LGE2024 Polisi Songwe wafanya doria kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

LGE2024 Polisi Songwe wafanya doria kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Saa chache kabla ya kufanyika kwa uchaguzi wa Serikali za mitaa, vitongoji na vijiji kesho Jumatano tarehe 27 Novemba, 2024 Jeshi la Polisi mkoa wa Songwe mapema leo Novemba 26, 2024 limefanya doria za magari na miguu katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Songwe ikiwemo mji wa Tunduma wilaya ya Momba, Isongole na Itumba wilaya ya Ileje pamoja na kata ya Vwawa na Mji Mdogo wa Mlowo wilaya ya Mbozi ikiwa ni sehemu ya kuimarisha ulinzi na usalama.
1732632956484.png
Akizungumza baada ya doria hiyo, Mkuu wa Operesheni mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi wa Polisi, ACP Nicholaus Livingstone amesema kuwa doria hiyo ni sehemu ya kuimarisha ulinzi katika maeneo ya mkoa wa Songwe na viunga vyake.

ACP Livingstone amesema kuwa doria katika vitongoji, vijiji, mitaa na kata mbalimbali ndani ya mkoa wa Songwe zinazofanywa na Jeshi hilo ni sehemu ya kujua changamoto za kiusalama zinazowakabili wananchi na kuchukua hatua za haraka za kuzitatua ili mkoa huo uendelee kuwa salama.
1732632973927.png
Vilevile ACP Livingstone amewataka wananchi wa mkoa huo kuendelea na shughuli zao za kujitafutia kipato bila wasiwasi wowote kwani Jeshi lao la Polisi mkoani humo lipo imara kuhakikisha ulinzi na usalama wa raia na mali zao unaendelea kuwepo wakati wote.

Ikumbukwe kuwa magari hayo ya doria na vitendea kazi vingine ni sehemu ya juhudi ya Serikali ambayo imekuwa ikitoa vifaa mbalimbali kwa awamu ili kuboresha utendaji kazi wa Polisi.
1732633012764.png

1732633138231.png
 
Mimi sioni sababu ya kufanya uchaguzi kama mambo yenyewe ndio kama haya . Ni bora Tanzania ijulikane tu kwamba ina chama kimoja cha siasa maana uhuni unaofanywa huko mikoani juu ya uchaguzi huu haufai kabisa, yaani yote hii ni ili kutaka kupata uhali wa watu wa chama flani katika uchaguzi ujao, which is not something on the ground,let them allow democracy prevail .
 
Saa chache kabla ya kufanyika kwa uchaguzi wa Serikali za mitaa, vitongoji na vijiji kesho Jumatano tarehe 27 Novemba, 2024 Jeshi la Polisi mkoa wa Songwe mapema leo Novemba 26, 2024 limefanya doria za magari na miguu katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Songwe ikiwemo mji wa Tunduma wilaya ya Momba, Isongole na Itumba wilaya ya Ileje pamoja na kata ya Vwawa na Mji Mdogo wa Mlowo wilaya ya Mbozi ikiwa ni sehemu ya kuimarisha ulinzi na usalama.
Akizungumza baada ya doria hiyo, Mkuu wa Operesheni mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi wa Polisi, ACP Nicholaus Livingstone amesema kuwa doria hiyo ni sehemu ya kuimarisha ulinzi katika maeneo ya mkoa wa Songwe na viunga vyake.

ACP Livingstone amesema kuwa doria katika vitongoji, vijiji, mitaa na kata mbalimbali ndani ya mkoa wa Songwe zinazofanywa na Jeshi hilo ni sehemu ya kujua changamoto za kiusalama zinazowakabili wananchi na kuchukua hatua za haraka za kuzitatua ili mkoa huo uendelee kuwa salama.
Vilevile ACP Livingstone amewataka wananchi wa mkoa huo kuendelea na shughuli zao za kujitafutia kipato bila wasiwasi wowote kwani Jeshi lao la Polisi mkoani humo lipo imara kuhakikisha ulinzi na usalama wa raia na mali zao unaendelea kuwepo wakati wote.

Ikumbukwe kuwa magari hayo ya doria na vitendea kazi vingine ni sehemu ya juhudi ya Serikali ambayo imekuwa ikitoa vifaa mbalimbali kwa awamu ili kuboresha utendaji kazi wa Polisi.
Haya ndiyo makaburu yetu
 
Yakitokea majanga
Huwaoni 😄
Ila mambo hayo wanayaweza

Ova
 
Cho
Saa chache kabla ya kufanyika kwa uchaguzi wa Serikali za mitaa, vitongoji na vijiji kesho Jumatano tarehe 27 Novemba, 2024 Jeshi la Polisi mkoa wa Songwe mapema leo Novemba 26, 2024 limefanya doria za magari na miguu katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Songwe ikiwemo mji wa Tunduma wilaya ya Momba, Isongole na Itumba wilaya ya Ileje pamoja na kata ya Vwawa na Mji Mdogo wa Mlowo wilaya ya Mbozi ikiwa ni sehemu ya kuimarisha ulinzi na usalama.
Akizungumza baada ya doria hiyo, Mkuu wa Operesheni mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi wa Polisi, ACP Nicholaus Livingstone amesema kuwa doria hiyo ni sehemu ya kuimarisha ulinzi katika maeneo ya mkoa wa Songwe na viunga vyake.

ACP Livingstone amesema kuwa doria katika vitongoji, vijiji, mitaa na kata mbalimbali ndani ya mkoa wa Songwe zinazofanywa na Jeshi hilo ni sehemu ya kujua changamoto za kiusalama zinazowakabili wananchi na kuchukua hatua za haraka za kuzitatua ili mkoa huo uendelee kuwa salama.
Vilevile ACP Livingstone amewataka wananchi wa mkoa huo kuendelea na shughuli zao za kujitafutia kipato bila wasiwasi wowote kwani Jeshi lao la Polisi mkoani humo lipo imara kuhakikisha ulinzi na usalama wa raia na mali zao unaendelea kuwepo wakati wote.

Ikumbukwe kuwa magari hayo ya doria na vitendea kazi vingine ni sehemu ya juhudi ya Serikali ambayo imekuwa ikitoa vifaa mbalimbali kwa awamu ili kuboresha utendaji kazi wa Polisi.
Chondechonde polisi msitumike kuiba kura maana mtalaanika na visasi vyenu. Kazi yenu ibaki kulinda amani kwa haki bila kutumika kwa namna yoyote ile.
 
Saa chache kabla ya kufanyika kwa uchaguzi wa Serikali za mitaa, vitongoji na vijiji kesho Jumatano tarehe 27 Novemba, 2024 Jeshi la Polisi mkoa wa Songwe mapema leo Novemba 26, 2024 limefanya doria za magari na miguu katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Songwe ikiwemo mji wa Tunduma wilaya ya Momba, Isongole na Itumba wilaya ya Ileje pamoja na kata ya Vwawa na Mji Mdogo wa Mlowo wilaya ya Mbozi ikiwa ni sehemu ya kuimarisha ulinzi na usalama.
Akizungumza baada ya doria hiyo, Mkuu wa Operesheni mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi wa Polisi, ACP Nicholaus Livingstone amesema kuwa doria hiyo ni sehemu ya kuimarisha ulinzi katika maeneo ya mkoa wa Songwe na viunga vyake.

ACP Livingstone amesema kuwa doria katika vitongoji, vijiji, mitaa na kata mbalimbali ndani ya mkoa wa Songwe zinazofanywa na Jeshi hilo ni sehemu ya kujua changamoto za kiusalama zinazowakabili wananchi na kuchukua hatua za haraka za kuzitatua ili mkoa huo uendelee kuwa salama.
Vilevile ACP Livingstone amewataka wananchi wa mkoa huo kuendelea na shughuli zao za kujitafutia kipato bila wasiwasi wowote kwani Jeshi lao la Polisi mkoani humo lipo imara kuhakikisha ulinzi na usalama wa raia na mali zao unaendelea kuwepo wakati wote.

Ikumbukwe kuwa magari hayo ya doria na vitendea kazi vingine ni sehemu ya juhudi ya Serikali ambayo imekuwa ikitoa vifaa mbalimbali kwa awamu ili kuboresha utendaji kazi wa Polisi.

Siku nyingine zote kuimarisha usalama hakuna maana????
 
Back
Top Bottom