Tetesi: Polisi Mara: Vincent Nyerere anakuja kuratibu vurugu za UKUTA, tutamshughulikia

Tetesi: Polisi Mara: Vincent Nyerere anakuja kuratibu vurugu za UKUTA, tutamshughulikia

SIMU YA TOCHI

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2014
Posts
1,385
Reaction score
894
Ikiwa ni muendelezo wa taharuki na hofu ya serikali, jeshi la polisi mkoani Mara limeingia kwenye jaribu jingine la kutumika na serikali kuwashughulikia wanachama na viongozi wowote ambao wataonekana au watahisiwa wanaratibu zoezi la UKUTA kuelekea Sept1.

Hali hii imejitokeza baada ya mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa Mara Mh Vincent Nyerere akitokea Butiama kwenye mazishi kuelekea nyumbani kwake Musoma Mjini, vijana wa bodaboda walipomuona walilazimika kuunga msafara na kumsindikiza jambo hili lilimchefua moja wa afisa wa jeshi la polisi na ikapelekea kuagiza kikosi maalumu ili walishughulikie suala hilo, kutokana na Mh Nyerere kupata taarifa hii mapema kutoka kwenye chanzo cha jeshi la polisi moja kwa moja ilimlazimu asiingie katikati ya mji wa Musoma na kuamua kurudi kata ya bweri Musoma mjini anapoishi ili kuwaokoa vijana ambao walikuwa wanatakiwa kuja kushughulikiwa na jeshi la polisi.

Ikawa ni kauli mbiu kila muda atapotoka nyumbani kwenda mahala popote ililazimika polisi kufuatilia nyendo zake ili wajue ametoka kwake kwa sababu gani na huko anakoenda anaenda kufanya nini

Ikumbukwe katika kipindi cha uchaguzi ni hawahawa baadhi ya wakubwa wa polisi walikuwa wakiwalazimisha polisi wadogo kupiga mabomu wanachadema waliokuwa wakitembea kumsindikiza mgombea baada ya mikutano, ni hawahawa wakubwa wa polisi walishiriki na kutumia baadhi ya watu kutega vilipuzi ndani ya gari ya mgombea ili kummaliza, ni hawa hawa wakubwa wa polisi walikuwa wanawaachia vijana wa CCM waliokuwa wanawashughulikia kwa mapanga wafuasi wa CHADEMA, ni hawahawa wakubwa wa jeshi la polisi waliahidiwa kupewa milioni 40 endapo wataisaidia CCM kushinda jimbo la Musoma Mjini.

Yapo mengi sana ya kusema ila kwa leo tuishie hapa ngoja tuone movie itavyoendelea.
 
Kweli UKUTA ni mwisho wa matatizo ndiyo maana wananchi wanaunga mkono
 
Polisi waangalie sana, walinde Amani na pale ambapo hakuna fujo hebu wakae pembeni wasizianzishe. Fujo zaweza kufikia kiwango ambacho wanaweza kushindwa kudhibiti mfano watu wakianza kuchoma mioto sehemu mbalimbali
 
Polisi waangalie sana, walinde Amani na pale ambapo hakuna fujo hebu wakae pembeni wasizianzishe. Fujo zaweza kufikia kiwango ambacho wanaweza kushindwa kudhibiti mfano watu wakianza kuchoma mioto sehemu mbalimbali

Mara kadhaa polisi na serikali ni watu ambao wamekua wakianzisha vurugu napale wanaposhindwa kuzikabili wanawarushia upinzani lawama,rejea mauaji ya arusha
 
Rais anapokuwa mvunja sheria na katiba unakuwa mtihani mkubwa sana.
 
Sio kupata presha tuuh!atajikuta miaka 10 imeisha hakuna LA maana alilofanya LA maendeleo zaidi ya kudili na chadema..!Tanzania ya viwanda haiwezi kujengwa, nchi kuwa katika hali hii.

Tanzania ya viwanda imekua ni tanzania ya kumshughulikia Lissu
 
Kumbe wewe humjui huyo, wanaomjua walishajitoa barabarani wameamua kufanya kazi na kujenga uchumi wa familia zao watakao lazimisha watakiona hiyo tarehe moja tusije sema hatukujua kama mambo yangekuwa hivi.
 
Ikawa ni kauli mbiu kila muda atapotoka nyumbani kwenda mahala popote ililazimika polisi kufuatilia nyendo zake ili wajue ametoka kwake kwa sababu gani na huko anakoenda anaenda kufanya nini
Hongera sana Polisi wa Mara
Viongozi wote wa serikali kazi yao kubwa ni kuleta maendeleo katika maeneo yao kwa ajili ya wananchi wa maeneo husika.Hivyo viongozi wote wa serikali kuanzia wa mikoa,wilaya,tarafa,kata,mitaa na vijiji wahakikishe wanawakamata na kuwashughulikia kikamilifu ikiwemo hata kuwafukuza maeneo husika watu wote ambao si wakazi wa maeneo husika ambao kazi yao ni kuleta maandamano maeneo husika badala ya maendeleo.

Mgeni yeyote ambaye si mkazi wa eneo husika liwe la mkoa,wilaya,tarafa,kata,mtaa au kijiji atakayekanyaga kwenye eneo ambalo si mkazi na kuleta maandamano badala ya maendeleo viongozi husika wamshughulikie mgeni huyo kikamilifu bila huruma sababu anakuja kukwamisha juhudi za maendeleo maeneo yasiyo yake.Kama anakuja kuleta maendeleo kama miradi ya maji,afya nk mkaribisheni kwa mikono miwili baada ya kuhakiki.Lakini mtu asiye mkazi hata awe anatoka mtaa wa pili kama si mkazi wa mtaa au kijiji husika hata kama ni eneo moja kama analeta maandamano kwenye mtaa au kijiji kisichokuwa chake viongozi wa vijiji na mitaa husika mshughulikieni bila huruma iwayo yoyote.

Wakuu wa mikoa watoe maagizo kwa viongozi wote wa wilaya,tarafa,mikoa,vijiji na mitaa watoe taarifa ya wageni wote wanaoleta maandamano kwenye maeneo yasiyo yao badala ya kupeleka maendeleo.

Huu sio wakati wa kuwachekea watu ambao si wakazi wa mitaa,vijiji,kata,tarafa,wilaya au mikoa husika wanaotoka maeneo ya kwao kwenda kuleta vurugu,maandamano badala ya maendeleo.

Huu ni wakati pia wa wakazi wa maeneo husika kuwashughulikia kikamilifu wageni wote watakaokanyaga maeneo yasiyo makazi yao kuendesha maandamano badala ya kuendesha miradi ya maendeleo ya kuwakwamua wananchi na umaskini.
 
Haya maneno uyaongee tar1 mwezi wa 9
Si bado wiki mbili tu tuone huyo nguri asiejua mamlaka aliopewa amiri Jeshi ni yapi,mliambiwa punguzeni mamlaka ya Rais ni makubwa nyie nyie mkajifanya mwachieni tu sasa kaja mtu anaweza kuyatumia mamlaka vizuri kama mlivyoainisha kwenye katiba ya mwaka 1977, tunaojua haya tunamsikiliza Rais, akisema leo msitoke nje atutoki maana ni sehemu ya mamlaka yake lakini kwakuwa wewe uyajui haya njoo tarehe 1 ukutane nae barabarani.
 
Ikiwa ni muendelezo wa taharuki na hofu ya serikali,jeshi la polisi mkoani mara limeingia kwenye jaribu jingine la kutumika na serikali kuwashughulikia wanachama na viongozi wowote ambao wataonekana au watahisia wanaratibu zoezi la UKUTA kuelekea sep1.
Hali hii imejitokeza baada ya mwenyekiti wa chadema mkoa wa mara mh Vincent Nyerere akitokea butiama kwenye mazishi kuelekea nyumbani kwake musoma mjini,vijana wa boda boda walipomuona walilazimika kuunga msafara na kumsindikiza jambo hili lilimchefua moja wa afsa wa jeshi la polisi na ikapelekea kuagiza kikosi maalumu ili walishughulikie suala hilo,kutokana na Mh Nyerere kupata taarifa hii mapema kutoka kwenye chanzo cha jeshi la polisi moja kwa moja ilimlazimu asiingie katikati ya mji wa musoma na kuamua kurudi kata ya bweri musoma mjini anapoishi ili kuwaokoa vijana ambao walikuwa wanatakiwa kuja kushughulikiwa na jeshi la polisi.Ikawa ni kauli mbiu kila muda atapotoka nyumbani kwenda mahala popote ililazimika polisi kufuatilia nyendo zake ili wajue ametoka kwake kwa sabau gani na huko anakoenda anaendakufanya nini

Ikumbukwe katika kipindi cha uchaguzi ni hawahawa baadhi ya wakubwa wa polisi walikuwa wakiwalazimisha polisi wadogo kupiga mabomu wanachadema waliokuwa wakitembea kumsindikiza mgombea baada ya mikutano,ni hawahawa wakubwa wa polisi walishiriki na kutumia baadhi ya watu kutega vilipuzi ndani ya gari ya mgombea ili kummaliza,ni hawa hawa wakubwa wa polisi walikuwa wanawaachia vijana wa ccm waliokuwa wanawashughulikia kwa mapanga wafuasi wa chadema,ni hawahawa wakubwa wa jeshi la polisi waliahidiwa kupewa milioni 40 endapo wataisaidia ccm kushinda jimbo la musoma mjini.
Yapo mengi sana ya kusema ila kwa leo tuishie hapa ngoja tuone movie itavyoendelea.
Mkuu kwa polisi kuendelea kujionyesha uhalisia wao hayo ndio mafanikio ya UKUTA
 
Si bado wiki mbili tu tuone huyo nguri asiejua mamlaka aliopewa amiri Jeshi ni yapi,mliambiwa punguzeni mamlaka ya Rais ni makubwa nyie nyie mkajifanya mwachieni tu sasa kaja mtu anaweza kuyatumia mamlaka vizuri kama mlivyoainisha kwenye katiba ya mwaka 1977, tunaojua haya tunamsikiliza Rais, akisema leo msitoke nje atutoki maana ni sehemu ya mamlaka yake lakini kwakuwa wewe uyajui haya njoo tarehe 1 ukutane nae barabarani.

Kweli ccm imetutengenezea mazuzu,ni katiba ipi inampa raisi mamlaka kuzuia vyama vya upinzani kufanya mikutano,ni katiba ipi inampa mamlaka kuwashughulikia wote ambao wanaonekana kutomuunga mkono pale anapokosea?
Na huko unapoelekea raisi anaweza kuingia nyumbani kwako na kukufanyia ndivyo sivyo na ukamuunga mkono na kumpigia makofi jitathmini gamba la lumumba
 
Kweli ccm imetutengenezea mazuzu,ni katiba ipi inampa raisi mamlaka kuzuia vyama vya upinzani kufanya mikutano,ni katiba ipi inampa mamlaka kuwashughulikia wote ambao wanaonekana kutomuunga mkono pale anapokosea?
Na huko unapoelekea raisi anaweza kuingia nyumbani kwako na kukufanyia ndivyo sivyo na ukamuunga mkono na kumpigia makofi jitathmini gamba la lumumba
Usiongee kama ujui mamlaka ya Rais, unanipotezea muda wangu,eti tena unasema CCM imetengeneza mazuzu,kwahiyo na wewe zuzu maana umezaliwa ndani ya ccm
 
Back
Top Bottom