Pius Msekwa: Kwa mujibu wa Katiba, mpaka sasa Halima Mdee na wenzake hawana sifa za kuwa Wabunge

Pius Msekwa: Kwa mujibu wa Katiba, mpaka sasa Halima Mdee na wenzake hawana sifa za kuwa Wabunge

Mkuu kuna mtu mwingine anaitumia ndiyo maana nikaibadilisha
Dah huyo jamaa hajafanya vizuri. Unajua GT comments zinanoga ukisoma na avatar ya mtu uliyemzoea. Yani nondo unzazoshusha
 
Bipi kuhusu wabunge kuapishwa kwenye ZiIZI ,Msekwa anasemaje?
 
Nchi inaendeshwa km group la wasap... mambo ya kisengerema kabisa aya.
[emoji23][emoji23][emoji23],admin akijisikia anakuleftisha,halafu Siku akiamka vizuri anakurudisha tena, inategemea tu ameamkaje
 
Spika Mstaafu wa Bunge, Pius Msekwa, amesema kwa mujibu wa katiba mpaka sasa Halima Mdee na wenzake 18, hawana tena sifa za kuwa wabunge

Kwa kuwa hawana chama kilichowapeleka Bungeni na hata wakihamia chama kingine hawawezi kupata nafasi hizo, labda mpaka uchaguzi ujao.

====

Mambo yameanza kuwa sio mambo.
Hiyo ni literally na Msekwa asijifanye kwamba hafahamu hii nchi haifuati sheria.

Hao ni wabunge halali kabisa wa mbeleko ya Spika Ndugai na NEC kwa maagizo ya Jiwe
 
Baadae atapigwa bati utasikia nilinukuliwa vibaya sikumaanisha hivyo [emoji28] [emoji28] [emoji28] [emoji28]
Lakini sio kauli yake kama Msekwa in kwa mujibu wa katiba ambayo waheshimiwa wameapa kuilinda kuitunza kuitetea nk.
 
Kumfuta Uanachama Mtu ni mchakato wa Kisheria & Kikanuni pia

Mchakato huo ili ukamilike haushii kwenye Kamati Kuu ya Chama husika pekee bali unaenda hadi ngazi ya Mahakama ya Rufaa!

Hivyo Mdee na wenzake 18 bado ni kiuhalisia Wabunge hadi itakapoamuliwa vinginevyo
na mamlaka husika kupitia mchakato huo!

Mzee wetu amekuwa na haraka mno kutoa hitimisho kana kwamba mchakato ulipoishia Ilikuwa Halali Kisheria na kuwa suala hilo limehitimishwa!

Katiba ipo mahsusi kulinda haki za wote na sio maamuzi ya Uongozi Wa Chama pekeyake!

Tusubiri mchakato ukamilike Kabla ya kutoa hitimisho
lengo la ccm kuwapigania hawa (waliokuwa) wanachama wa chadena siyo kwamba ccm inawapenda sana ila ccm wanafanya hivyo kwa lengo lao mahususi la kuhalalisha haram na hivyo kukubalika kwa jamii ya kitaifa na kimataifa. hivyo basi hata kama ccm ikifanikiwa kuwalinda (waliokuwa) wanachadema hawa bado lengo mahususi la ccm halitatimia na zaidi sana watazidi kuhalalisha kuwa nchi hii ni ya kidikteta unaochagizwa kupitia vyombo rasmi vya kidola ikiwemo mahakama, bunge na serikali yenyewe kiujumla.

Mwisho wa siku kinachotakiwa hapa ni Katiba mpya na Tume Huru ya uchaguzi..hiyo ndiyo agenda kuu ya chadema na upinzani kiujumla na kiukweli hii ilipaswa pia kuwa agenda kuwa ya kila mwananchi wakiwemo wananchi-ccm..kila mwenye akili timamu anajiuliza kwa nini ccm haitaki kabisa kusikia katiba mpya na tume huru ya uchaguzi?!!! jibu ni kwamba ukiona mtu anapenda gizagiza tu hataki mwanga jua huyo kama si kibaka ni jambazi kabisa
 
Ili kuwanusuru hawa wabunge wapya wa Spika, inabidi wakakate rufaa Mahakamani ya kuvuliwa uanachama wa Chadema. Kisha Hakimu aseme waendelee na majukumu yao hadi kesi itakaposikilizwa tena hapo mwakani July 25, 2021
 
Kumfuta Uanachama Mtu ni mchakato wa Kisheria & Kikanuni pia

Mchakato huo ili ukamilike haushii kwenye Kamati Kuu ya Chama husika pekee bali unaenda hadi ngazi ya Mahakama ya Rufaa!

Hivyo Mdee na wenzake 18 bado ni kiuhalisia Wabunge hadi itakapoamuliwa vinginevyo
na mamlaka husika kupitia mchakato huo!

Mzee wetu amekuwa na haraka mno kutoa hitimisho kana kwamba mchakato ulipoishia Ilikuwa Halali Kisheria na kuwa suala hilo limehitimishwa!

Katiba ipo mahsusi kulinda haki za wote na sio maamuzi ya Uongozi Wa Chama pekeyake!

Tusubiri mchakato ukamilike Kabla ya kutoa hitimisho
Mkuu hata mahakama ya mwanzo inapotoa hukumu mtu anakuwa tayari ameshahukumiwa na hata gerezani hupelekwa
lkn km hatakuwa hajaridhika ipo nafasi ya muda wa kukata rufaa
Hvyo alichokisema ni kwa mujibu wa sheria ukishafutiwa uanachama wewe si mbunge unless usonge mbele kwenye mamlaka zaidi
So yupo sahihi kma kina mdee hawajaridhika
Wakate rufaa lakini kwa sasa si wabunge tena
 
Wafukuzwe tuu wameshindwa kusimama na chadema katika kipindi kigumu.
 
Vp kama CCM wakiwatosa hao COVID-19 na kutafuta njia mbadala, CDM inabidi iwe makini mana hapo CCM watakuwa hawana cha kupoteza lakini CDM itakuwa imepoteza wanachama wake walio kengeuka na kuwa COVID-19
Wana chakupoteza ndiyo maana drama haziishi-Trilion 2 zipo at stake na hawana utayari kuzipoteza.
 
Baadae atapigwa bati utasikia nilinukuliwa vibaya sikumaanisha hivyo [emoji28] [emoji28] [emoji28] [emoji28]
Hapana hawezi fanya hivyo kwani kanukuu Katiba ya Nchi. Ndugai anatia aibu kwa kukiuka Katiba na Kanuni za Bunge wazi wazi kwakuwa hakuna wa kumuuliza wala kumkemea. Bali yuko anayefurahishwa na upuuzi wa Ndugai.
 
Mbona mchezo unajulikana. Wataenda mahakamani kupinga kufukuzwa na kesi itavutwa miaka na miaka hadi wanamaliza ubunge. Kuchoshana tu.
 
Back
Top Bottom