Polisi wa Kuzuia Fujo wasambazwa jijini Dar: Ni kutangaza hali ya hatari?

Polisi wa Kuzuia Fujo wasambazwa jijini Dar: Ni kutangaza hali ya hatari?

nguvu ya umma wanaisikia tu hawajawahi kuishuhudia ila siku moja wataishuhudia
 
Wanafanya zao doria za kawaida tu we endelea na shughuli zako
 
swali hili unatakiwa uliulize iwapo utawaona JWTZ wapo mitaani kwa utayari. lakini hawa police swali lako umeliwahisha sana.
 
21 September 2024

Ulinzi umeimarishwa jijini Dar es Salaam huku magari ya polisi yakionekana yakizunguka kuweka ukuta wa kufikirika


View: https://m.youtube.com/watch?v=IJgCHuVI4dA

Tanzania ni nchi ya kipekee kwa kutoonekana askari polisi kuzagaa ambapo nchi zingine kama Ethiopia, Kenya n.k ni kawaida huko kuona hali hiyo kila siku huku vizuizi vya mageti ya misumari kutoboa matairi hukweka na polisi.

Katika hali isiyokuwa ya kawaida, maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam leo 21 September 2024 yamejaa askari wa Jeshi la Polisi, wanaozunguka huku na kule.

TOKA MAKTABA :
Ikulu
Dar es Salaam, Tanzania

View attachment 3101983
20 September 2024 amiri jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama ambaye ni Rais Samia Hassan alipowaita IGP Camilius Wambura na viongozi wakuu waandamizi wa jeshi la Polisi katika Ikulu ya Dar es Salaam.
View attachment 3101984

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dr. Samia S. Hassan akiwa ktk picha ya pamoja, mara baada ya Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP) Camillus Wambura pamoja na Makamishna wa Jeshi hilo kumaliza mkutano uliyo fanyika Ikulu Jijini Dar es salaam tarehe 20 Septemba, 2024.



Mama wa teka teka. Iko siku utaondoka madarakani na kujuta kama Mkapa
 
Mtawala akiona ana mamlaka ya uhai ya wanachi ndio shida inaanzia hapo
Raisi kajikuta kiziwi
yanayolalamikiwa na wananchi kachukua uuzaji personal ya kichama badala ya kutafuta suluhu kama jina lake linavojinadi na linavotamkwa

Wanaomshauri kutoa speech ile wameharibu kila kitu speech ya kujaza hamasa na nia ovu kwa wananchi
Chadema wanaweza wasifanikiwe kwenye maandamano vipi kihusu uelewa wa raia ambao wameeanza kuandamana kila mahali Kuhusu kudai haki zao za msingi. Ngorongoro , dar es salaam , Simanjiro na kwingine

Washauri wake hawamtakii mema ipo siku vijana wa kukosa ajira wakiamka ndio balaa zaidi maana hatasaidiwa na polisi kabsa

Anahitaji suluhu zaidi ya polisi ipo siku yake jazba na kiburi alichinacho ipo siku ataona havina muhimu zaidi ya kutafuta suluhu kumbe muda utakua umeenda
 
Damu zitakazomwagwa na polisi hawa Jumatatu ndiyo kaburi la CCM. Rais ameingizwa chaka kiboya sana
Nakwambia utakuja kuniambia jumatatu hakuna maandamano yoyote yataofanikiwa zaidi ya vurugu uchwara na watadhibitiwa mapema sana
 
nguvu ya umma wanaisikia tu hawajawahi kuishuhudia ila siku moja wataishuhudia
Mtawala akiona ana mamlaka ya uhai ya wanachi ndio shida inaanzia hapo
Raisi kajikuta kiziwi
yanayolalamikiwa na wananchi kachukua uuzaji personal ya kichama badala ya kutafuta suluhu kama jina lake linavojinadi na linavotamkwa

Wanaomshauri kutoa speech ile wameharibu kila kitu speech ya kujaza hamasa na nia ovu kwa wananchi
Chadema wanaweza wasifanikiwe kwenye maandamano vipi kihusu uelewa wa raia ambao wameeanza kuandamana kila mahali Kuhusu kudai haki zao za msingi. Ngorongoro , dar es salaam , Simanjiro na kwingine

Washauri wake hawamtakii mema ipo siku vijana wa kukosa ajira wakiamka ndio balaa zaidi maana hatasaidiwa na polisi kabsa

Anahitaji suluhu zaidi ya polisi ipo siku yake jazba na kiburi alichinacho ipo siku ataona havina muhimu zaidi ya kutafuta suluhu kumbe muda utakua umeenda
Nakwambia utakuja kuniambia jumatatu hakuna maandamano yoyote yataofanikiwa zaidi ya vurugu uchwara na watadhibitiwa mapema sana
Chadema wanaweza wasifanikiwe kuhusu Maandamano yao hayo ambayo wamepanga kuyafanya hapo tarehe 23 Septemba, 2024. Isipokuwa Hakuna kitu kibaya hapa duniani Kama watu (raia) kufanya Maandamano ya Rohoni, hiyo ni hatari Sana kupita kiasi. Mathalani, nchi ya Iran inakabiliwa na kitisho kikubwa Sana cha Maandamano ya namna hii, Watawala wa nchi hiyo wamepiga marufuku kabisa mtu yoyote yule kuandamana kwa wazi Wazi katika nchi hiyo, na wananchi nao wamebuni njia nyingine mbadala ya kuandamana kwa kufanya maandamano ya rohoni ambayo nchi hiyo imekuwa ikikumbwa na madhara makubwa Sana kutokana na maandamano ya namna hiyo.
 
ANGUKO LA CHAMA DOLA KULE NCHINI ROMANIA, BAADA YA HOTUBA IILIYOSHANGILIWA NA WENGI


View: https://m.youtube.com/watch?v=TcRWiz1PhKU

Nicolae Ceaușescu (matamshi ya Kiromania: [nikoˈla.e t͡ʃe̯a.uˈʃesku]; 26 Januari 1918 -- 25 Desemba 1989) alikuwa mwanasiasa wa Kikomunisti wa nchini Romania.

Alikuwa Kiongozi mkuu wa Chama cha Kikomunisti cha Romania kuanzia 1965 hadi 1989, na kwa hivyo alikuwa kiongozi wa pili na wa mwisho wa Kikomunisti nchini humo.

Pia alikuwa mkuu wa nchi kutoka 1967 hadi 1989. Utawala wake uliwekwa alama katika muongo wa kwanza na sera ya wazi kuelekea Ulaya Magharibi na Marekani, ambayo ilikengeuka kutoka kwa mataifa mengine ya Warsaw Pact wakati wa Vita Baridi.

Aliendelea na mtindo ulioanzishwa kwanza na mtangulizi wake, mwendazake Gheorghe Gheorghiu-Dej, ambaye kwa busara alishawishi Muungano wa Sovieti kuondoa wanajeshi wake kutoka Rumania mwaka wa 1958. , serikali kali zaidi ya Stalinist katika kambi ya Soviet.


Ilikuwa pia awamu ya muendelezo wa kuitupilia mbali Sera ya utu na kuingiza sera ya mkono wa chuma wenye damu iliyoenea kila mahali, uzalendo uchwara na kuzorota kwa uhusiano wake na wadau wa maendeleo wa kimataifa na madola ya Magharibi na Umoja wa Kisovieti.

Serikali ya Ceaușescu ilipinduliwa katika mapinduzi ya Desemba 1989, na yeye na mke wake kuhukumiwa adhabu ya juu kufuatia kikao cha mahakama cha saa mbili kilichorushwa na televisheni na kwa haraka.

ENGLISH:
Nicolae Ceaușescu (Romanian pronunciation: [nikoˈla.e t͡ʃe̯a.uˈʃesku]; 26 January 1918 -- 25 December 1989) was a Romanian Communist politician.

He was Secretary General of the Romanian Communist Party from 1965 to 1989, and as such was the country's second and last Communist leader. He was also the country's head of state from 1967 to 1989.

His rule was marked in the first decade by an open policy towards Western Europe and the United States, which deviated from that of the other Warsaw Pact states during the Cold War.

He continued a trend first established by his predecessor, Gheorghe Gheorghiu-Dej, who had tactfully coaxed the Soviet Union into withdrawing its troops from Romania in 1958.

Ceaușescu's second decade was characterized by an increasingly brutal and repressive regime—by some accounts, the most rigidly Stalinist regime in the Soviet bloc.

It was also marked by an ubiquitous personality cult, nationalism and a deterioration in foreign relations with the Western powers as well as the Soviet Union.

Ceaușescu's government was overthrown in the December 1989 revolution, and he and his wife were executed following a televised and hastily organised two-hour court session.
 
Ulinzi umeimarishwa au wameshikwa na kiwewe???

Hata hivyo, Siyo kweli hata kidogo kwamba SSH au JPM ndio chanzo cha kushamiri kwa vitendo vya Utekaji na Mauaji hapa nchini kwa sababu tatizo lililopo siyo JPM wala siyo SSH, Bali tatizo ni kwamba Tanzania kuna Katiba mbaya sana pamoja na Sheria zilizopo ni mbaya sana ambazo pia ni sheria kandamizi.

Aidha, nasisitiza kwamba kutokana na kuwepo kwa janga la vitendo viovu hapa Tanzania, chanzo chake au tatizo siyo JPM wala siyo SSH. Mathalani, JPM tayari ameondoka zake, na SSH naye ipo siku lazima ataondoka, lakini vitendo viovu vya Utejaji, utesaji na Mauaji kamwe havitaondoka, na badala yake vitaendekea kuwepo kwa sababu Katiba na Sheria zinazohalalisha vitendo hivyo viovu kuwepo bado zipo na wala hazijaondolewa kutoka hapa nchini Tanzania.
Katiba na sheria ni zawakoloni watu wanaishi kwa hisani ya Rais tuliondoa mkoloni tukabakiza katiba yake ambayo ndo mkoloni mwenyewe
 
Mambo haya ni mepesi saana, sema uwoga wa CCM umetufikisha hapa, jamaa wana maovu mengi wanaogopa hadi maandamano ambayo katiba ya nchi imeruhusu.
 
Hiyo ni nguvu ya Chadema.

Sasa kuna siku watakutana na nguvu ya umma.
Yatawakuta siku moja ya Bangladesh.Watu sijui wakoje.Hivi kwani kuna shida gani,kwa nini wasiachie hao mateka wanaotakiwa na chadema? Hivi kama kweli wana nia njema na nchi,kuna ubaya gani kuwaachia kina soka ? Nasikitika sana.Ccm inatupeleka pabaya .
 
Nguvu ya Umma itakuja yenyewe tu bila kupitia vyama amini ilo hapo ndo itakua balaah

Ni kweli chama dola kongwe kijitokeze kunusuru tunapoelekea kwa CCM kukaza shingo kwa kiburi kutotaka kuongea kwa nia njema na chama cha kisiasa kinachosikilizwa pia kukubaliwa kinawawakilisha sehemu kubwa ya umma wa waTanzania.

Umma utapogundua na kuona hata chama wanachokikubali kinachobeba matumaini yao kinasakamwa na kudoofishwa kwa njia za kiuovu na umma ukaamua sasa watachukua mamlaka mikononi mwao kujinusuru kwakuwa tegemeo lao kupitia mfumo rasmi wa kisiasa umeharamishwa kwa chama dola tawala kutumia mbinu chafu.

Basi umma huo unaweza kujichukulia mamlaka mikononi mwake huku hakuna tena viongozi wa kuwatuliza kama kule wakati wa mazishi ya kiongozi wa CHADEMA marehemu Ali Mohamed Kibao mjini Tanga, hali ya nchi itakuwa ngumu na CCM itakuwa hawana chama cha upinzani kukishawishi kupoza hasira za umma.
 
Back
Top Bottom