KERO Polisi Mtwara acheni tamaa mnatukwamisha, sisi pia tupo kazini na tuna familia

KERO Polisi Mtwara acheni tamaa mnatukwamisha, sisi pia tupo kazini na tuna familia

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Kaka kama hujawahi drive kwa safari za kila siku au ndefu , hawa jamaa japo si wote wana njaa isiyo elezeka. Arusha walikuwepo wa mianzini, wale huwa wanafanya kama ni biashara kabisa, tena wana confidence kabisa as if ni halali
Mkuu,njaa,kiu,usongo ama urafi wa polisi ni kitu halisi sio ndoto.

Mtu kusema alikamatwa akiwa hana kosa,huu ni unafiki wa wazi,huna kosa unatoa rushwa ili wasikuue ama??

Ukitaka kujua akili za wabongo ni za hovyo kuliko traffic,mtu analalamika kwanini polisi anajificha kichakani kupiga tochi!!!!huu ni utoto kiwango cha juu.
Yaani nia yake akimbie mwendo anaoutaka popote tu.
 
Mkuu,njaa,kiu,usongo ama urafi wa polisi ni kitu halisi sio ndoto.

Mtu kusema alikamatwa akiwa hana kosa,huu ni unafiki wa wazi,huna kosa unatoa rushwa ili wasikuue ama??

Ukitaka kujua akili za wabongo ni za hovyo kuliko traffic,mtu analalamika kwanini polisi anajificha kichakani kupiga tochi!!!!huu ni utoto kiwango cha juu.
Yaani nia yake akimbie mwendo anaoutaka popote tu.
Probably sijui mazingira yake yakoje, ila mimi limenikuta arusha, moshi, tanga, singida, even pwani. Mara ya kwanza nililalamika baadae nikaambiwa usipowatoa watakubana mahali. By then nilikuwa natembelea chuma kipya. Asipokuluta na kosa, atakwambia hela ya chai. Imezoeleka japokuwa ni kinyume na sheria
 
Mkuu huna kosa unatoa pesa ya nini???
Si ukubali kwenda kituoni kisha mahakamani ukatetee haki yako??,kama unahisi huna muda basi malalamiko yako yote yanakosa maana hapa maana unatoa kwa hiyari yako.

Polisi wanatumia uzembe na mapuuza yenu kujinufaisha.
Mtu akifikiria danadana atazopigwa polisi na makosa atayobambikiwa akigoma kutowa hiyo elfu tano, anaona ni heri atowe huku anasononeka.
 
Inasikitisha sana siku hizi polisi kama nchi ni ya kwao kabisa.! As if Serikali imeshawapa ruhusa ya wanachokifanya. Mikoa mingine sijui, hapa Mtwara Kilimanjaro kuna hawa polisi wanatoza tu hela kwa wenye magari hata kama huna kosa sijui tuwaite watoza ushuru au polisi maana mauza uza uza tu.

Kuna hawa wa Mitengo yaani wanataka hela kwa lazima sh 5,000 kila bajaji kweli!

Sasa bajaj kutoka Mkanaled mpaka Mikindani bajaj inaingia abiria wanne ambao ni elfu 4 halafu utoe elfu tano bila kosa lolote huu ni uonevu wa hali ya juu na huku ni kujinufaisha wao tu.

Kuna hawa wengine hapa Mangamba njiani kama unaenda ziwani, hawa askari hapa imekuwa kama upatu kila gari la mchanga wanachukua elfu 5 na hii ni kila siku. Hata kama huna kosa lolote na wanakuambia kabisa tukuandikie kosa elfu 30 au utoe elfu 5.

Tumerudi zama za kikoloni mno

Tunaomba msaada Mtwara askari wanatajirika kupitia madereva

Askari wa Mangamba, Mitengo, na Kilimanjaro wanatunyonya mno

Siku yake nitakuja na picha na videos za hawa askari wetu.
Hakuna jambo jipya hapa ambalo umeongea!
Hii hali ipo katika sehemu zote hapa Tanzania, wala siyo kitu kigeni.
Rushwa imekuwa sehemu mojawapo ya Utoaji huduma hapa Tanzania, no Utamaduni wa kiutendaji ktk karibia Ofisi zote za umma hapa Tanzania.
 
Njia ya kuondoa Huu ni polisi avae camera muda wote ili chochote anachofanya kionekane Kwa umma na kuwashughulikia kirahisi.tuwaige wa marekani na wanywarwanda
Hilo haliwezekani kwasababu wao pia wamepewa target na mabosi wao! Na mabosi wao pia wamepewa target na mabosi wao,ni chain inaenda hivyo hivyo mpaka juu kabisa! Sijui umenielewa?
 
Mtu akifikiria danadana atazopigwa polisi na makosa atayobambikiwa akigoma kutowa hiyo elfu tano, anaona ni heri atowe huku anasononeka.
kila mwananchi akiwa na mtizamo huu,basi hakuna maana ya maisha.

kila mwananchi akiwa serious na haki zake uonezi utapungua,yaani unatoa mwenyewe elfu 5 kwa uoga wako,halafu unaanza kulalamika traffic wana njaa!!!!
 
Inasikitisha sana siku hizi polisi kama nchi ni ya kwao kabisa.!

Tunaomba msaada Mtwara askari wanatajirika kupitia madereva

Askari wa Mangamba, Mitengo, na Kilimanjaro wanatunyonya mno

Siku yake nitakuja na picha na videos za hawa askari wetu.
Kwanza hakuna askari polisi tajiri, labda wanawanyonya nini.... madushe?
 
Labda gari ndogo binafsi ndo hazinaga makosa ila hizi za biashara traffic kikuta kosa ana zaidi ya asilimia 80 hadi 90.
Ndio maana mnatoa hizo buku 5 maana mtu anajijua ana kosa.

Mfano hizi daladala za mijini, yaani hata abiria ambae hana ABC za magari na sheria za barabarani anajua hii chuma ina kosa, sembuse trafki mpenda rushwa.
 
Back
Top Bottom