ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 66,537
- 75,687
My Take
Nakubalina na PM 💯 💯
Kwenye suala la Maendeleo Samia hana mshindani Kila mtu anaona huko aliko 👇👇
---
RAIS DKT. SAMIA NI TIBA YA MAENDELEO – MAJALIWA
▪️ Waziri Mkuu asema Rais Dkt. Samia amedhamiria kutekeleza na kukamilisha miradi yote ya kimkakati.
▪️ Aeleza kuwa Rais Dkt. Samia ni kiongozi anayeona, kusikiliza na kutatua changamoto za wananchi.
▪️ Atoa wito kwa wananchi kuendelea kuiunga mkono CCM kwa weledi na uaminifu.
▪️ Asisitiza kuwa CCM imeleta, inaleta na itaendelea kuleta maendeleo nchini.
▪️ Asema chama hicho kinasema, kinaahidi na kinatekeleza.
Maswa, 16 Februari 2025 – Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, amesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ni "tiba ya maendeleo" kwa Watanzania kutokana na jitihada zake za kusimamia utekelezaji wa miradi ya kimkakati inayoboresha maisha ya wananchi.
Akizungumza katika Mkutano Mkuu Maalum wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Jimbo la Maswa Mashariki, uliofanyika katika Uwanja wa Nguzo Nane, Maswa, mkoani Simiyu, Waziri Mkuu amesema kuwa Rais Dkt. Samia ni kiongozi mwenye maono makubwa, anayeona, kusikiliza na kutatua changamoto za Watanzania kwa ustadi wa hali ya juu.
"Rais Dkt. Samia amejidhihirisha kama kiongozi shupavu mwenye nia ya dhati ya kuleta maendeleo. Anafanya kazi kwa bidii kuhakikisha miradi yote ya kimkakati inatekelezwa na kukamilika kwa wakati, huku akihakikisha wananchi wananufaika na huduma bora za kijamii," alisema Mhe. Majaliwa.
Aidha, Waziri Mkuu amesisitiza kuwa CCM itaendelea kuwa mstari wa mbele katika kuwaletea Watanzania maendeleo ya kweli, kwa kuwa ndicho chama chenye dira na dhamira ya kuwatumikia wananchi kwa weledi na uaminifu mkubwa.
"CCM ni chama kinachosema, kinaahidi na kinatekeleza. Tumekuwa tukitekeleza miradi mikubwa ya maendeleo katika sekta mbalimbali kama afya, elimu, miundombinu, maji na umeme. Chama hiki kimeleta maendeleo, kinaendelea kuleta maendeleo na kitaendelea kuongoza kwa maendeleo," alisisitiza Waziri Mkuu.
Aliwataka wananchi waendelee kuiunga mkono Serikali inayoongozwa na CCM kwa kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo na kuhakikisha miradi inayotekelezwa inakuwa na tija kwa jamii.
Imetolewa na:
Idara ya Siasa na Uenezi
Chama Cha Mapinduzi (CCM) – Mkoa wa Simiyu
Nakubalina na PM 💯 💯
Kwenye suala la Maendeleo Samia hana mshindani Kila mtu anaona huko aliko 👇👇
---
RAIS DKT. SAMIA NI TIBA YA MAENDELEO – MAJALIWA
▪️ Waziri Mkuu asema Rais Dkt. Samia amedhamiria kutekeleza na kukamilisha miradi yote ya kimkakati.
▪️ Aeleza kuwa Rais Dkt. Samia ni kiongozi anayeona, kusikiliza na kutatua changamoto za wananchi.
▪️ Atoa wito kwa wananchi kuendelea kuiunga mkono CCM kwa weledi na uaminifu.
▪️ Asisitiza kuwa CCM imeleta, inaleta na itaendelea kuleta maendeleo nchini.
▪️ Asema chama hicho kinasema, kinaahidi na kinatekeleza.
Maswa, 16 Februari 2025 – Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, amesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ni "tiba ya maendeleo" kwa Watanzania kutokana na jitihada zake za kusimamia utekelezaji wa miradi ya kimkakati inayoboresha maisha ya wananchi.
Akizungumza katika Mkutano Mkuu Maalum wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Jimbo la Maswa Mashariki, uliofanyika katika Uwanja wa Nguzo Nane, Maswa, mkoani Simiyu, Waziri Mkuu amesema kuwa Rais Dkt. Samia ni kiongozi mwenye maono makubwa, anayeona, kusikiliza na kutatua changamoto za Watanzania kwa ustadi wa hali ya juu.
"Rais Dkt. Samia amejidhihirisha kama kiongozi shupavu mwenye nia ya dhati ya kuleta maendeleo. Anafanya kazi kwa bidii kuhakikisha miradi yote ya kimkakati inatekelezwa na kukamilika kwa wakati, huku akihakikisha wananchi wananufaika na huduma bora za kijamii," alisema Mhe. Majaliwa.
Aidha, Waziri Mkuu amesisitiza kuwa CCM itaendelea kuwa mstari wa mbele katika kuwaletea Watanzania maendeleo ya kweli, kwa kuwa ndicho chama chenye dira na dhamira ya kuwatumikia wananchi kwa weledi na uaminifu mkubwa.
"CCM ni chama kinachosema, kinaahidi na kinatekeleza. Tumekuwa tukitekeleza miradi mikubwa ya maendeleo katika sekta mbalimbali kama afya, elimu, miundombinu, maji na umeme. Chama hiki kimeleta maendeleo, kinaendelea kuleta maendeleo na kitaendelea kuongoza kwa maendeleo," alisisitiza Waziri Mkuu.
Aliwataka wananchi waendelee kuiunga mkono Serikali inayoongozwa na CCM kwa kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo na kuhakikisha miradi inayotekelezwa inakuwa na tija kwa jamii.
Imetolewa na:
Idara ya Siasa na Uenezi
Chama Cha Mapinduzi (CCM) – Mkoa wa Simiyu