Polisi jifunze namna bora ya kuishi na jamii

Polisi jifunze namna bora ya kuishi na jamii

Damaso

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2018
Posts
3,978
Reaction score
6,739
Ni asubuhi umeamka zako na unajiandaa kwa ajili ya kwenda kazini ila ghafla unasikia sauti yenye ukali mlangoni kwako ikikutaka utoke nje, unaamua kufungua unakutana na mtu ambaye amevaa jeans na jezi ya Man United pamoja na kofia nyeusi ya New York. Anajitambulisha kuwa yeye ni afisa wa Polisi kutoka Kituo cha jirani hapo na hana hata kitambulisho na anahitaji uongozane naye muende kituo kwa sababu kuna kesi anahitaji kukuhoji.​
1727885649110.png

Ile unamuelekeza kuwa akusubirie upate kuweka mambo sawa, huyu mtu anayedai kuwa ni polisi anachomoa pocket knife na kukutishia kuwa unataka uondoke naye. Najiuliza kama ni wewe utakubali kuondoka naye au utamfundisha na kujilinda kikatiba? Binafsi atachagua anipeleke huko akanihoji nikiwa maiti au yeye abakie maiti ndani kwangu.

Hakuna ambaye kwa sasa ana imani tena na jeshi la Polisi wala huruma, matendo ya maafisa hawa yamefanya jamii iwaone watu wa tofauti kabsa, sio kwa ubaya ila wanafuata maagizo ambayo mengine sio maagizo yenye maana za msingi kabsa. Polisi na akili zako timamu kabsa unamshambulia kwa silaha mtu ambaye hana wembe wala pini? Na unasema kuwa unatuliza ghasia?​
1727884451466.png

Kuna baadhi ya maagizo yamekuwa yakiwafanya watu ndani ya jamii wawe na mioyo migumu. Jambo baya kama vifo au ulemavu kwa afisa wa polisi basi ni sherehe kubwa sana kwa wananchi na wanamshukuru Mungu.

Nikupe mfano, Umetoka usiku kwenye starehe zako ukaona Askari polisi amevamiwa na kupigwa na vibaka kisha kuwekwa kwenye kichaka akiwa hoi bin taabani, ukimtazama yule askari unamfahamu vyema kabsa na ni moja ya wale maaskari wababe, SWALI, je utatoa msaada wa kumsaidia na kutoa taarifa kwenye kituo cha polisi kuwa kuna askari amekutana na vibaka na kujeruhiwa?
1727884616358.png

Je wakikugeuzia kibao kwamba wewe ni mmoja wa wale vijana waliomjeruhi askari wao, ni nani atakusaidia? Nafahamu kwa hali ilivyo, watu wengi watamuacha pale pale huyo askari yeye na Mungu wake.
1727884553865.png

Maafisa usalama nao ni watu ambao tunaishi nao ndani ya jamii, tunaishi na wazazi wao, watoto wao na ndugu zao, tunakwenda kwenye sherehe zao za harusi, vipaimara, send off, lakini pia tunahusika kwenye kuwafariji kwenye misiba na nyakati ngumu kama ugonjwa au ulemavu, ni moja ya sehemu ya jamii yetu tunaishi nao.

Ila ajabu, wanajisahau sana na kuona wao wapo mbingu tofauti na ile ambayo tunaishi sisi, wanaishi kana kwamba wao sio sehemu ya jamii kabsa. Hivi huwa wanakwenda Makanisani na misikitini kweli au ndo wapagani!? Jumapili mnakwenda kanisani kufanya nini, Ijumaa mnakwenda kufanya nini?​
1727884840403.png

Sio kitu kizuri kusikia kuwa askari fulani nyumba yake imepata hitilafu ya umeme na kutetekea huku majirani wakikataa kutoa msaada wa kuzima moto, kiubinadamu ni suala ambalo sio jema ila kwa upande mwingine mioyo ya watu hujisikia vizuri wakiona askari na maafisa usalama wakipata uchungu sawia na ule wanaoupata wananchi na familia zao.

Rai yangu, IGP pamoja na wasaidizi wako na maafisa polisi wafundishe kuwa na utu haswa linapokuja suala la kuishi na wanajamii. Andaeni semina na warsha mbalimbali na waalikeni wataalamu wa saikolojia wapate kuwafundisha maaskari kuwa jamii wanaoishi inajifunza kuhusu matendo yao, wakumbushe kuwa “Muosha ipo siku ataoshwa”, leo wanafurahi kuona maumivu ya wanafamilia wa Savita ila wakisikia vijana wao wamekutana na kadhia hii ya Savita, basi watahuzunika sana.
1727884719571.png
Mkitaka kufahamu kuwa wananchi kwa sasa hawana tena huruma wala mioyo ya huzuni kwenye misiba, tazama taarifa kuhusu askari wa Kikosi cha Valantia (KVZ) Haji Machano Mohamed, ukitembelea ukurasa wa Facebook wa Millard Ayo pamoja na Ukurasa wa EATV, utakutana na comments za watu zikisifia kabsa na kuridhika kusikia taarifa za mtu kupoteza maisha. Taarifa za kifo cha A/INSP Eliuterius Hyera, ambaye alikuwa Mkuu wa Kituo Kidogo cha Polisi Chiungutwa wilayani Masasi Mkoani Mtwara.​
Screenshot_20241002_190422_Lite.jpg

Yaani ukitegemea kukutana na jumbe za watu za pole ndo kwanza watu wanashukuru kuona kumbe na Maafisa Polisi nao wanaweza kupoteza maisha. Yaani tunategemea kuona watu wakitoa pole ila ndo kwanza unakutana na nukuu ya kauli ya Rais Samia kuwa Kifo ni Kifo tu.

Hivi kweli tumepoteza utu kiasi cha kwamba Polisi wanaona ni sawa kupoteza maisha ya mtu ili tu wapate kuonekana wanachapa kazi kwa kiongozi fulani? Yaani maisha ya Akwilina yalikuwa ni sadaka kwa askari ambao walipokea maagizo kutoka kwa Kamanda Lazaro Mambosasa? Hivi Biswalo Mganga unajisikiaje ulipoamua kufunga jalada la kesi ya Akwilina kwa kigezo cha Jeshi la Polisi linapotumia nguvu kuzuia maandamano au vurugu na kusababisha mauaji, haliwezi kushtakiwa.​
1727885208436.png

Familia yako inakuchukuliaje ukiwa kama Baba na kuamua kuzima kesi ya binti ambaye kwao walimtazama kama sehemu ya msingi wa familia. Yaani polisi sita ambao walikuwa wanatakiwa wahojiwe, wewe Biswalo Mganga kwa utashi wako tu ukaamua kufunga jalada la kesi na kuwaeleza wananchi kauli isiyo na mashiko. Shame on you Biswalo Mganga na Lazaro Mambosasa.

Maafisa polisi kumbukeni mnaishi na watu, na wanawatazama ipo siku ingawa siombei lakini mtaanza kuona kuna mikosi na vifo vya ajabu ndani ya familia zenu, msianze kuuliza fahamu kuwa nature ya maisha huwa haidanganyi, law of nature ipo kazini ikishirikiana na karma. Kama watu watashindwa kuwashughulikia na kuwaonesha namna nzuri ya maisha ipo siku mtakutana na vitu vizito.​
1727885260813.png

Maagizo yapo ila fahamuni kuwa mnaishi na watu, sabuni, chumvi na vocha utaenda kununua kwa Mangi, Ukipata hitilafu ya umeme utamuita Side akusaidie, septic tank limejaa maji machafu utamuita Eze pamoja na wenzake waje kukusaidia kuzibua.​

MAISHA NI KUSAIDIANA PAMOJA NA KUISHI KWA WEMA! JIFUNZENI WEMA!
 
Kwa kipindi cha hivi karibuni taswira ya Polisi imezidi kuchafuka, polisi inaonekana ipo dhidi ya wananchi na sio kuwasaidia wananchi..
 
Kwa kipindi cha hivi karibuni taswira ya Polisi imezidi kuchafuka, polisi inaonekana ipo dhidi ya wananchi na sio kuwasaidia wananchi..
Ukisikia polisi jirani yako amevamiwa na anapewa kichapo je utaenda kumsaidia!??
 
Inasikitisha

Imani ilitakiwa iwe kwamba ikitokea mtu kauwawa na polisi watu kiotomati waassume 'huyo atakuwa alikuwa na ubaya maana polisi wanalinda raia tu' bila utata.

Saaa inapokuwa kinyume chake asee ni kuisikitikia tu hiyo nchi maana ufalme hauwezi kufitinika ndani kwa ndani na ukaendelea kusimama. We sikia, wizara ya mambo ya NDANI!!.

Hiyo ni sambamba na mahakama inatakiwa ikitoa hukimu watu waasume kiotomati kwamba hiyo ndiyo haki yenyewe inavyotakiwa. Sio kuwa kinyume chake watu waanze kujiuliza kuwa labda inawezekana kaonewa, au hakuwa na hela tu ila asingehukumiwa vile.

Hapo tukifikia huko ni suala la muda tu maana kama sentensi ya HAKI HUINUA TAIFA ni ya kweli basi pia UOVU UKITAMALAKI MAHALA ILIPOTAKIWA KUWA HAKI KINACHOFUATA NI KUANGUKA KWA TAIFA.

Tuwe makini, nafasi bado tunayo
 
Ukisikia polisi jirani yako amevamiwa na anapewa kichapo je utaenda kumsaidia!??
Hakika, maana baada ya kazi akirudi anarudi na kuwa miongoni mwa wanajamii kwenye jamii ileile. Naamini atajifunza mengi kutoka kwenye msaada huo.
 
Inasikitisha

Imani ilitakiwa iwe kwamba ikitokea mtu kauwawa na polisi watu kiotomati waassume 'huyo atakuwa alikuwa na ubaya maana polisi wanalinda raia tu' bila utata.

Saaa inapokuwa kinyume chake asee ni kuisikitikia tu hiyo nchi maana ufalme hauwezi kufitinika ndani kwa ndani na ukaendelea kusimama. We sikia, wizara ya mambo ya NDANI!!.

Hiyo ni sambamba na mahakama inatakiwa ikitoa hukimu watu waasume kiotomati kwamba hiyo ndiyo haki yenyewe inavyotakiwa. Sio kuwa kinyume chake watu waanze kujiuliza kuwa labda inawezekana kaonewa, au hakuwa na hela tu ila asingehukumiwa vile.

Hapo tukifikia huko ni suala la muda tu maana kama sentensi ya HAKI HUINUA TAIFA ni ya kweli basi pia UOVU UKITAMALAKI MAHALA ILIPOTAKIWA KUWA HAKI KINACHOFUATA NI KUANGUKA KWA TAIFA.

Tuwe makini, nafasi bado tunayo
Well said Mkuu
 
Hakika, maana baada ya kazi akirudi anarudi na kuwa miongoni mwa wanajamii kwenye jamii ileile. Naamini atajifunza mengi kutoka kwenye msaada huo.
Wanasahau kuwa wanakula vyakula mitaani! Je wana imani gani kuwa hizo chips ni salama, je kama kuna sumu!?? Uhasama unaweza kuchipuka taratibu kizembe zembe tu!
 
Umenena kwa hekima sana na ubarikiwe.
Mimi police hata kama akiwa ni mdogo wangu undugu umeishia hapo tutakuwa tunakutana msibani
Hawa siwezi kutoa msaada wowote ule. watu wapuvu walio feli darasani hadi maisha.
Binafisi siwapendi na sitokaa niwapende hawa.
 
Malipo ni hapahapa duniani

ndio maana wengi wao hata akistaafu na cheo kikubwa na mafao tele lakini bado wanakuwa hawana amani na utulivu maisha

wengi wanapenda kitonga na ubabe
 
Umenena kwa hekima sana na ubarikiwe.
Mimi police hata kama akiwa ni mdogo wangu undugu umeishia hapo tutakuwa tunakutana msibani
Hawa siwezi kutoa msaada wowote ule. watu wapuvu walio feli darasani hadi maisha.
Binafisi siwapendi na sitokaa niwapende hawa.
Ukitazama ndani ya jamii sio watu waoga wanaweza kumfanyia yete ubaya au hata familia. Yaani kosa la mdogo wako basi familia nzima mnalipa 😔 wajitazame tena maana imefika hatua watu wanashukuru kuona askari amefariki.
 
Malipo ni hapahapa duniani

ndio maana wengi wao hata akistaafu na cheo kikubwa na mafao tele lakini bado wanakuwa hawana amani na utulivu maisha

wengi wanapenda kitonga na ubabe
Ni huzuni sana
 
Back
Top Bottom