Polisi: Tunamshikilia Franco Ruhinda, hajatekwa

Polisi: Tunamshikilia Franco Ruhinda, hajatekwa

Mtoa Taarifa

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2024
Posts
213
Reaction score
671
Screenshot_2024-11-05-07-04-37-328_com.instagram.android-edit.jpg

Kuna taarifa zinazotengenezwa na kusambazwa katika makundi sogozi yenye nia ya kudanganya ili kuleta taharuki kwa umma kumhusu Franco Kashaija Ruhinda kuwa haijulikani alipo toka alipowasili nchini akitokea Dubai.

Jeshi la Polisi lingependa kutoa taarifa kuwa Franco Kashaija Ruhinda alikamatwa alipowasili nchini Novemba 3,2024 kwa tuhuma za kujihusisha na Uhalifu wa kupanga na bado anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi ili kukamilisha yaliyokuwa yamesalia katika uchunguzi ili hatua zingine za kisheria zifuate.

Imetolewa na:
David A. Misime - DCP Msemaji wa Jeshi la Polisi Dodoma, Tanzania.

ruhinda.jpg
 
Picha yake tafadhali!
 
Sawa Jeshi la Polisi mtu mkimkamata mpelekeni mahakamani kwa tuhuma zinazomkabili mtaendelea kupata hizi tuhuma kwa mfumo huu wa kizamani mnaotumia yaani mnamkamata mtu bila kutoa taarifa watu wakihoji mnajitokeza akipotea kweli nanyi mnajifanya kumtafuta kazi ipo hapo..
 
Yaani nilipoona jina la kihaya tu, nikajua lazima atakuwa tapeli. Chadema wamekithiri kwa habari za uongo
 
View attachment 3143852

Kuna taarifa zinazotengenezwa na kusambazwa katika makundi sogozi yenye nia ya kudanganya ili kuleta taharuki kwa umma kumhusu Franco Kashaija Ruhinda kuwa haijulikani alipo toka alipowasili nchini akitokea Dubai.

Jeshi la Polisi lingependa kutoa taarifa kuwa Franco Kashaija Ruhinda alikamatwa alipowasili nchini Novemba 3,2024 kwa tuhuma za kujihusisha na Uhalifu wa kupanga na bado anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi ili kukamilisha yaliyokuwa yamesalia katika uchunguzi ili hatua zingine za kisheria zifuate.

Imetolewa na:
David A. Misime - DCP Msemaji wa Jeshi la Polisi Dodoma, Tanzania.
View attachment 3143855View attachment 3143856
Viazi wa Taifa wanafanya ukamataji kwa mtindo wa kuteka nyara halafu wanakuja kujieleza fyoko fyeke fyoko. Mtu mnamkamata na kunyakua simu zake halafu mtuambie hajatekwa nyara?

Wajinga sana hawa mandata
 
Jeshi letu lijotahidi kukamata mtu baada ya kukusanya ushahidi wa kutosha kumpeleka mahakamani. Tupunguze hii mambo ya tunamshikilia uchunguzi ukikamilika tutampeleka mahakamani.
 
Kichaka cha wahalifu siku hizi ni kutekwa, Kuna mambo ya Ki Police kiuchunguzi huwa lazima yapindishe sheria kidogo!
 
Angetujibu maswali yafuatayo huyo msemaji wa jeshi letu
1. Sheria zilifuatwa pindi Mtuhumiwa aliposhikwa?
2. Mtuhumiwa anatakiwa kupelekwa mahakamani baada ya muda gani? Huo muda umefuatwa?
3. Definition ya kutekwa (abduction) kwa jeshi la polisi ni ipi?
 
Wakati anakamatwa alipewa haki ya kujulisha Familia, Mwanasheria, Balozi, n.k ?

Kama hakupewa haki hizo basi Alitekwa.
Hiyo ndiyo hoja ya msingi ...hii serikali pumbavu ya sa100 inawaona watanzania wapumbavu kama wao ,..
 
Katika hali ya kukamatwa, mtu ana haki ya kujulisha familia, mwanasheria, na mara nyingine hata balozi, kulingana na sheria za nchi husika na mkataba wa kimataifa wa haki za binadamu. Ikiwa mtu hakupata haki hizo, inaweza kuashiria kuwa ametekwa au kukamatwa kwa njia isiyo halali.

Haki hizi ni sehemu ya mchakato wa kuhakikisha kwamba mtu anapewa ulinzi wa kisheria na haki za kibinadamu. Kukosekana kwa haki hizi kunaweza kuleta wasiwasi kuhusu taratibu za kisheria zinazotumika katika kukamatwa kwake.

Ikiwa unahitaji maelezo zaidi au msaada kuhusu kesi maalum, ni vyema kuwasiliana na mwanasheria mwenye ujuzi katika masuala ya haki za binadamu.
 
Back
Top Bottom