LGE2024 Polisi: Kada wa CHADEMA aliyefariki alipata ajali ya Bodaboda akiwa amelewa

LGE2024 Polisi: Kada wa CHADEMA aliyefariki alipata ajali ya Bodaboda akiwa amelewa

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
photo_2024-11-01_18-48-43.jpg

Tumeshuhudia kupitia mitandao ya kijamii ikitolewa taarifa ya kutaka kuupotosha umma kuhusiana na kifo cha Joseph Remigius, Miaka 52 mkazi wa Kijiji cha Karagara, Wilaya ya Misenyi Mkoa wa Kagera ambaye alikuwa ametia nia ya kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Kijiji kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Taarifa sahihi ni kwamba Oktoba 31, 2024 Joseph Remigius majira ya saa tatu usiku akiwa anatoka kwenye Bar waliyokuwa wanakunywa pombe akiwa amebebwa na bodaboda walipata ajali na baada ya ajali hiyo walipata msaada na kufikishwa katika Kituo cha Afya Minziro na kupatiwa matibabu na kuruhusiwa.

Novemba 1,2024 majira ya saa kumi na dakika ishirini alfajiri ndipo zikapokelewa taarifa katika Kituo Kidogo cha Polisi Minziro kuwa Joseph Remigius amefariki dunia akiwa nyumbani kwake.

Hivyo hadi sasa kulingana na ushahidi wa mashuhuda wa ajali na waliompatia msaada na kumfikisha katika Kituo cha Afya Minziro, ajali ndiyo chanzo cha kifo chake. Endapo kuna mwenye ushahidi tofauti na huo wa mashuhuda wa ajali basi aufikishe Polisi ili ufanyiwe kazi.

Imetolewa na:
David A. Misime - DCP
Msemaji wa Jeshi la Polisi
Dodoma, Tanzania.

Pia soma ~ Missenyi, Kagera: Kada CHADEMA, Joseph Elemedius auawa akingojea Uteuzi kugombea Serikali za Mitaa
 
Ndugu zangu Watanzania,

Jeshi la polisi Nchini limekanusha vikali taarifa za upotoshaji zinazoenea mitandaoni juu ya kifo cha kada wa CHADEMA aliyefariki Dunia .ambapo taarifa hizi za upotoshaji zinahusisha kifo chake na masuala ya siasa hasa kutia nia kwake.

Na hii ndio taarifa yake👎
Screenshot_20241101-190205_1.jpg


Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Jeshi la polisi Nchini limekanusha vikali taarifa za upotoshaji zinazoenea mitandaoni juu ya kifo cha kada wa CHADEMA aliyefariki Dunia .ambapo taarifa hizi za upotoshaji zinahusisha kifo chake na masuala ya siasa hasa kutia nia kwake.

Na hii ndio taarifa yake👎View attachment 3140830

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Shahawa nyingine heri zingemwagwa chooni tu
 
Acha
Mbowe aliporomoka kwenye ngazi akiwa amelewa Joyce Mukya akadhani amekufa akatimua mbioo.
Hospital kadanganya eti kakanyagwa na wanaume watatu.
Chadema wamezoea ulevi na uongo.
Acha kuwa na mabezo
Kuwa na utu
Hizo siasa na vyeo vya watu visikutoe utu
Haya amekufa umefurahi kama utamla nyama
 
Mbowe aliporomoka kwenye ngazi akiwa amelewa Joyce Mukya akadhani amekufa akatimua mbioo.
Hospital kadanganya eti kakanyagwa na wanaume watatu.
Chadema wamezoea ulevi na uongo.
Unapata faida gani kutoa kauli za uongo..

Ile kesi ya ugaidi iliishiaga wap??!
 
Ndugu zangu Watanzania,

Jeshi la polisi Nchini limekanusha vikali taarifa za upotoshaji zinazoenea mitandaoni juu ya kifo cha kada wa CHADEMA aliyefariki Dunia .ambapo taarifa hizi za upotoshaji zinahusisha kifo chake na masuala ya siasa hasa kutia nia kwake.

Na hii ndio taarifa yake👎View attachment 3140830

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Sasa hapa Mama anaingiaje kwa mfano
 

Tumeshuhudia kupitia mitandao ya kijamii ikitolewa taarifa ya kutaka kuupotosha umma kuhusiana na kifo cha Joseph Remigius, Miaka 52 mkazi wa Kijiji cha Karagara, Wilaya ya Misenyi Mkoa wa Kagera ambaye alikuwa ametia nia ya kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Kijiji kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Taarifa sahihi ni kwamba Oktoba 31, 2024 Joseph Remigius majira ya saa tatu usiku akiwa anatoka kwenye Bar waliyokuwa wanakunywa pombe akiwa amebebwa na bodaboda walipata ajali na baada ya ajali hiyo walipata msaada na kufikishwa katika Kituo cha Afya Minziro na kupatiwa matibabu na kuruhusiwa.

Novemba 1,2024 majira ya saa kumi na dakika ishirini alfajiri ndipo zikapokelewa taarifa katika Kituo Kidogo cha Polisi Minziro kuwa Joseph Remigius amefariki dunia akiwa nyumbani kwake.

Hivyo hadi sasa kulingana na ushahidi wa mashuhuda wa ajali na waliompatia msaada na kumfikisha katika Kituo cha Afya Minziro, ajali ndiyo chanzo cha kifo chake. Endapo kuna mwenye ushahidi tofauti na huo wa mashuhuda wa ajali basi aufikishe Polisi ili ufanyiwe kazi.

Imetolewa na:
David A. Misime - DCP
Msemaji wa Jeshi la Polisi
Dodoma, Tanzania.

Pia soma ~ Missenyi, Kagera: Kada CHADEMA, Joseph Elemedius auawa akingojea Uteuzi kugombea Serikali za Mitaa
Ueni tu ila mjue kila anayeua kwa upanga naye atakufa kwa upanga
 
Back
Top Bottom