LGE2024 Polisi Rukwa: Vijana CCM hawakuwa na nia ya kuchoma nyumba ya Mbunge

LGE2024 Polisi Rukwa: Vijana CCM hawakuwa na nia ya kuchoma nyumba ya Mbunge

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Wakuu,

Maake hapo kwanza ncheke!

===

1732725251562.png

Jeshi la Polisi mkoani Rukwa limetoa ufafanuzi wa taarifa inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu vijana sita wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kukamatwa nyumbani kwa Mbunge wa Jimbo la Nkasi Kaskazini, Aida Kenan wakiwa na petroli lita 20 kwa lengo la kuiangamiza familia ya mbunge huyo.

Kupata taarifa na matukio ya kimkoa kuhusu Uchaguzi Serikali za Mitaa ingia hapa: LGE2024 - Special Thread: Orodha ya Mijadala ya Mikoa yote Tanzania Bara inayoshiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Katika taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi, imesema uchunguzi wa awali unaonesha kuwa vijana hao waliokamatwa na wafuasi wa CHADEMA, walifika nyumbani kwa Mkuu wa Wilaya ya Nkasi, Peter Lijualikali majira ya saa moja jioni wakiwa na pikipiki mbili na dumu lenye mafuta ya petroli lita 20, kwa lengo la kuchukua pikipiki zingine zilizokuwa hapo na kuziwekea mafuta.

“Kwa kuwa nyumbani kwa Mkuu wa Wilaya na nyumbani kwa Mbunge ni karibu sana nyumba zao zikitenganishwa na barabara, ndipo vijana hao walipokamatwa na kutuhumiwa kwamba walikuwa na lengo la kuchoma moto nyumba ya Mbunge Aida,” imeeleza taarifa ya Polisi.

Swahili Times

Pia soma:
- LGE2024 - Nkasi: Wanaodaiwa kutumwa na DC kulipua nyumba ya Mbunge Aida Kenani usiku huu wakamatwa, wametumia pikipiki za Samia
 
Tunapofunga vituo vya kupiga kura kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Taifa limeendelea kushuhudia tena ubaradhuli wa wazi na wa aibu toka kwa mamlaka zote za Serikali kushirikiana kuipatia CCM na wagombea wake ushindi wa aibu hata kwa gharama za maisha ya Watanzania.

Tunalaani mauaji na kujeruhiwa kwa wagombea, viongozi na wanachama wetu mbalimbali wakiwemo:

1) Steven Chalamila wa Jimbo la Tunduma aliyevamiwa na kukatwakatwa mapanga kikatili hadi umauti kumkuta.
2) Modestus Timbisimilwa, Mgombea nafasi ya Ujumbe wa Serikali ya Mtaa wa Ulongoni A, Kata ya Gongolamboto, Jimbo la Ukonga, Dar es Salaam aliyeuwawa na askari kwa kupigwa risasi wakati wa purukushani za kuzuia kura bandia na batili kuingizwa kituo cha kupiga kura.
3)George Juma Mohammed wa Kitongoji cha Stand Kata ya Mkwese Jimbo la Manyoni Mkoani Singida aliyevamiwa nyumbani kwake na watu waliofahamika kuwa askari na kumpiga risasi iliyomsababishia umauti.

Aidha, tuna taarifa kadhaa za kujeruhiwa na kukamatwa na Polisi viongozi, wagombea, wanachama na wapenzi wetu maeneo mbalimbali ya nchi walipokuwa wakijitahidi kukamata na kuzuia kuingizwa vituoni kura bandia na batili zilizopigwa tayari kuwabeba wagombea wa CCM.

Tunataka watu wetu hawa waachiwe haraka na bila masharti yeyote.

Tunaendelea kuwasiliana na Chama kitatoa tamko rasmi zoezi hili likikamilika.

Tunaamini kinachofanyika kina maagizo na baraka zote za @SuluhuSamia na Serikali yake na au nchi iko kwenye "autopilot" na yeyote katika eneo lake ana mamlaka ya kunajisi uchaguzi anavyotaka kwani tayari wamepewa kinga na Kanuni ya 49 ya Kanuni za Uchaguzi wa Viongozi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa, Ngazi ya Vijiji, Vitongoji na Mitaa inayosema, nanukuu:

"Msimamizi wa Uchaguzi, Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi, Msimamizi wa Kituo, Wajumbe wa Kamati ya Rufani au mtumishi yeyote wa Umma aliyehusika na usimamizi wa uchaguzi hatowajibika kwa Jinai au Madai au kuchukuliwa kwa hatua za kinidhamu au za kiutawala kwa jambo lolote alilolifanya au kuacha kulifanya kwa nia njema wakati wa kutekeleza majukumu yake chini ya Kanuni hizi". Mwisho wa kunukuu.

Hakika Taifa lina Msiba mwingine!!
 
Wakuu,

Maake hapo kwanza ncheke!

===

Jeshi la Polisi mkoani Rukwa limetoa ufafanuzi wa taarifa inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu vijana sita wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kukamatwa nyumbani kwa Mbunge wa Jimbo la Nkasi Kaskazini, Aida Kenan wakiwa na petroli lita 20 kwa lengo la kuiangamiza familia ya mbunge huyo.

Katika taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi, imesema uchunguzi wa awali unaonesha kuwa vijana hao waliokamatwa na wafuasi wa CHADEMA, walifika nyumbani kwa Mkuu wa Wilaya ya Nkasi, Peter Lijualikali majira ya saa moja jioni wakiwa na pikipiki mbili na dumu lenye mafuta ya petroli lita 20, kwa lengo la kuchukua pikipiki zingine zilizokuwa hapo na kuziwekea mafuta.

“Kwa kuwa nyumbani kwa Mkuu wa Wilaya na nyumbani kwa Mbunge ni karibu sana nyumba zao zikitenganishwa na barabara, ndipo vijana hao walipokamatwa na kutuhumiwa kwamba walikuwa na lengo la kuchoma moto nyumba ya Mbunge Aida,” imeeleza taarifa ya Polisi.

Pia soma:
- LGE2024 - Nkasi: Wanaodaiwa kutumwa na DC kulipua nyumba ya Mbunge Aida Kenani usiku huu wakamatwa, wametumia pikipiki za Samia
Erythrocyte unaona uhuni wa polisi. Litolee tamko kali kulaani
 
Wakuu,

Maake hapo kwanza ncheke!

===

Jeshi la Polisi mkoani Rukwa limetoa ufafanuzi wa taarifa inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu vijana sita wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kukamatwa nyumbani kwa Mbunge wa Jimbo la Nkasi Kaskazini, Aida Kenan wakiwa na petroli lita 20 kwa lengo la kuiangamiza familia ya mbunge huyo.

Katika taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi, imesema uchunguzi wa awali unaonesha kuwa vijana hao waliokamatwa na wafuasi wa CHADEMA, walifika nyumbani kwa Mkuu wa Wilaya ya Nkasi, Peter Lijualikali majira ya saa moja jioni wakiwa na pikipiki mbili na dumu lenye mafuta ya petroli lita 20, kwa lengo la kuchukua pikipiki zingine zilizokuwa hapo na kuziwekea mafuta.

“Kwa kuwa nyumbani kwa Mkuu wa Wilaya na nyumbani kwa Mbunge ni karibu sana nyumba zao zikitenganishwa na barabara, ndipo vijana hao walipokamatwa na kutuhumiwa kwamba walikuwa na lengo la kuchoma moto nyumba ya Mbunge Aida,” imeeleza taarifa ya Polisi.

Pia soma:
- LGE2024 - Nkasi: Wanaodaiwa kutumwa na DC kulipua nyumba ya Mbunge Aida Kenani usiku huu wakamatwa, wametumia pikipiki za Samia
Kabisa yaani, Tunaishukuru Polisi kwa umakini mkubwa sana!
 
Back
Top Bottom