Plasduce Mbossa wa TPA: Serikali Kupitia TPA imesaini MoUs na Kampuni za Saudi Arabia,China na Egypt Ili Kuendeleza Bandari ya Bagamoyo

CCM nyie ni wehu Magufuli alipokataa huo mradi akishangiliwa leo hivi mnaukubali kwa mara nyingine anashangiliwa atakuja mwingine tena apinge anashangiliwa, hovyo kabisa
Hapana magufuli alikataa huo mradi hata mama pia alikataa ila hao wanao sign Sasa ni wengine kabisa
 
Hapana magufuli alikataa huo mradi hata mama pia alikataa ila hao wanao sign Sasa ni wengine kabisa
Alikataa huo mradi kwa sababu za kisiasa, akidhani kwamba akikubaliana nao atampa umaarufu JK kwani awamu ya nne aliupigania sana ufanikiwe. Zile sababu za kuukataa alizozitoa pale ikulu ni za kisiasa tu.

Mungu katupa fukwe ndefu kwa sababu maalum, tutakuwa wajinga tukiishia kuridhika kuwa na hizi bandari tatu za sasa wakati dunia ya kisasa hiyo bandari ya Bagamoyo ikishirikiana na ile ya Dar zinaweza kiuchumi kutufikisha mbali sana.

Mwanasheria mkuu wa sasa ndiye aliyepambana DPW akaweza kupewa tender ya kuiendesha bandari ya Dar na yupo makini sana kwenye vifungu vyote ambavyo vinaweza kuwa na sura ya kinyonyaji dhidi ya maslahi ya Tanzania.
 
Kaka hii ccm ya Samia na machawa wake wanachoangalia wao ni jinsi gani wanavyonufaika wao binafsi kwanza na hakuna anayejali athari zinazoweza kutokana na maamuzi anayofanya Samia sasa kwa vizazi vya mbeleni huko.... imagine mtu unamkabidhi mradi akuendeshee kwa miaka 30 tena akiwa na full authority ni akili hiyo kweli?

Serikali ya samia ndio serikali ya ovyoo kuwa kutokea hapa nchini, hawa machawa wake ambao wengi ni watanganyika acha wamfurahie tu kwa sababu ya hivyo visenti wanavyoambulia kwa sasa....lakin hata familia zao watakuwa na wahanga huko mbeleni
 
Kabla ya uwekezaji wa DP World,wewe ulikuwa inanufaika vipi na Bandari?

Ukinijibu hili swali nafuta Uzi 😂😂
 
Hapana magufuli alikataa huo mradi hata mama pia alikataa ila hao wanao sign Sasa ni wengine kabisa
Sama sio mbumbumbu kwamba aache kutekeleza miradi Kwa sababu za kipuuzi za wajamaa mbuzi wasiojitambua.
 
Kama angekataa kwasababu za kisiasa basi Samia angesign nao haraka sana ila hata yeye alikataa kumbuka huo mkataba ulikuwa unahusisha china merchants na Serikali ya Oman
 
Kama angekataa kwasababu za kisiasa basi Samia angesign nao haraka sana ila hata yeye alikataa kumbuka huo mkataba ulikuwa unahusisha china merchants na Serikali ya Oman
Alidanganywa kuhusu vipengele vya mikataba pia alidhani kuwa Kikwete angepiga bao iwapo Bandari ya Bagamoyo ingejengwa kipindi cha awamu ya tano, tukizingatia Bagamoyo ni mkoa wa Pwani nyumbani kwa Mkwere.

Tunaihitaji bandari ya Bagamoyo iweze kuzisaidia bandari za Dar, Tanga na Mtwara katika kuinua uchumi wa Tanzania.
 
Akili yako ya kitoto mpuuzi wewe. Wanasiasa walioiongoza nchi hii kwa miaka yote wangekuwa na akili kama za kwako Tanzania ingeshakufa kipindi kirefu sana.
Wewe unanufaikaje kwa kuungana na Zanzibar? ukinunua TV Zanzibar kuvuka kuja dar unalipa ushuru, lakini ukinunua TV Dar unaenda nayo mpk kwenu Bukoba bila usumbufu, Mzanzibar anapata haki zote kama wewe ulizo nazo, ajira zikitoka Zanzibar anaomba na bara anaomba wewe unanufaikaje na huu muungano fake? wewe akili ako dada angu ni ya kijinga sn shituka.
 
Alidanganywa na nani? Kwaiyo ulitaka JPM apitishe mkataba wa kimangungo ili amfurahishe mkwere.

Haya na Samia kwanini alishindwana nao?
 
Muda sio mrefu ofisi ya mwanasheria mkuu itaanza kupitia wasifu wa hawa wawekezaji watatu watakaopitishwa na serikali kwa ajili ya shughuli za uwekezaji kuanza.
Halafu mwanasheria akishapitia wasifu wao nini kinafuatia? Anaushirikisha na uma kabla ya kuwakabidhi rasimi mradi au akishapitia tu yeye na akajiridhisha imetosha?

Na pia hapa tunachotaka ni kuona mkataba unasema nini kipengele kimoja baada ya kingine...
Tunaweza kupiga kelele kadri tuwezavyo lakini hatuwezi kukwepa umuhimu wa bandari ya Bagamoyo.
umuhimu huo uwe na tija kwa taifa zima na sio kwa ajili ya maslahi ya genge la watu wa chache tu likiongozwa na yule babu wa msoga.
Sawa, sasa watanzania wanataka kila kitu kiwe wazi, washirikishwe kila hatua ya uwekezaji/mradi huo, na pia hata pesa zitakazopatikana hapo waone jinsi gani zinavyotumika na wasiishie kuambiwa tu tumejenga zahanati 20 kumbe uongo mtupu hela zimeishia mifukoni mwa mafisadi yanayoimba kila mara bibi anaupiga mwingi.
 
Hakuna mkataba wa kuuona ,sheria hazitaki hayo unayosema wewe.
But this is an argument from tradition logical fallacy.

You are basically saying let's do it this way because we have been doing it this way. This is a logical fallacy.

It is also an argument from authority logical fallacy.

You are saying the law is the authority, let's not think critically, let's just follow the law.

Laws get outdated, they should be changed.

Kutetea kitu kwa hoja ya "sheria zinasema" ni ujinga. Afrika Kusini sheria zilisema watu weusi wabaguliwe, je, hilo lilikuwa jambo la sawa na haki kwa sababu sheria ilisema?

Uwazi ni kitu muhimu, usiri ni kichaka cha rushwa. Siku hizi hata hao mnaowaita mabeberu wa World Bank wanasisitiza uwazi katika miradi wanayo i fund na miradi ya serikali. Kwa nini serikali ya Tanzania inafanya usiri sana katika mambo yenye public interest?

Wewe huoni kuwa kutetea mikataba ambayo hujaiona, hujui terms zake, hata kwa juu juu tu, ni ujinga?

Kama hujui chochote kuhusu mikataba utajuaje kuwa unatetea kitu kisichokuumiza?

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…