Polisi kuwapiga raia huu ujeuri wanautoa wapi? Naomba mwenye ushahidi wowote wa raia wa Tanzania kupambana na Polisi auweke hapa

Polisi kuwapiga raia huu ujeuri wanautoa wapi? Naomba mwenye ushahidi wowote wa raia wa Tanzania kupambana na Polisi auweke hapa

Kwa jinsi anavyohangaika asipokuwa makini yatamshinda.
Yatamshinda kwa sababu amekataa kupelekeshwa na tantalila za Chadema?

Polisi wamekuwa hivyo miaka mingi toka enzi za Mkapa, Kikwete na Magufuli.

Na si Tanzania peke yake. Kwani kilio cha "defund the police" huko Marekani unafikiri ni kwa sababu gani?

Au kule Nigeria na "end SARS"?

Kama ni kudeal na police incompetence na police brutality msitake kuchanganya na mambo yenu ya siasa.

Police ni taaluma na ishughulikieni kitaaluma. Basi.
 
Tatizo wanachapwa ni wale wanakulitafuta.

Ndio maana hampati sapoti kutoka kwa wananchi wote.
 
Tatizo wanachapwa ni wale wanakulitafuta.

Ndio maana hampati sapoti kutoka kwa wananchi wote.
Mawazo ya kipumbavu kama haya yanasababishwa na ujinga ambao ni mtaji mkubwa wa CCM. Polisi kufanya mazoezi mtaani ni ulimbukeni na ukimtazama huyo afande anayetishia kuwapa raia kipigo cha mbwa koko, unaona moja kwa moja kwamba hana tofauti na kibaka wa mtaani ni vile tu kavaa magwanda.

Upuuzi kama huu huwezi kuuona popote pale isipokuwa hapa Bongo. Bahati yao ni kwamba Watanzania wana uvumilivu usio na mfano. Polisi aliyeiva kimafunzo hawezi kufanya ujinga huo, ni vile tu wengi wamefika walipo kupitia UVCCM. Kama alivyowahi kuonya Baba wa taifa, aliyeonja nyama ya mtu haachi.

Polisi wa namna hiyo ni sadists, wengi wao ni wagonjwa kiakili...bila kumwaga damu hawapati usingizi na hata sura zao zinaonesha walivyo na hamu ya kuumiza. Ukatili na kuumiza raia kunawapa raha!
 
Mawazo ya kipumbavu kama haya yanasababishwa na ujinga ambao ni mtaji mkubwa wa CCM. Polisi kufanya mazoezi mtaani ni ulimbukeni na ukimtazama huyo afande anayetishia kuwapa raia kipigo cha mbwa koko, unaona moja kwa moja kwamba hana tofauti na kibaka wa mtaani ni vile tu kavaa magwanda.

Upuuzi kama huu huwezi kuuona popote pale isipokuwa hapa Bongo. Bahati yao ni kwamba Watanzania wana uvumilivu usio na mfano. Polisi aliyeiva kimafunzo hawezi kufanya ujinga huo, ni vile tu wengi wamefika walipo kupitia UVCCM. Kama alivyowahi kuonya Baba wa taifa, aliyeonja nyama ya mtu haachi.

Polisi wa namna hiyo ni sadists, wengi wao ni wagonjwa kiakili...bila kumwaga damu hawapati usingizi na hata sura zao zinaonesha walivyo na hamu ya kuumiza. Ukatili na kuumiza raia kunawapa raha!
Una mizigo mingi kichwani ipunguze,upumue kidogo.

Adui wa chadema sio polisi,sio ccm,sio rais,wala si katiba.ni mtazamo wao.
Kudhani tu polisi ni watii kwa ccm sababu hawana akili ni sehemu tu ya ugonjwa mkubwa mlio nao.
Polisi hawakatazwi popote kukimbia mtaani,maana hata ofisi zao ziko mtaani pia.
Swala la umasikini wao bado ni mtambuka,maana kuna polisi bado wanakuzidi kipato pamoja na kuitumikia kwao ccm.

Mtambueni kwanza adui yenu kiundani,mtapata kuungwa mkono mpaka na mawe.
 
Tabia ya polisi wa Tanzania kuwatisha, kuwapiga na kuwaumiza wananchi wanaotumia haki yao ya kuhoji utendaji wa serikali inazidi kuota mizizi na kuibua maswali kuhusu wajibu wa polisi kwa raia wanaotuhumiwa kuvunja sheria.

Kwa hali isiyoeleweka Polisi wa Tanzania wameamua kutoheshimu uhuru wa mikusanyiko na uhuru wa mawazo kama ilivyooanishwa kwenye Katiba kama vile ni uvunjaji wa sheria na hivyo kujipa mamlaka ya kuwaadhibu watuhumiwa kwa vipigo.

Kauli za maafande wa polisi katika miaka ya karibuni imezidi kuwa ya kibabe na ya kiuonevu kiasi cha kutishia amani ya nchi kama wananchi wataamua kujibu mapigo kama invyotokea katika mataifa mengine ndani na nje ya Afrika.

Imekuwa kawaida polisi, ambao jukumu lao la msingi ni kuwalinda raia na mali zao, wamesikika wakitoa kauli za vitisho utadhani muda wote wako vitani na raia ambao kimsingi ndio waajiri wao kupitia serikali yao waliyoichagua wao.

Baadhi ya kauli hizo ni kama ifuatavyo...
  • Wanaopanga kuandamana kesho watakiona cha moto
  • Wakiandamana watapigwa kama mbwa koko.
  • Watu watakaoandamana kwa amani watapigwa hadi wachakae
Kwa kauli kama hizi, wananchi waelewe nini? Kwa nini vyombo ambavyo vinatakiwa kulaani kauli kama hizi viko kimya? Hii jeuri ya polisi mbona imeachwa kukomaa hadi polisi kuonekana wako juu ya sheria? Kwa nini serikali haikemei kauli kama hizi? Je ni serikali inawatuma na kuwaruhusu polisi kuwaumiza wananchi?

Katika ombi langu hapo juu, nimeomba mwenye ushahidi wowote wa raia wa nchi hii kujibu mapigo kama inavyotokea katika nchi nyingine auweke hapa. Binafsi sina, ila naona kila mara polisi wakitoa vipigo kwa raia wasio hata na fimbo.

Hawaishii kupiga tu watu wazima wanaume kwa wanawake, wamethubutu kuwapiga hadi vitoto wa shule na hakuna tamko lolote limewahi kutolewa na vyombo vyenye jukumu la kuhakikisha raia wanatendewa haki.

Watu wanapigwa kabla ya kukamatwa, wanapigwa baada ya kukamatwa, wanapigwa wakiwa mikononi mwa polisi tayari iwe ndani ya gari au kwenye vituo vya polisi kama vile jukumu la polisi kwa sasa ni kupiga, kuumiza na hata kuua.

Watu waliokamatwa wamefikishwa mahakamani wakiwa na majeraha makubwa hadi kutembea wanashindwa lakini sijawahi kuisikia hata Mahakama ikitaka kujua kilichotokea au hata kuhoji kwa nini mtuhumiwa anachechemea.

Wananchi wamekamatwa majumbani wakiwa na afya zao lakini baada ya muda mfupi kwenye kituo cha polisi, wanapelekwa mahakamani wamebebwa hawawezi kutembea. Je ni kitu gani kinawapata hawa raia kwenye vituo vya polisi?

Juzi nimemsikia IGP mwenyewe kwa kauli yake akiwatishia wananchi waliopanga kufika mahakamani kusikiliza kesi ya Mbowe aliyeshtakiwa kwa kosa la ugaidi kwamba wasithubutu la sivyo watakiona cha moto na serikali ya SSH kimyaa!

Na siku hiyo ikafika. Polisi walivyotanda utadhani wanaenda vitani. Kila aina ya silaha ilikuwepo kupambana na maadui waliopanga kuhudhuria kesi. Wakaona hata hiyo hiitoshi wakakumbuka mbinu ya makaburu ya kuwatumia mbwa!

Kweli tumefika huko! Na hata miezi sita haijafika tayari hatuna tofauti na makaburu wa Afrika Kusini miaka karibu sitini enzi za Nelson Mandela na wenzake walipofunguliwa kesi ya ugaidi na serikali ya kibaguzi ya wakati huo.

Je ikitokea wananchi wakachoka na uonevu, wakaamua potelea mbali, kama ni keba keba kama inavyotokea sehemu mbali mbali duniani, je kutakalika? Tumshukuru Mungu aliyetujaalia Watanzania uvumilivu lakini mpaka lini?
We don't fight with "Trained Fools" yaani ni mwendo tu wa kuwasaidia "majukumu" ya nyumba zao! Ukifika unapikiwa, unakula ukimaliza unakula na mpishi! Wakati huo yeye kaenda Lindo Bank ya NMB au CRDB huko anapigwa baridi
 
Una hakika mimi sielewi? Jaribu tena kusoma OP na conclusion aliyofikia utajua maana ya nilichoandika. Video niliyoweka ni mwananchi naye aliyechoka uonevu wa polisi akaamua potelea mbali. Liwalo na liwe. Yalimtokea umeyaona.
Kama unaelewa maana ya hilo neno, basi unayoandika hapa unajichanganya mwenyewe, sijui kwa manufaa gani.
 
Tabia ya polisi wa Tanzania kuwatisha, kuwapiga na kuwaumiza wananchi wanaotumia haki yao ya kuhoji utendaji wa serikali inazidi kuota mizizi na kuibua maswali kuhusu wajibu wa polisi kwa raia wanaotuhumiwa kuvunja sheria.

Kwa hali isiyoeleweka Polisi wa Tanzania wameamua kutoheshimu uhuru wa mikusanyiko na uhuru wa mawazo kama ilivyooanishwa kwenye Katiba kama vile ni uvunjaji wa sheria na hivyo kujipa mamlaka ya kuwaadhibu watuhumiwa kwa vipigo.

Kauli za maafande wa polisi katika miaka ya karibuni imezidi kuwa ya kibabe na ya kiuonevu kiasi cha kutishia amani ya nchi kama wananchi wataamua kujibu mapigo kama invyotokea katika mataifa mengine ndani na nje ya Afrika.

Imekuwa kawaida polisi, ambao jukumu lao la msingi ni kuwalinda raia na mali zao, wamesikika wakitoa kauli za vitisho utadhani muda wote wako vitani na raia ambao kimsingi ndio waajiri wao kupitia serikali yao waliyoichagua wao.

Baadhi ya kauli hizo ni kama ifuatavyo...
  • Wanaopanga kuandamana kesho watakiona cha moto
  • Wakiandamana watapigwa kama mbwa koko.
  • Watu watakaoandamana kwa amani watapigwa hadi wachakae
Kwa kauli kama hizi, wananchi waelewe nini? Kwa nini vyombo ambavyo vinatakiwa kulaani kauli kama hizi viko kimya? Hii jeuri ya polisi mbona imeachwa kukomaa hadi polisi kuonekana wako juu ya sheria? Kwa nini serikali haikemei kauli kama hizi? Je ni serikali inawatuma na kuwaruhusu polisi kuwaumiza wananchi?

Katika ombi langu hapo juu, nimeomba mwenye ushahidi wowote wa raia wa nchi hii kujibu mapigo kama inavyotokea katika nchi nyingine auweke hapa. Binafsi sina, ila naona kila mara polisi wakitoa vipigo kwa raia wasio hata na fimbo.

Hawaishii kupiga tu watu wazima wanaume kwa wanawake, wamethubutu kuwapiga hadi vitoto wa shule na hakuna tamko lolote limewahi kutolewa na vyombo vyenye jukumu la kuhakikisha raia wanatendewa haki.

Watu wanapigwa kabla ya kukamatwa, wanapigwa baada ya kukamatwa, wanapigwa wakiwa mikononi mwa polisi tayari iwe ndani ya gari au kwenye vituo vya polisi kama vile jukumu la polisi kwa sasa ni kupiga, kuumiza na hata kuua.

Watu waliokamatwa wamefikishwa mahakamani wakiwa na majeraha makubwa hadi kutembea wanashindwa lakini sijawahi kuisikia hata Mahakama ikitaka kujua kilichotokea au hata kuhoji kwa nini mtuhumiwa anachechemea.

Wananchi wamekamatwa majumbani wakiwa na afya zao lakini baada ya muda mfupi kwenye kituo cha polisi, wanapelekwa mahakamani wamebebwa hawawezi kutembea. Je ni kitu gani kinawapata hawa raia kwenye vituo vya polisi?

Juzi nimemsikia IGP mwenyewe kwa kauli yake akiwatishia wananchi waliopanga kufika mahakamani kusikiliza kesi ya Mbowe aliyeshtakiwa kwa kosa la ugaidi kwamba wasithubutu la sivyo watakiona cha moto na serikali ya SSH kimyaa!

Na siku hiyo ikafika. Polisi walivyotanda utadhani wanaenda vitani. Kila aina ya silaha ilikuwepo kupambana na maadui waliopanga kuhudhuria kesi. Wakaona hata hiyo hiitoshi wakakumbuka mbinu ya makaburu ya kuwatumia mbwa!

Kweli tumefika huko! Na hata miezi sita haijafika tayari hatuna tofauti na makaburu wa Afrika Kusini miaka karibu sitini enzi za Nelson Mandela na wenzake walipofunguliwa kesi ya ugaidi na serikali ya kibaguzi ya wakati huo.

Je ikitokea wananchi wakachoka na uonevu, wakaamua potelea mbali, kama ni keba keba kama inavyotokea sehemu mbali mbali duniani, je kutakalika? Tumshukuru Mungu aliyetujaalia Watanzania uvumilivu lakini mpaka lini?
Jeuri wanaipata kutokana na nafasi zao walizo nazo ,na hii inachagizwa na katiba mbovu iliyopo!

Kwaharaka kabisa hatusahau kwamba wanateswa na kiburi Cha uzima!
 
Sote tunajua ukatili waliofanyiwa raia wa nchi hii na Polisi wakati wa awamu ya mwendakuzimu aliyesalimu amri kwa corona mwezi wa tatu. Hebu tazameni simulizi hii...

Part I
View attachment 1888930


Part 2
View attachment 1888928

Part 3
View attachment 1888936

Hawa Waliomtendea hivi Elisha Mwanjala waliingia vipi Jeshi la Polisi?
Hiyo ilikuwa awamu ya tano na sasa tunashuhudia ya awamu ya sita.
Watanzania majoka ya kibisa kabisa. Sasa tunangoja nini? Polisi wanajivunia umoja na silaha zetu. Si Wana ndugu na watoto hawa? Tit for tat
 
Yatamshinda kwa sababu amekataa kupelekeshwa na tantalila za Chadema?

Polisi wamekuwa hivyo miaka mingi toka enzi za Mkapa, Kikwete na Magufuli.

Na si Tanzania peke yake. Kwani kilio cha "defund the police" huko Marekani unafikiri ni kwa sababu gani?

Au kule Nigeria na "end SARS"?

Kama ni kudeal na police incompetence na police brutality msitake kuchanganya na mambo yenu ya siasa.

Police ni taaluma na ishughulikieni kitaaluma. Basi.
Taaluma ya kuonea badala ya ulinzi WA mali na raia? Ngojea kidogo weka haya akiba polisi watapigwa na raia waliochoka
 
Tabia ya polisi wa Tanzania kuwatisha, kuwapiga na kuwaumiza wananchi wanaotumia haki yao ya kuhoji utendaji wa serikali inazidi kuota mizizi na kuibua maswali kuhusu wajibu wa polisi kwa raia wanaotuhumiwa kuvunja sheria.

Kwa hali isiyoeleweka Polisi wa Tanzania wameamua kutoheshimu uhuru wa mikusanyiko na uhuru wa mawazo kama ilivyooanishwa kwenye Katiba kama vile ni uvunjaji wa sheria na hivyo kujipa mamlaka ya kuwaadhibu watuhumiwa kwa vipigo.

Kauli za maafande wa polisi katika miaka ya karibuni imezidi kuwa ya kibabe na ya kiuonevu kiasi cha kutishia amani ya nchi kama wananchi wataamua kujibu mapigo kama invyotokea katika mataifa mengine ndani na nje ya Afrika.

Imekuwa kawaida polisi, ambao jukumu lao la msingi ni kuwalinda raia na mali zao, wamesikika wakitoa kauli za vitisho utadhani muda wote wako vitani na raia ambao kimsingi ndio waajiri wao kupitia serikali yao waliyoichagua wao.

Baadhi ya kauli hizo ni kama ifuatavyo...
  • Wanaopanga kuandamana kesho watakiona cha moto
  • Wakiandamana watapigwa kama mbwa koko.
  • Watu watakaoandamana kwa amani watapigwa hadi wachakae
Kwa kauli kama hizi, wananchi waelewe nini? Kwa nini vyombo ambavyo vinatakiwa kulaani kauli kama hizi viko kimya? Hii jeuri ya polisi mbona imeachwa kukomaa hadi polisi kuonekana wako juu ya sheria? Kwa nini serikali haikemei kauli kama hizi? Je ni serikali inawatuma na kuwaruhusu polisi kuwaumiza wananchi?

Katika ombi langu hapo juu, nimeomba mwenye ushahidi wowote wa raia wa nchi hii kujibu mapigo kama inavyotokea katika nchi nyingine auweke hapa. Binafsi sina, ila naona kila mara polisi wakitoa vipigo kwa raia wasio hata na fimbo.

Hawaishii kupiga tu watu wazima wanaume kwa wanawake, wamethubutu kuwapiga hadi vitoto wa shule na hakuna tamko lolote limewahi kutolewa na vyombo vyenye jukumu la kuhakikisha raia wanatendewa haki.

Watu wanapigwa kabla ya kukamatwa, wanapigwa baada ya kukamatwa, wanapigwa wakiwa mikononi mwa polisi tayari iwe ndani ya gari au kwenye vituo vya polisi kama vile jukumu la polisi kwa sasa ni kupiga, kuumiza na hata kuua.

Watu waliokamatwa wamefikishwa mahakamani wakiwa na majeraha makubwa hadi kutembea wanashindwa lakini sijawahi kuisikia hata Mahakama ikitaka kujua kilichotokea au hata kuhoji kwa nini mtuhumiwa anachechemea.

Wananchi wamekamatwa majumbani wakiwa na afya zao lakini baada ya muda mfupi kwenye kituo cha polisi, wanapelekwa mahakamani wamebebwa hawawezi kutembea. Je ni kitu gani kinawapata hawa raia kwenye vituo vya polisi?

Juzi nimemsikia IGP mwenyewe kwa kauli yake akiwatishia wananchi waliopanga kufika mahakamani kusikiliza kesi ya Mbowe aliyeshtakiwa kwa kosa la ugaidi kwamba wasithubutu la sivyo watakiona cha moto na serikali ya SSH kimyaa!

Na siku hiyo ikafika. Polisi walivyotanda utadhani wanaenda vitani. Kila aina ya silaha ilikuwepo kupambana na maadui waliopanga kuhudhuria kesi. Wakaona hata hiyo hiitoshi wakakumbuka mbinu ya makaburu ya kuwatumia mbwa!

Kweli tumefika huko! Na hata miezi sita haijafika tayari hatuna tofauti na makaburu wa Afrika Kusini miaka karibu sitini enzi za Nelson Mandela na wenzake walipofunguliwa kesi ya ugaidi na serikali ya kibaguzi ya wakati huo.

Je ikitokea wananchi wakachoka na uonevu, wakaamua potelea mbali, kama ni keba keba kama inavyotokea sehemu mbali mbali duniani, je kutakalika? Tumshukuru Mungu aliyetujaalia Watanzania uvumilivu lakini mpaka lini?
Mkuu shukrani mingi sana
 
Ngoja waendelee kutujaza sumu raia, siku tutalipuka zaidi ya Tsar Bomba.. na hawata amini.
 
Back
Top Bottom