Polepole: Wana-CCM tusikae kimya Serikali ikikosea, tuwe wakali na jasiri kukosoa

Kuna binadamu mshipa wa aibu umekatika
Watu waliuawa sababu ya kukosoa awamu ya 5, wengine walipotezwa, wengine walibambikiwa kesi, wengine walitekwa, wengine walinyang'anywa mali zao, wengine walihojiwa uraia wao, wengi accounts zao zilifungwa na wengine wakaporwa fedha zao!! And huyu jamaa anaongea nini?
 
Huyu jamaa mnafiki sana
 
Yupo sahihi.Nchi haieleweki inaelekea wapi.Lazima watu wasikae kimya.Zama za Magufuli hapakuwa na jambo la kukosoa ndio maana watu walikuwa kimya lakini kwa uongozi huu uliopo lazima watu waongee huku tozo,huku umeme,huku maji,kule wapigaji... yaani serikali ya hovyo kabisa
 

Kwa sababu ya ujinga ndio maana watu kama hawa bado wanapewa mda wa kuongea
 
Huyu ni mfano wa viongozi wa Taifa hili miaka hii. A lot of inconsistencies. Hawezi kujua watasimamia jambo gani kwa wakati gani. Wako wengi tu sio huyu peke yake. Kinachosikitisha mpaka wasomi wa highest level yaani maprofessor wamekuwa goigoi tu. Wametupa taaluma wanacheza siasa vumbini na kina Livingstone Lusinde na Mh. MSUKUMA
 
Unaumwa wewe!! Unasema zama za Magufuli kulikuwa hakuna kitu cha kukosoa? Kuna jambo lililitia aibu Taifa kama Lissu kupigwa risasi? Watu waliohoji wengine si walitimuliwa chama na uwaziri? Jambazi lililokuwa linalindwa na Magufuli limehukumiwa miaka 30, kesi ya Mrosso nayo anapigwa 30 nyingine, eti Magufuli ndiyo alikuwa anataka kumpa ukuu wa mkoa huyo! Taja Upigaji mmoja uliofanyika awamu ya 6
 
Lissu kupigwa risasi au kutopigwa ingepeleka maji kwa wakazi zaidi ya 47,000 kijiji cha Busekelo? Hoja za kipumbavu kabisa! Au unadhani watanzania ni wajinga na siasa zenu uchwara??
 
Lissu kupigwa risasi au kutopigwa ingepeleka maji kwa wakazi zaidi ya 47,000 kijiji cha Busekelo? Hoja za kipumbavu kabisa! Au unadhani watanzania ni wajinga na siasa zenu uchwara??
Awamu ya 5 ilikuwa ni awamu ya uovu kuliko awamu zote zimewahi kutokea nchi hii, kudhihirisha hilo "Mother nature" itself ikaamua "kurara nayo mbere", Kwa mara ya kwanza kikatokea kitu hakijawahi kutokea nchi hii....Nitajie upigaji kwenye awamu ya 6 Mkuu, hujanijibu hilo swali
 
Unaandika kama mtu mwenye mihemko asiye na akili timamu.Awamu ya uovu imetenda mambo makubwa mno watanzania tumejionea! Wala haihitaji nguvu kubwa kuelezea.Wakulima wamefurahia pembejeo za kilimo! Bodaboda wamenufaika na miundombinu ya kisasa! Wagonjwa wamefaidika na huduma bora za afya! Waliokuwa wanakufa kwa ubovu wa miundombinu wakielekea hospital wamenusurika! N.k n.k kama ndio uovu huo! Hakika ulikuwa uovu bora kabisa! Watanzania tumeukubali kabisa 100%
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…