KERO Polisi Mtwara acheni tamaa mnatukwamisha, sisi pia tupo kazini na tuna familia

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Kaka kama hujawahi drive kwa safari za kila siku au ndefu , hawa jamaa japo si wote wana njaa isiyo elezeka. Arusha walikuwepo wa mianzini, wale huwa wanafanya kama ni biashara kabisa, tena wana confidence kabisa as if ni halali
Mkuu,njaa,kiu,usongo ama urafi wa polisi ni kitu halisi sio ndoto.

Mtu kusema alikamatwa akiwa hana kosa,huu ni unafiki wa wazi,huna kosa unatoa rushwa ili wasikuue ama??

Ukitaka kujua akili za wabongo ni za hovyo kuliko traffic,mtu analalamika kwanini polisi anajificha kichakani kupiga tochi!!!!huu ni utoto kiwango cha juu.
Yaani nia yake akimbie mwendo anaoutaka popote tu.
 
Probably sijui mazingira yake yakoje, ila mimi limenikuta arusha, moshi, tanga, singida, even pwani. Mara ya kwanza nililalamika baadae nikaambiwa usipowatoa watakubana mahali. By then nilikuwa natembelea chuma kipya. Asipokuluta na kosa, atakwambia hela ya chai. Imezoeleka japokuwa ni kinyume na sheria
 
Mtu akifikiria danadana atazopigwa polisi na makosa atayobambikiwa akigoma kutowa hiyo elfu tano, anaona ni heri atowe huku anasononeka.
 
Hakuna jambo jipya hapa ambalo umeongea!
Hii hali ipo katika sehemu zote hapa Tanzania, wala siyo kitu kigeni.
Rushwa imekuwa sehemu mojawapo ya Utoaji huduma hapa Tanzania, no Utamaduni wa kiutendaji ktk karibia Ofisi zote za umma hapa Tanzania.
 
Njia ya kuondoa Huu ni polisi avae camera muda wote ili chochote anachofanya kionekane Kwa umma na kuwashughulikia kirahisi.tuwaige wa marekani na wanywarwanda
Hilo haliwezekani kwasababu wao pia wamepewa target na mabosi wao! Na mabosi wao pia wamepewa target na mabosi wao,ni chain inaenda hivyo hivyo mpaka juu kabisa! Sijui umenielewa?
 
Mtu akifikiria danadana atazopigwa polisi na makosa atayobambikiwa akigoma kutowa hiyo elfu tano, anaona ni heri atowe huku anasononeka.
kila mwananchi akiwa na mtizamo huu,basi hakuna maana ya maisha.

kila mwananchi akiwa serious na haki zake uonezi utapungua,yaani unatoa mwenyewe elfu 5 kwa uoga wako,halafu unaanza kulalamika traffic wana njaa!!!!
 
Inasikitisha sana siku hizi polisi kama nchi ni ya kwao kabisa.!

Tunaomba msaada Mtwara askari wanatajirika kupitia madereva

Askari wa Mangamba, Mitengo, na Kilimanjaro wanatunyonya mno

Siku yake nitakuja na picha na videos za hawa askari wetu.
Kwanza hakuna askari polisi tajiri, labda wanawanyonya nini.... madushe?
 
Labda gari ndogo binafsi ndo hazinaga makosa ila hizi za biashara traffic kikuta kosa ana zaidi ya asilimia 80 hadi 90.
Ndio maana mnatoa hizo buku 5 maana mtu anajijua ana kosa.

Mfano hizi daladala za mijini, yaani hata abiria ambae hana ABC za magari na sheria za barabarani anajua hii chuma ina kosa, sembuse trafki mpenda rushwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…