ndetichia
JF-Expert Member
- Mar 18, 2011
- 27,767
- 6,575
Pishi la Pweza
Vipimo
Pweza 1 Kilo
Mafuta ½ kikombe
Chumvi 1 kijiko cha chai
Tangawizi mbichi iliyosagwa 1 kijiko cha chai
Thomu iliyosagwa 1 kijiko cha chai
Masala ukipenda 1 kijiko cha supu
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Osha pweza kisha mkatekate
Mtie viungo vyote ulotayarisha na chumvi
Muache nusu saaa akolee viungo
Mtie ndani ya sufuria bila maji mfunike kisha weka jikoni, atatumbuka maji mwenyewe kwa moto wa kiasi paka awe rangi ya damu yam zee (maroon)
Akishawiva kwa rangi hiyo basi sasa mwaga maji yote,chukua pweza pekee weka kwenye bakuli au sahani
Weka karai au kikaango (frying pan) motoni tia mafuta acha kwa muda wa dakika tano hivi mafuta yapate moto.
Mimina pweza kwenye karai aacha wakaangike paka wabadilike ukiwageuza geuza kila baada ya muda wa dakika kumi hivi. Pweza tayari kwa kuliwa kwa ugali, bagia, kacholi au muhogo
kazi kwenu
Vipimo
Pweza 1 Kilo
Mafuta ½ kikombe
Chumvi 1 kijiko cha chai
Tangawizi mbichi iliyosagwa 1 kijiko cha chai
Thomu iliyosagwa 1 kijiko cha chai
Masala ukipenda 1 kijiko cha supu
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Osha pweza kisha mkatekate
Mtie viungo vyote ulotayarisha na chumvi
Muache nusu saaa akolee viungo
Mtie ndani ya sufuria bila maji mfunike kisha weka jikoni, atatumbuka maji mwenyewe kwa moto wa kiasi paka awe rangi ya damu yam zee (maroon)
Akishawiva kwa rangi hiyo basi sasa mwaga maji yote,chukua pweza pekee weka kwenye bakuli au sahani
Weka karai au kikaango (frying pan) motoni tia mafuta acha kwa muda wa dakika tano hivi mafuta yapate moto.
Mimina pweza kwenye karai aacha wakaangike paka wabadilike ukiwageuza geuza kila baada ya muda wa dakika kumi hivi. Pweza tayari kwa kuliwa kwa ugali, bagia, kacholi au muhogo
kazi kwenu