Police Brutality in Tanzania: The World has a Right to know!

Police Brutality in Tanzania: The World has a Right to know!

Na
EDO KUMWEMBE

SIKU Fulani ya maisha yako. Hakutakuwa na wale walinzi kando yako. Hakutakuwa na rafiki zako kando yako. Hakutakuwa na wale washkaji zako wa mtaani kwako. Hakutakuwa na wale wapambe wako kando yako. Hata kama watakuwepo hautawaona.
Pua zako zitakuwa zimewekwa pamba ndani ya jeneza. Foleni ya watu itakuwa ikikuaga. Hautakuwa na fahamu. Ina maana atakayeshika kifua chako hatasikia mapigo yoyote. Hautajua kama anayekuaga ni rafiki yako au adui yako. Mama yako na dada zako kando ya jeneza watakuwa wakilia wakiliwazwa na rafiki zako, ndugu na jamaa zako.
Kaka zako watakuwa bize sana kuhakikisha watu wote walio msibani wanapata mahitaji yao. Mmoja atakuwa anahakikisha kila mtu amekula. Mwingine atakuwa akifarijiwa na rafiki zako wa karibu. Mwingine atakuwa kaburini kuhakikisha kaburi lako limechimbwa vema. Mwingine atakuwa anaongea na sheikh au askofu kuhusu mpangilio mzima wa mazishi.
Kama una cheo kikubwa sana basi wakubwa waliobaki watakuwa wanapiga saluti mbele ya jeneza lako. Hata hivyo haitasaidia sana. Haitakurudishia pumzi. Kama ulikuwa mwanamuziki mahiri sana, bado haitakurudishia pumzi. Alikufa Michael Jackson na bado hajarudishwa.
Kama ulikuwa kiongozi maarufu bado haitasaidia. Alikufa Mwalimu Nyerere na bado hajarudishwa. Alikufa Nelson Mandela, alikufa Martin Luther King, alikufa JF Kennedy. Wote hawa hawajarudi tena. Kila siku tunapita kando ya makaburi yao na kuishia kusema “Walikuwa mashujaa”. Lakini mbona hawanyanyuki chini ya udongo na kusimama?. Kumbe hawakuwahi kuwa wakubwa kuliko wewe.
Kuna mkubwa mmoja tu ambaye hapigiwi saluti lakini anabakia kuwa mkubwa. Anaitwa Mungu. Kwanini uringa sana hapa duniani? Ni swali linaloendelea kushangaza sana. Wakati mwingine maisha yanashangaza sana. Sana. Sana. Kuliko tunavyofikiri.
Wakati tukikaribia kukuaga, mtu ambaye ataendelea kuheshimika kwa muda tu, ndani ya siku hiyo, atakuwa MC wa shughuli hiyo. Hautaweza kumpinga. Yeye ndiye ambaye atatuambia muda gani ‘utabebwa’ kwenda eneo moja kwenda jingine. Yeye ndiye ambaye atatuambia muda wa maziko, muda wa kula, muda wa kwenda makaburini. Yeye ndiye ambaye kwa mbwembwe atatuambia matanga au Arobaini yatakuwa lini.
Leo utakuwa na mbwembwe nyingi katika kundi la mashabiki wa muziki wako wanaokuhusudu. Leo utakuwa na mbwembwe nyingi kwa walinzi wanaokulinda na silaha. Leo utakuwa katika baa Fulani ya sehemu Fulani ukitoa kila amri ambayo wanyonge wanatekeleza bila ya kuguna. Unalipa bili unaondoka. Lakini duniani kuna mkubwa mmoja tu.
Wakati mwingine unajidanganya kuwa unachofanya ni sahihi. Lakini mbona hautaki kusikiliza mawazo tofauti Edo? Ni kwa sababu ya maisha ya kidunia ambayo wakati mwingine huwa tunadhani ni marefu sana. Wakati mwingine huwa tunadhania kwamba tulizaliwa kabla ya Mlima Kilimanjaro.
Kama ungepewa pumzi ya kutafakari wakati tukikupeleka futi sita chini ya ardhi ndipo utakapogundua kuwa kuna vitu vilikuwa vikubwa kuliko wewe. Ndipo utakapogundua kuwa ile bahari ya Indi pale Coco Beach na kwinginepo ilikuwepo kabla ya wewe.
Tenda mema kadri unavyoweza. Hili sio suala la dini wala kabila wala rangi. Kuna sehemu mwanadamu unakosea sana lakini kiburi cha pumzi za muda ndicho ambacho kinatusumbua kwa sasa. Mwisho wa siku pumzi zikiisha tutaondoka makaburini kurudi nyumbani kwako na kuanza kuongelea maisha mengine ya duniani.
Nyakati hizo wengi tutajikumbusha kimoyomoyo kwamba kuna mkubwa mmoja tu ambaye anapaswa kututia hofu na sio wewe ambaye dakika chache zilizopita tulikuwa tumetoka kuweka mikono ya sala kando ya kaburi lako na kurudi nyumbani kwako kuondoa tarubai angali ukiwa haupo.
Hapa namzungumzia kila mtu mwenye madaraka makubwa na madogo, umaarufu, au pesa au hulka ya kujisikia kuliko wengine. Binafsi nilizaliwa nikiwa uchi juu ya kitanda fulani cha hospitali ya Ocean Road kuelekea mwishoni mwa miaka ya 1970. Siku nikipoteza pumzi watakaonizika wanaweza kuamua nizikwe nikiwa uchi. Maringo ya nini?
Ni nyakati tata katika nchi yetu. Katika ngazi ya mtu binafsi au taasisi zetu au serikali Kuu. Kuna sehemu tunakosea sana kwa kujiamini kupita kiasi. Maringo ya mwanadamu yanazidi kupitiliza. Inakera sana. Wengi wanafunga mdomo. Wengi wana hofu. Nilikuwa nawakumbusha tu, kuna mkubwa mmoja tu. MUNGU.
Usijivunie kuwa bosi wa Chadema. Usijivunie kuwa na sauti kubwa kwa Waislamu au Wakristo. Usijivunie kuwa bosi wa CCM. Usijivunie kuwa kiongozi mkubwa. Usijivunie kuwa tajiri wa mtaani kwako. Kuna sehemu moja unakosea sana.
Mwanamuziki Sunday Mjeda ‘Linex’ aliwahi kulalamika katika wimbo wa “Moyo wa Subira’ akitamani kurudisha nyakati nyuma arekebishe ubaya aliowahi kuufanya. Uzuri kwa Mungu, au ubaya kwetu, ni kwamba wakati watu wakitawanyika katika misiba yetu hatutaweza kurudisha nyakati nyuma. Ni nyakati hizo ndipo tutajua kwamba kuna mwanaume mmoja tu. MUNGU.
Walionielewa vizuri nadhani watakuwa wamenielewa vizuri sana, hasa kwa kila kitu kinachoendelea katika nchi yetu kwa sasa. Life goes on. Kuna Mungu mmoja tu. Na kuna mimi mmoja tu. Edo kumwembe. Na kuna wewe mmoja tu, unayesoma Makala hii. TUTAFAKARI.
Mbwembwe tu.
 
Wanabodi, tusiwalaumu sana vijana wa kamanda Sirro, as if tukio la kifo cha Akwilina ndio mwanzo!. Hawa hizi ndio zao!.

Polisi hawakuanza leo matukio kama haya, hivyo hapa ni katika kukumbushana tuu, mambo kama haya yaliishatokea huko nyuma, yametokea sasa, na yatatokea tena!. Tutakumbushana!.
P
 
When you are under the regime where human beings are treated like discarded animals, then there is a need to sit down and evaluate our decisions.
 
Of course sycophants like you will say or do anything to give excuses for this uncouth and evil regime, that what idiots do believing they are somewhat safe, for now. Contrary to what you insinuate about police brutality worldwide ours is state-sponsored police brutality witnessed mostly in similar fascist regimes. In the US any action that results in injury or loss of life investigation is immediately begun and if there is any wrong-doing, action is taken and culprits punished.

Your are terribly misinformed about USA my friend…but what else would you know with the state of the mind you are in!? Oh did I read right that you are really against police brutality, that would be very funny coming from u…your abusive language speaks a lot about you!…what about verbal brutality from your side, where do people run to!? People like you have no right to point fingers to whatever kind of brutality one can talk about. With your kind of sentiment I wonder the kind of treatment one would receive from you incase you are a police officer holding a gun! That goes without saying how brutal/harsh you would treat someone like me who don't necessarily share your self centered, egocentric opinion!

Your abusive language put you at same level of psychiatric patient who really need psychoanalysis and prompt psychiatric treatment. In my opinion, psychoanalysis to all our men & women in uniform should be a routine treatment so that they receive prompt treatment before they commit atrocities!
 
This is so nice news for ccm members and their blool thirsty chairman
 
Naona maLandcruiser ya Makonda yakiwa kazini, hii sio Tanzania tunayoijua, hatujazoea vurugu jamani, sisi ni amani tu.
 
Wakuu ni ombi tu hizi picha zinazidisha hasira kwa wale walio namna moja au nyengine athirika na fujo au matukio hayo. Sidhani kama ni busara kuziweka kwani unachochea chuki katika jamii!! Ni mtazamo tu.
Zisipoonyeswa wataongeza kazi ya kutuua, maana watadhani hatujui.
 
Wanabodi, tusiwalaumu sana vijana wa kamanda Sirro, as if tukio la kifo cha Akwilina ndio mwanzo!. Hawa hizi ndio zao!.

Polisi hawakuanza leo matukio kama haya, hivyo hapa ni katika kukumbushana tuu, mambo kama haya yaliishatokea huko nyuma, yametokea sasa, na yatatokea tena!. Tutakumbushana!.
P
Kwa hio tuyaache yaendelee?
 
Bashite aliwaambia wasipige mabomu ya machozi wapige risasi wananchi waanze kuzizoea.
Somo nililojifunza: ukisikia mlio wa bunduki ujue haijakupata, songa mbele.
 
Wamefundishwa. Kwenye sheria ya Jeshi la Polisi kuna kifungu hiki:

29.-(1) Any police officer may use arms against–
(a) any person in lawful custody charged with or convicted of an offence when such person is escaping or attempting to escape where such police officer has reasonable ground to believe that he cannot otherwise prevent the escape and has given a warning to such person that he is about to use such arms against him and such warning is unheeded;
(b) any person who–
(i) by force, rescues or attempts to rescue any other person from lawful custody; or
(ii) by force, prevents attempts to prevent the lawful arrest of any other person, where such police officer has reasonable ground to believe that he or any other person is in danger of grievous bodily harm and that he cannot otherwise effect such arrest or prevent such rescue.
 
Wanabodi, tusiwalaumu sana vijana wa kamanda Sirro, as if tukio la kifo cha Akwilina ndio mwanzo!. Hawa hizi ndio zao!.

Polisi hawakuanza leo matukio kama haya, hivyo hapa ni katika kukumbushana tuu, mambo kama haya yaliishatokea huko nyuma, yametokea sasa, na yatatokea tena!. Tutakumbushana!.
P
 

Attachments

z.jpg


Toa maoni yako mdau......
 
Back
Top Bottom