Polisi: Madereva wa Serikali wana kiburi sababu ya Namba za Magari yao

Hili jambo la madereva wa serikali lina ishushia heshima serikali yenyewe na viongozi wanaondeshwa. Huwezi kuwa kiongozi wa serikali alafu unachekelea dereva aki-overtake kwenye mlima au kona kali. Akili za hao viongozi zipimwe.
 
Kidogo Jeshi la wananchi wao hujitahidi kufuata sheria za usalama barabarani ingawa nao wana ushamba fulani barabarani na kaubabe ka kijinga, mimi Dereva wao mmoja niliwahi kumfundisha adabu maeneo ya Masika Morogoro akiwa na vile vibasi vyao viashok vifupi, ili ajifunze kuwa naye ni raia kama walivyo wengine katika matumizi ya barabara., nisisimulie ilivyokuwa naweza kudisclose ID yangu.

Ukija kwa hawa PT mh kufuata sheria za usalama barabarani kwao ndo kama wenzao Tiss ambao nao wanajikutaga miungu watu kwa barabara, bahati nzuri chuma yangu ni Prado iliyoapgrediwa to LX imekula ngao mbele ngao nyuma, huwa sikwepeshi ukija njoo tu!

Ambao hujitahidi kidogo kufuata sheria ni magereza, fire na uhamiaji. Hawa huwa wana hofu kidogo ya kuchukuliwa hatua hivyo hufuata sheria.

ST( K,L, na M), hawa SU, SM ndo wa hovyo sana huko barabarani hasa hawa ST! Ila kwangu wanaisomaga namba! Afu tunamalizana huko huko juu kwa ju, ukileta utabe ndo tunafikishana kwa maboss zako ambao wananywea na kukuachia msala uusolve mwenyewe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…