kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 13,778
- 14,214
Ukweli askari polisi ni kero kubwa kwa wananchi. Ni kero kubwa kwa wakulima, wafugaji, wasafirishaji, wafanyabiashara na hata madereva barabarani. Kila jambo na kila kitendo wanachokifanya ni kwaajili ya kupata hela kwa njia ya rushwa au unyang'anyi kunakosababisha Wananchi wanakata tamaa ndani ya nchi yao wenyewe. Hizi mashine za kutozea watu faini wanazotembea nazo ndio silaha kubwa wanayoitumia kusumbua watu kuwabambikiza makosa watu kwa lengo la kuwafanya watu wavutike kulipa hela punguvu kuliko sh. 30,000 zinazotozwa kwakutumia vifaa hivyo vya mkononi, ni kero.
Naomba kwa kuanzia polisi wanyang'anywe hizi mashine za mkononi ambazo wanazitumia vibaya. Wanaigombanisha serikali na wananchi wake. Barabarani hawaachi pesa, wanapokea kuanzia sh. 2000 ili kusamehe tsh 30,000 za kubambikia au kosa la kweli.
Kwa wakulima na wafugaji, polisi wanashirikiliana na wakulima/wafugaji kujipatia fedha kwa makosa ya kubambikia. Huku vijijini kero ni kubwa sana kiasi cha watu kukata tamaa kwa vitendo vya polisi kwa "michongo" ya polisi kwa ushirikiano na baadhi ya wanavijiji.
Wasafirishaji wa mizigo na abiria wako hoi, vijana wanaosafirisha mizigo kwa kutumia pikipiki za magurudumu 3 wana shida sana barabarani, wanawindwa kama swala na jeshi la polisi.
Ukweli jeshi hili livunjwe ili lipangwe upya.
Naomba kwa kuanzia polisi wanyang'anywe hizi mashine za mkononi ambazo wanazitumia vibaya. Wanaigombanisha serikali na wananchi wake. Barabarani hawaachi pesa, wanapokea kuanzia sh. 2000 ili kusamehe tsh 30,000 za kubambikia au kosa la kweli.
Kwa wakulima na wafugaji, polisi wanashirikiliana na wakulima/wafugaji kujipatia fedha kwa makosa ya kubambikia. Huku vijijini kero ni kubwa sana kiasi cha watu kukata tamaa kwa vitendo vya polisi kwa "michongo" ya polisi kwa ushirikiano na baadhi ya wanavijiji.
Wasafirishaji wa mizigo na abiria wako hoi, vijana wanaosafirisha mizigo kwa kutumia pikipiki za magurudumu 3 wana shida sana barabarani, wanawindwa kama swala na jeshi la polisi.
Ukweli jeshi hili livunjwe ili lipangwe upya.