PLO Lumumba: Tundu Lissu ni muongo, nimefika Chato Hayati Magufuli hana utajiri wa kumlinganisha na Mobutu Sese Seko

PLO Lumumba: Tundu Lissu ni muongo, nimefika Chato Hayati Magufuli hana utajiri wa kumlinganisha na Mobutu Sese Seko

Mkuu hujawahi kumiminiwa SMG magazine nzima!! Sio rahisi kama tunavyofikiria kusahau. Kwake yeye kuongea ya moyoni mwake inampa relief ya lile tukio maana polisi wameshindwa play their part. Kma wahusika wangenyongwa Lissu moyo ungetulia na hasira zingeisha.
Kumiminiwa SMG inahusiana nini na maslahi ya wananchi?
 
Nimemsikiliza PLO Lumumba, mzee anajua Sana. Nataman Sana serikali ya JMT ingekua na mtu mwenye uwezo wa kuisemea Kama Prof. Kwa ufafanuzi wake, Sasa ni rasmi dunia nzima inajua Lissu ana chuki binafsi na JPM, na ni hakika Magufuli alikuwa Kiongozi mwema, mpenda nchi yake aliyetamani kuona nchi ikipiga hatua kimaendeleo.
#TANZANIA NI YETU SOTE, TUIPENDE NA KUITUMIKIA
JPM alikuwa mwizi, muuaji, mbinafsi, mkabila, mpenda sifa na madaraka, mnafiki wa kujifanya mcha Mungu, mzinzi, mwongo na fisadi wa elimu
 
Hakukuwa na ulazima wa kuingia barabarani watu wapoteze maisha dhidi ya yule ibilisi, tulichofanya ni kuongea na Mungu ndani ya miezi sita ibilisi asiwepo kuendelea kumwaga damu za wananchi. Na kweli leo hii ibilisi yuko motoni, anatoa mahesabu ya mauaji aliyofanya kwa uchu na kiburi cha madaraka.
Kabla ya hayo maombi mlikuwa mnajua Magufuli siku yake ya kufa ni lini hadi useme maombi yenu ndio sababu ya umauti wake?
Kuanzia kifo chake hadi kuzikwa kwake hakuoneshi dalili ya huo mtu kufa kwa maombi ya watu kwa Mungu.
 
Kabla ya hayo maombi mlikuwa mnajua Magufuli siku yake ya kufa ni lini hadi useme maombi yenu ndio sababu ya umauti wake?
Kuanzia kifo chake hadi kuzikwa kwake hakuoneshi dalili ya huo mtu kufa kwa maombi ya watu kwa Mungu.

Mungu wetu ana nguvu, hivyo ilikuwa ni kutusikiliza tu sisi waja wake dhidi ya yule muovu.
 
JPM alikuwa mwizi, muuaji, mbinafsi, mkabila, mpenda sifa na madaraka, mnafiki wa kujifanya mcha Mungu, mzinzi, mwongo na fisadi wa elimu
JPM alikuwa Kiongozi mcha Mungu kweli na mwenye msimamo dhabiti(JIWE/MWAMBA/KEFA/PETROUS). Na binafsi nilipenda kumchukulia Kama mtu mwenye nia njema na Taifa, aliyetamani kuona kila mtanzania ananufaika na raslimali za nchi. Alikubali kuwa jiwe la msingi wa maendeleo ya watu wake na hata kuhatarisha maisha yake. Alifanya hivyo, huku akitambua hatari iliyokuwa mbele yake. Ndio maana wengine wanaamini hata kifo chake huenda kimechangizwa na misimamo yake dhidi ya mataifa yenye password na system ya pacemakers. Hata hivyo, katika kutekeleza hayo, naelewa kuwa baadhi ya watu waliumizwa na Sera zake. Tukubali, hakuna mabadiliko ya kweli pasipo maumivu. Una haki ya kumuona hivyo unavyomuona, lakin kwa uhalisia, JPM atabaki Kama alama ya Pan Africanist na mzalendo halisi wa kizazi Cha Leo.
 
Mungu wetu ana nguvu, hivyo ilikuwa ni kutusikiliza tu sisi waja wake dhidi ya yule muovu.
Kama Mungu ana nguvu na mliomba akasikia kwa nini mungu Yule yule Magufuli akiwaambia muombe na ametukinga kwa corona mnakataa? au sio nyie mnaodai tutumie njia za kiscience? au mungu yuko kwenye tu kwa wenngine hayuko?
 
Mungu wetu ana nguvu, hivyo ilikuwa ni kutusikiliza tu sisi waja wake dhidi ya yule muovu.
Nimekuuliza mlikuwa mnajua ni lini Magufuli ndio ilikuwa siku yake ya kufa kabla ya kumuombea afe? kwa sababu tunajua kila mtu lazima siku moja afe tu sasa nyie mnajuaje kwamba Magufuli kafa kwa sababu ya maombi yenu na si kwamba ilikuwa tu siku yake ya kufa kama ilivyo kwa wengine?

Nitajie hata dalili moja tu kuonesha kwamba kifo cha Magufuli ni matokeo ya hayo maombi yenu? Maana maombi mabaya ya kwa Magufuli na ccm kwa ujumla yalikuwepo toka 2015,sasa 2021 Magufuli kafa ndio mnahusisha na maombi?
 
Kwa kusema eneo la Mwendazake Chato ni la kimaskini imedhihirisha kuwa nae ni muongo.

Amandla...
 
Aache unafiki wake huyo mkenya Mali zilizopo Chato Butiama,msoga wala Masasi hakuna
 
Back
Top Bottom