera ya Jamhuri kisha kuna Bendera ya Zanzibar. Hakuna Wimbo wa Taifa kisha kuna Wimbo wa Taifa wa Zanzibar! ZANZIBAR SIO NCHI!

Namuunga mkono kwa dhati kabisa, Waziri Mkuu, Mhe. Pinda Peter Mizengo Kayanda, kwamba, SERIKALI IWE MOJA, kwani hii ni NCHI MOJA, inayojulikana kwa jina la, JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA!

IDUMU JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA!
MUNGU IBARIKI TANZANIA.
MUNGU WABARIKI WATANZANIA NA VIONGOZI WAKE!
MUNGU TULINDE WATANZANIA!
MUNGU TUEPUSHE NA UFISADI!

./Mwana wa Haki

P.S. Bado nitaendelea kusema. Mwenye kukerwa, aende kujirusha FERI! Au Bahari ya Hindi kama Magogoni hapatoshi!

Ahsante sana kwa utungo wako mrefu wenye baadhi ya ukweli na upotoshaji lakini pengine huu ndio uelewa wako. La pili ni kukupa hongera kwa maoni yako na ninakubali kuwa ukiwa mdau wa suala hili una haki kutowa maoni yako.
Kuhusu suala la kusudi hasa la Muungano nafikiri umekosea. Kwani aliyeenda kwa mwenziwe ni nani , Karume au Nyerere? Ukishapata jawabu ndio utafahamu kuwa nani alieuza hiyop idea ya Muungano kwa mwenziwe na kuona kama kweli Zanzibar ilitaka Muungano huo ili kulindwa. Ushahidi mwingi umeshatolewa kuonyesha nini madhumuni na lengo la kumtega Karume aingie kwenye Muungano huo.
Kuhusu uchumi wa Zanzibar, Zanzibar haiukuwahi kuwa na uchumi dhaifu kiasi cha kuifanya Zanzibar kuutegemea Muungano. Unahitaji kuwa na umri na uelewa sahihi ili kuelewa namna nchi mbili hizi zilivyokuwa zikiendeshwa kabla ya kufa kwa Karume. Zanzibar ikijitegemea yenyewe kwa kila kitu na kejeli ya huyo Nyerere ilkuja pale tu baada ya kufa kwa Karume.
Zanzibar na Bara zilikuwa kama nchi mbili tofauti ndani ya Muungano huu na hilo halikumfanya Nyerere aseme chochote hadi pale alipomlaghai Jumbe na kukivunja ASP. Wakati ule si Polisi si Jeshi lilikuwa ni la Wazanzibari wenyew watupu na Zanzibar haikuhitaji KITU CHOCHOTE kutoka Bara. Hiyo unayoiita uchumimwa Karafuu ulitosha hata kutowa misaada kwa Bara. Silaha zilizokuwa zikitumika Zanzibar zikinunuliwa na serikali ya Zanzibar sasa unaposema suala la kulindwa hapo linakujaje?
Ama suwala la Uwakilishi na Bunge huo ni mfumo mlioubuni nyie ili ionekane kuwa kuna uwakilishi wa zanzibar katika Bunge. Ukweli wenyewe ni kuwa Zanzibar hainufaiki na shughuli za Bunge la Muungano kwani tangu lini ukaona Bunge likazungumzia suala la Zanzibar? Hata zile sehemu zilizokubaliwa kwa Muungano Zanzibar hainufaiki nazo. Chukuwa mfano wa suala la OIC, Zanzibar kama Zanzibar ikijiunga na OIC Bara inakosa nini? Kama suala la dini basi pigeni marufuku kuweko kwa kadhi na ofisi ya Mufti. Vitu hivyo vipo Zanzibar na tunajuwa kuwa hivyo ni vyombo vya dini (uislamu). Hamjafanya hivyo kwani havikudhuruni nyie Bara kuwepo kwao. Kwa mantiki hiyo hiyo Zanzibar kujiunga OIC hakukudhuruni nyie kidini lakini kutakudhuruni nyie KILENGO. Zanzibar ikisaidiwa itajikwamua kiuchumi nahilo hamlitaki . Sasa niambie faida gani Zanzibar inapata katika chombo kama hichi (MAMBO YA NJE) kama chombo cha Muungano?
Kuhusu mfumo wa Serikali, pia una uhuru na mawazo wewe na Pinda wa kutaka Serikali moja lakini haki yenu isisahau haki ya Wazanzibari kama sehemu moja ya Muungano ya kutaka kuona kuwa Serikali ya Tanganyika iache kujificha ndani ya ile ya Muungano badala yake tuwe sawaw kuweni na serikali yenu )Uone kama Wazanzibari wataingia humo) na tuwe na ile ya Wazanzibari(isiyo na wabara kama ilivyo) na tukutane kwente Muungano.
Hili lilikwishapendekezwa na Wasomi wenu mnaowaamini only kupingwa na vichwa ngumu wa akina Nyerere kwa kuona kuwa kutakwenda tofauti na malengo ya kuikamata Zanzibar.
 
Muungano ni mzuri tu pale serikali zinapowajibika vizuri kwa Wananchi wake. Tatizo kubwa lililopo TZ, ni Umaskini unaosababishwa na viongozi wetu. Kwa mfano, angalia muungano wa USA unamanufaa kwa sababu serikali inawajibika vizuri kwa Wananchi wake; lakini muungano wa nchi za Soviet umevunjika kwa sababu ya serikali ilikuwa haiwajibiki ipasavyo. Kazi kwetu sasa WTZ.


Unajuwa tunakosea sana tunapoufananisha muungano wa USA na huu wetu. Ule ni sawa na kuunganisha utemi na uchifu uliokuwepo Bara. Hakuna Utemi au Mkoa utakaodai kuwa una haki zaidi kuliko wenzake Bara lakini unapozungumza Nchi mbili kuifanya nchi moja ni sawa na ndowa tena ya Kiislamu inayotambuwa hiari ya pande mbili katika kuendela na ndoa hiyo. Sasa mwanamme anapotunisha misuli awe bora au mwanamke anaporingia uzuri wake ili awe bora nadi ya yandowa ni matatizo matupu.
 
So let me get this straight. Umesema Z'bar inaibeba Tanganyika. Pia ukasema Muungano unarudisha nyuma maendeleo ya Z'bar na pia kwamba Z'bar would be better off alone. Lakini bado kuvunja Muungano hamtaki? Kama nilivyo sema mwanzo Z'bar can keep it's oil. No point fighting over a venture which has not even made a single penny yet.

We would not be this far in the debate if PINDA and his coleagues would have this very very wise stand of yours.
 
Wanzibar, wananichekesha kweli, kuamua hawako tayari. Hebu basi japo mwaka huu mjaribu kuamua. Kwakuwa nyie mna serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, ambayo haiitendi lolote lililo la muungano. Na kwa kuwa hata pale ambapo hata rais wa Zanzibar anahudhuria baraza la mawazi la muungano, kwenye masuala yanayohusu Tanganyika yeye huweka pamba masikioni, basi mwaka ujao na uwe wa kwanza kuteua wagombea wote wa nafasi za urais wa Zanzibar huko huko Zanzibar na sio kusikilizia chimwaga kama tulivyowazoea, msipoweza hilo, haya mengine mtayaweza je, wakati hamna rais wenu?

Unajuwa wa kukuchekesha hapa si Wazanzibari bali ni hao waliopanga hilo kwani si unajuwa (pengine ni breaking news kwako, kwa ninavyokuona) Dr Salmin Amour hakuwahi kuhudhuria na huyo alieamuwa kuhudhuria alifanya hivyo kwa vile mlimbeba. Sina uhakika kama alihudhuria zaidi ya kiao kimoja.
 
Comoro wako huru tangu hapo! Juzi tu Sambi anatamani kujiunga na Bara!

Suluhisho Muungano ufe kwa mda...Comoro wajiunge na Bara ili Visiwani wajifunze..na kisha walete maombi kujiunga upya na Bara!

Mnakumbuka ni mara ngapi Bara walirekebisha mambo Ushelisheli ..1979 wakati wa Mapinduzi??

Ndo maana Pinda anesema..wadhubutu..ila hakuna anayedhubutu..yaani ni kelele ..na malalamiko tu kama kinda!
 
Maneno yako yana harufu ya ukadhi na OIC, maana ndio inaonekana ni maendeleo kuwa na vitu hivyo viwili! Kazi kucheza bao na kuota misaada toka uarabuni bila kufanya kazi!

Hiyo isiwe nongwa kwani kati ya Zanzibar na Bara ni wepi wanaosafiri kufuata misaada. Nafikiri hili la kuomba omba nliwaonea choyo Wazanzibari na mkaamuwa kuwazuia wasiombe ili kazi hiyo mfanye nyie. Jee yupo anaebisha?
 
Back
Top Bottom