#COVID19 Polepole: Hatuwezi kuzuia watalii kwa sababu ya Corona, tutapambana nayo kama tunavyopambana na Upinzani. Nchi inategemea watalii

#COVID19 Polepole: Hatuwezi kuzuia watalii kwa sababu ya Corona, tutapambana nayo kama tunavyopambana na Upinzani. Nchi inategemea watalii

Mihemko mibaya sana, tulikuwa hatujapata sample ya virusi ila saivi tunayo,
Tunaahidi tiba na chanjo tunazitafiti tupo maabara saivi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tunaongelea hapa chama kukua,nikakuuliza ili chama kikue tunatakiwa kuangalia viashiria vipi?Ukanitajia na nikatumia hivyo hivyo viashiria kukuonesha kuwa CDM sasa imekua zaidi ya kipindi cha Dr Slaa!Nakuongeza na vigezo vingine ukiachana na idadi ya wabunge!
Wanachama sasa wameongezeka kuliko wakati wa Slaa!Lakini pia ruzuku ya chama imeongezeka kutokana na idadi ya kura milion 6 mwaka 2015 na wabunge lukuki!
Hizo ulizoleta hapo juu ni blah blah,hoja hujibiwa kwa hoja na sio mipasho!
Usiongelee ruzuku utaibua mengi...ila kubali tu wananchin hawana imani na nyie tena.
 
Usiongelee ruzuku utaibua mengi...ila kubali tu wananchin hawana imani na nyie tena.
Hapo ndipo nilipo na tatizo na wewe!Umetumia kipimo gani kufikia hilo hitimisho?Nami naweza nikasema wananchi hawana imani na JPM tena!
 
Sina ushabiki wa mambo ya kijinga lakini kwa hili mtoa mada umenigusa, then kwanini Khamis Mwinjuma aendelee kujiweka Quarantine wakati walitangaza kuwa wagonjwa watapelekwa Mloganzila? Inafikirisha sana!

ˡ ˡⁱᵏᵉ ᵇⁱᵍ⁻ᵗⁱᵗᵗʸ ʷᵒᵐᵃⁿ [emoji377]
 
Hapo ndipo nilipo na tatizo na wewe!Umetumia kipimo gani kufikia hilo hitimisho?Nami naweza nikasema wananchi hawana imani na JPM tena!
Mwenyekiti wa Chadema taifa (mb) alizomewa na wananchi wa hai. Na mahudhurio kiduchu kama karanga za kuonjeshwa.
 
Mwenyekiti wa Chadema taifa (mb) alizomewa na wananchi wa hai. Na mahudhurio kiduchu kama karanga za kuonjeshwa.
Unazungumzia wale walevi makada wa UVCCM waliotumwa na Sabaya?Huo upuuzi wenzako hawautumii tena maana umebuma!
 
Nimeangalia taarifa ya habari ya BBC usiku huu hali ni Mbaya sana nchini Irani kusu ugonjwa wa Corona. Takwimu zinasema kila dakika kumi mtu mmoja anakufa na huko ktk wodi za wagonjwa Mahututi kumejaa wagonjwa na hakuna vifaa tiba.

Madaktari wamekata tamaa na hali iliyopo. Madaktari wengi wamekufa wakiwa wanapambana kuokoa maisha ya wagonjwa na wao kuambukizwa virusi vya korona.

Kitendo cha bwana Polepole kusema kuwa hawawezi kuzuia watalii kuingia nchini eti watakosa hela sio tuu ni kiburi cha madaraka pia ni kauli ya kujikinai kufuru kwa watanzania.

Kwa jinsi nilivyo ona taarifa ile hali ilivyo ktk mahospitali huko Irani ambako kiasi fulani wako mbele kimaendeleo huu ugonjwa sio wa kuufanyia mzaha kama hata mimi awali nilidhania ni ugonjwa wa kawaida tuu. Msdatkari walio hojiwa wanatia simanzi mno ktk utendaji wa kazi zao na wanaonekana hawana Promising future.

Kwa mahesabu rahisi tuu kama kila baada ya dakika kumi mtu mmoja anakufa, hivyo kila saa moja Irani wanakufa watu sita. Hii ina maana kuwa ndani ya masaa 24 watu 144 wanakufa huko Irani kwa takwimu za leo hii.

Watanzania wenzangu tuchukue tahadhari ya kutosha hali ikisha anza kuwa Mbaya hawa akina Polepole hatuta waona hadharani tena. Sisi maskini makapuku ndio tutakufa kama mbwa koko. Majuto ni mjukuu ndugu zangu hima tusifanye mzaha Dunia kwa sasa imo ktk tatizo baya.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuleta shida kiuchumi sawa lakin kwann awausishe chadema na corona
Akihojiwa clouds Humphrey polepole amesema wapinzani Ni sawa Corona.

Kauli hii ya kiongozi kijana inaweza tafsiriwa Kama kauli ya kiongozi aliyepoteza dira na ambaye kwake maisha ya watu wasio ccm si kitu bali binadamu sahihi ni mwanaccm.

Niwaomba viongoz wa chama tawala kuchukua hatua kwake na pia vyombo vya dola kumshughulikia kwani kumwacha aendelee na tabia hii kutasababisha wapinzani nao kutumia kauli Kama hizi kujibu mapigo na hivyo kusababisha mgawanyiko kwenye taifa.

Tukumbuke ishu ya MENDE kwa wenzetu...

**********
Amesema ukizuia Watalii kuingia Nchini kwa mwezi mmoja kutokana na #coronavirus italeta shida kiuchumi, hivyo ni kuomba Mungu ugonjwa huu uondoke. #COVID19 ni sawa na wapinzani Nchini

Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi wa CCM, amesema "Tuna vituo Nchi nzima ambavyo vimetengwa kwa ajili ya kuwahudumia waathirika wa ugonjwa wa virusi vya hivyo."

Kuhusu CCM kununua Wapinzani amesema "Si kweli kuwa CCM inatoa fedha kununua Wanachama wa upinzani bali inabidi wapinzani watazame jinsi wanavyoharibikiwa wenyewe ndani kwa ndani"

"Kuna mwanachama wa Mbowe anaitwa Paulina, aliondoka kwenye Chama kwasababu alikuwa anatakiwa kimahusiano na viongozi wake hivyo akaamua kuhama ili kuokoa ndoa yake lakini alivyohama wapinzani wakatafuta kisingizo kuwa amenunuliwa"

Ameongeza, "Chama cha Freeman Mbowe wanaiitana Bwana au Kamanda wao sio ndugu. Katika chama chetu huwa natumia sana neno ndugu na siyo Mheshimiwa kwa kwasababu sisi si kitu bila ya watu waliotupa dhamana"

Aidha, amesema "Hii tume ya Uchaguzi ni huru kabisa kama si huru mbona Halima Mdee na Joseph Mbilinyi walishinda? Mtu pekee anayeweza kuzungumzia kuhusu tume ya Uchaguzi ni Umma na siyo Vyama Vya Siasa."

"Tume ya utumishi wa umma ndiyo inachakata majina 5 ya Mwenyekiti wa tume ya Taifa ya uchaguzi na kumpelekea Rais ili ateue jina moja"

"Freeman Mbowe anataka tufanye maridhiano lakini sisi na wao hatufikirii pamoja kwenye kile wanachohitaji wananchi hadi sasa"

"Tangu nimekuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM sijawahi kufanya mkutano wa hadhara.
Sisi kama CCM huwa hatufanyi mikutano ya hadhara kwenye majimbo yasiyoongozwa na wanachama wetu, mfano Mbeya ni Jimbo la Joseph Mbilinyi yeye huwa anafanya mikutano lakini akifanya anazungumzia jela kubaya"

"Godbless Lema hajawahi kutembelea miradi ya kimaendeleo Arusha Mjini na akifanya mikutano ya hadhara hazungumzii vitu hivyo bali yeye anazungumza kuhusu Jela tu. Kila tunachokifanya wanasema ni kibaya na sisi hatukatai kushauriwa kwasababu siyo maroboti lakini tangu tumeanza kupewa ushauri hatujawahi kupewa ushauri wa maana."

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Akihojiwa clouds Humphrey polepole amesema wapinzani Ni sawa Corona.

Kauli hii ya kiongozi kijana inaweza tafsiriwa Kama kauli ya kiongozi aliyepoteza dira na ambaye kwake maisha ya watu wasio ccm si kitu bali binadamu sahihi ni mwanaccm.

Niwaomba viongoz wa chama tawala kuchukua hatua kwake na pia vyombo vya dola kumshughulikia kwani kumwacha aendelee na tabia hii kutasababisha wapinzani nao kutumia kauli Kama hizi kujibu mapigo na hivyo kusababisha mgawanyiko kwenye taifa.

Tukumbuke ishu ya MENDE kwa wenzetu...

**********
Amesema ukizuia Watalii kuingia Nchini kwa mwezi mmoja kutokana na #coronavirus italeta shida kiuchumi, hivyo ni kuomba Mungu ugonjwa huu uondoke. #COVID19 ni sawa na wapinzani Nchini

Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi wa CCM, amesema "Tuna vituo Nchi nzima ambavyo vimetengwa kwa ajili ya kuwahudumia waathirika wa ugonjwa wa virusi vya hivyo."

Kuhusu CCM kununua Wapinzani amesema "Si kweli kuwa CCM inatoa fedha kununua Wanachama wa upinzani bali inabidi wapinzani watazame jinsi wanavyoharibikiwa wenyewe ndani kwa ndani"

"Kuna mwanachama wa Mbowe anaitwa Paulina, aliondoka kwenye Chama kwasababu alikuwa anatakiwa kimahusiano na viongozi wake hivyo akaamua kuhama ili kuokoa ndoa yake lakini alivyohama wapinzani wakatafuta kisingizo kuwa amenunuliwa"

Ameongeza, "Chama cha Freeman Mbowe wanaiitana Bwana au Kamanda wao sio ndugu. Katika chama chetu huwa natumia sana neno ndugu na siyo Mheshimiwa kwa kwasababu sisi si kitu bila ya watu waliotupa dhamana"

Aidha, amesema "Hii tume ya Uchaguzi ni huru kabisa kama si huru mbona Halima Mdee na Joseph Mbilinyi walishinda? Mtu pekee anayeweza kuzungumzia kuhusu tume ya Uchaguzi ni Umma na siyo Vyama Vya Siasa."

"Tume ya utumishi wa umma ndiyo inachakata majina 5 ya Mwenyekiti wa tume ya Taifa ya uchaguzi na kumpelekea Rais ili ateue jina moja"

"Freeman Mbowe anataka tufanye maridhiano lakini sisi na wao hatufikirii pamoja kwenye kile wanachohitaji wananchi hadi sasa"

"Tangu nimekuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM sijawahi kufanya mkutano wa hadhara.
Sisi kama CCM huwa hatufanyi mikutano ya hadhara kwenye majimbo yasiyoongozwa na wanachama wetu, mfano Mbeya ni Jimbo la Joseph Mbilinyi yeye huwa anafanya mikutano lakini akifanya anazungumzia jela kubaya"

"Godbless Lema hajawahi kutembelea miradi ya kimaendeleo Arusha Mjini na akifanya mikutano ya hadhara hazungumzii vitu hivyo bali yeye anazungumza kuhusu Jela tu. Kila tunachokifanya wanasema ni kibaya na sisi hatukatai kushauriwa kwasababu siyo maroboti lakini tangu tumeanza kupewa ushauri hatujawahi kupewa ushauri wa maana."
Ukisikia mtu kazungumza pumba ndio kama hizi!!!! Unalinganisha kifo na pesa!!!! Labda sababu anajua yeye atakuwa mbali na hao watalii kwa hiyo poa tu!!! Hao watakao wahudumia hao watalii wakikamata ugonjwa na kufa potelea kwao!!!! Kwetu bei ya Maisha (Uhai) ni rahisi sana. Ingekuwa nchi ambazo raia wana nguvu juu ya seriklia yao huyu bwana alikuwa ajiuzuru haraka sana. Nchi kama Italia inategemea sana utalii lakini imefunga kila kitu au leo sisi ndio tunaijua pesa kuliko wazungu!!!!!??? Inasikitisha sana…...
 
Kj
Unazungumzia wale walevi makada wa UVCCM waliotumwa na Sabaya?Huo upuuzi wenzako hawautumii tena maana umebuma!
Hamkosi kisingizio,jamaa wanaweka wazi miaka ishirini treni ilikuwa haijakanyaga moshi JPM kawezesha barabara mbovu mbunge anakula bata mjini.
 
Back
Top Bottom