Pre GE2025 PM Majaliwa: Rais Samia ni Tiba ya Maendeleo, hakuna mbadala

Pre GE2025 PM Majaliwa: Rais Samia ni Tiba ya Maendeleo, hakuna mbadala

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
66,537
Reaction score
75,687
My Take
Nakubalina na PM 💯 💯

Kwenye suala la Maendeleo Samia hana mshindani Kila mtu anaona huko aliko 👇👇

---
RAIS DKT. SAMIA NI TIBA YA MAENDELEO – MAJALIWA

▪️ Waziri Mkuu asema Rais Dkt. Samia amedhamiria kutekeleza na kukamilisha miradi yote ya kimkakati.
▪️ Aeleza kuwa Rais Dkt. Samia ni kiongozi anayeona, kusikiliza na kutatua changamoto za wananchi.
▪️ Atoa wito kwa wananchi kuendelea kuiunga mkono CCM kwa weledi na uaminifu.
▪️ Asisitiza kuwa CCM imeleta, inaleta na itaendelea kuleta maendeleo nchini.
▪️ Asema chama hicho kinasema, kinaahidi na kinatekeleza.

Maswa, 16 Februari 2025 – Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, amesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ni "tiba ya maendeleo" kwa Watanzania kutokana na jitihada zake za kusimamia utekelezaji wa miradi ya kimkakati inayoboresha maisha ya wananchi.

Akizungumza katika Mkutano Mkuu Maalum wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Jimbo la Maswa Mashariki, uliofanyika katika Uwanja wa Nguzo Nane, Maswa, mkoani Simiyu, Waziri Mkuu amesema kuwa Rais Dkt. Samia ni kiongozi mwenye maono makubwa, anayeona, kusikiliza na kutatua changamoto za Watanzania kwa ustadi wa hali ya juu.

"Rais Dkt. Samia amejidhihirisha kama kiongozi shupavu mwenye nia ya dhati ya kuleta maendeleo. Anafanya kazi kwa bidii kuhakikisha miradi yote ya kimkakati inatekelezwa na kukamilika kwa wakati, huku akihakikisha wananchi wananufaika na huduma bora za kijamii," alisema Mhe. Majaliwa.

Aidha, Waziri Mkuu amesisitiza kuwa CCM itaendelea kuwa mstari wa mbele katika kuwaletea Watanzania maendeleo ya kweli, kwa kuwa ndicho chama chenye dira na dhamira ya kuwatumikia wananchi kwa weledi na uaminifu mkubwa.

"CCM ni chama kinachosema, kinaahidi na kinatekeleza. Tumekuwa tukitekeleza miradi mikubwa ya maendeleo katika sekta mbalimbali kama afya, elimu, miundombinu, maji na umeme. Chama hiki kimeleta maendeleo, kinaendelea kuleta maendeleo na kitaendelea kuongoza kwa maendeleo," alisisitiza Waziri Mkuu.

Aliwataka wananchi waendelee kuiunga mkono Serikali inayoongozwa na CCM kwa kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo na kuhakikisha miradi inayotekelezwa inakuwa na tija kwa jamii.

Imetolewa na:

Idara ya Siasa na Uenezi
Chama Cha Mapinduzi (CCM) – Mkoa wa Simiyu
 
My Take
Nakubalina na PM 💯 💯

Kwenye suala la Maendeleo Samia hana mshindani Kila mtu anaona huko aliko 👇👇

View: https://www.instagram.com/reel/DGJGCOoi9px/?igsh=Y21keDlwN2Fvdzgy

Ogopa watu wanaokusifu sana. Hata Magufuli wanaomsifu mama sasa hivi ndiyo wale wale walikuwa washaanza kampeni awe rais wa kudumu.
Wabongo si watu wa kuwaamini amini maana wanaweza sema chochote ilimrad wapate kula. Nimemkumbuka aliyesema baada ya Yesu na Mohamad anafuata Samia.
 
Wakati wa Kikwete hata waziri mkuu hakuwa akimsifia wala kutajwa kwenye kila jambo. Huenda ni sababu walijua Kikwete ni mwerevu, sifa za kinafki hakuwa anazikubali. Mtu kukusifia sifia kila muda inakuwa sio kwa ukweli.

Sifa za rais zitakuwa na maana kama atasifiwa na watu walio nje ya circle yake na wasio na uhusiano na chama chake moja kwa moja. Anaishia kusifiwa na wale wale wanaomzunguka. Hata yeye hawezi kufurahia sifa hizo za uongo.
 
Ogopa watu wanaokusifu sana. Hata Magufuli wanaomsifu mama sasa hivi ndiyo wale wale walikuwa washaanza kampeni awe rais wa kudumu.
Wabongo si watu wa kuwaamini amini maana wanaweza sema chochote ilimrad wapate kula. Nimemkumbuka aliyesema baada ya Yesu na Mohamad anafuata Samia.
Kusifia na Kampeni za kuwa Rais wa kudumu vinahusianaje?

Swali la msingi ni Je anasifiwa uongo au ukweli?
 
Wakati wa Kikwete hata waziri mkuu hakuwa akimsifia wala kutajwa kwenye kila jambo. Huenda ni sababu walijua Kikwete ni mwerevu, sifa za kinafki hakuwa anazikubali. Mtu kukusifia sifia kila muda ni dalili ya yeye kukuona hujielewi.

Sifa za rais zitakuwa na maana kama atasifiwa na watu walio nje ya circle yake na wasio na uhusiano na chama chake moja kwa moja. Anaishia kusifiwa na wale wale wanaomzunguka. Hata yeye hawezi kufurahia sifa hizo za uongo.
Uongo na dalili ya wivu na chuki 🤣 🤣
 

RAIS DKT. SAMIA NI TIBA YA MAENDELEO – MAJALIWA

▪️ Waziri Mkuu asema Rais Dkt. Samia amedhamiria kutekeleza na kukamilisha miradi yote ya kimkakati.
▪️ Aeleza kuwa Rais Dkt. Samia ni kiongozi anayeona, kusikiliza na kutatua changamoto za wananchi.
▪️ Atoa wito kwa wananchi kuendelea kuiunga mkono CCM kwa weledi na uaminifu.
▪️ Asisitiza kuwa CCM imeleta, inaleta na itaendelea kuleta maendeleo nchini.
▪️ Asema chama hicho kinasema, kinaahidi na kinatekeleza.

Maswa, 16 Februari 2025 – Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, amesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ni "tiba ya maendeleo" kwa Watanzania kutokana na jitihada zake za kusimamia utekelezaji wa miradi ya kimkakati inayoboresha maisha ya wananchi.

Akizungumza katika Mkutano Mkuu Maalum wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Jimbo la Maswa Mashariki, uliofanyika katika Uwanja wa Nguzo Nane, Maswa, mkoani Simiyu, Waziri Mkuu amesema kuwa Rais Dkt. Samia ni kiongozi mwenye maono makubwa, anayeona, kusikiliza na kutatua changamoto za Watanzania kwa ustadi wa hali ya juu.

"Rais Dkt. Samia amejidhihirisha kama kiongozi shupavu mwenye nia ya dhati ya kuleta maendeleo. Anafanya kazi kwa bidii kuhakikisha miradi yote ya kimkakati inatekelezwa na kukamilika kwa wakati, huku akihakikisha wananchi wananufaika na huduma bora za kijamii," alisema Mhe. Majaliwa.

Aidha, Waziri Mkuu amesisitiza kuwa CCM itaendelea kuwa mstari wa mbele katika kuwaletea Watanzania maendeleo ya kweli, kwa kuwa ndicho chama chenye dira na dhamira ya kuwatumikia wananchi kwa weledi na uaminifu mkubwa.

"CCM ni chama kinachosema, kinaahidi na kinatekeleza. Tumekuwa tukitekeleza miradi mikubwa ya maendeleo katika sekta mbalimbali kama afya, elimu, miundombinu, maji na umeme. Chama hiki kimeleta maendeleo, kinaendelea kuleta maendeleo na kitaendelea kuongoza kwa maendeleo," alisisitiza Waziri Mkuu.

Aliwataka wananchi waendelee kuiunga mkono Serikali inayoongozwa na CCM kwa kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo na kuhakikisha miradi inayotekelezwa inakuwa na tija kwa jamii.

Imetolewa na:

Idara ya Siasa na Uenezi
Chama Cha Mapinduzi (CCM) – Mkoa wa Simiyu
 
Huyu babu nilivyogundua anapaka nywele kiwi ili apate mademu nikajua hapa hatuna mtu ni hovyo kabisa, hata akifanya ziara hakuna mtu anashitika. hayupo sawa kuna shida na sijui anatumia kinywaji gani?
 
Ni ujinga uliopitiliza kufikiri kuwa maendeleo yanaletwa na Rais.
Ni sahihi kazi gani anafanya kama huyu babu lakini analipwa mamilioni ya walipa kodi masikini na hakuna cha maana anafanya, kaletewa maendeleo yeye binafsi na mafisadi wenzie, ajira za walimu wameomba zaidi ya laki 2 hutakuta hata mjukuu wake au ndugu ake ameenda kufanya interview watoto wao utawakuta TCRA, Bandarini, BoT, TANAPA, Mambo ya nje, Hazina, bungeni kote kwenye pipi. Tunaongozwa na majangili tupu
 
Wakati wa Kikwete hata waziri mkuu hakuwa akimsifia wala kutajwa kwenye kila jambo. Huenda ni sababu walijua Kikwete ni mwerevu, sifa za kinafki hakuwa anazikubali. Mtu kukusifia sifia kila muda inakuwa sio kwa ukweli.

Sifa za rais zitakuwa na maana kama atasifiwa na watu walio nje ya circle yake na wasio na uhusiano na chama chake moja kwa moja. Anaishia kusifiwa na wale wale wanaomzunguka. Hata yeye hawezi kufurahia sifa hizo za uongo.
Haya majangili yakiimba mali za umma ndiyo yanaanza kumsifia kinafiki, huyu babu anafanya nini zaidi ya kupaka kiwi nywele apendwe na mademu. Hovyo kabisa
 
Back
Top Bottom