Polisi wabadili gia angani, Wanadai hawajui alipo Mfanyakazi wa LHRC Tito Magoti

Polisi wabadili gia angani, Wanadai hawajui alipo Mfanyakazi wa LHRC Tito Magoti

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi Kinondoni asema hana taarifa za kukamatwa na kushikiliwa kwa mwanaharakati,Tito Magoti

Mussa Taibu amesema kuwa mpaka sasa hana taarifa ya kukamatwa kwa Ofisa wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu [LHRC] Tito Magoti, katika eneo la himaya yake na hata amejaribu kuwauliza wenzake lakini nao hawana taarifa hizo.

Awali Kamanda Lazaro Mambosasa aliuthibitisha Umma kwamba Magoti alikamatwa Mwenge wilayani Kinondoni

Taarifa za awali kuhusu kutekwa kwa Tito Magoti ni kuwa alikuwa katika bodaboda akielekea Mwenge kununua simu, alipofika katika kituo cha mafuta cha Puma watu 5 waliokuwa na gari aina ya Harrier walimchukua kwa mabavu kisha kuondoka kwa uelekeo wa Posta, Dar es Salaam.

Jana Kamanda wa Polisi wa Kanda ya Dar, Lazaro Mambosasa amekaririwa akisema Polisi inamshikiliwa Magoti na wenzake watatu kwa uchunguzi wa tuhuma za makosa ya jinai inayowakabilia.

Hata hivyo, Mambosasa hajawahi kubainisha ni kituo gani ambacho Magoti anashikiliwa.

Zaidi, soma:


 
Duh....

Hii ni hatari sana......

Wanawezaje hivi sasa kukanusha, wakati hapo nyuma waliikiri kuwa wao ndiyo wanaomshikilia huyo Tito Magoti?

Huu ni ushahidi wa mazingira kuwa wao Polisi, kumbe ndiyo wale watu tunaofahamishwa kuwa ni watu WASIOJULIKANA!
 
Mpaka tutekwe wote ndio tutajua umuhimu wa kuungana kama Taifa kupinga huu udhalimu.

Naanza kupata mashaka kama Tito bado tunae na kama tunae,basi sijui atakuwa katika hali gani.

Ukiona hivi, ujue kuna uwezekana wa mambo mawawili:wamemtanguliza au wamemuumiza na kumjeruhi vibaya kiasi kwamba hawako tayari kuhusishwa/kutuhumiwa na hivyo tunaweza kumuokota akiwa kama Dr.Ulimboka.
 
Jeshi la polisi lilimkamata Tito Magoti kwa madai eti anatumia fake I'd kuitukana serikali huku wakimhusisha na Kigogo wa Twitter pamoja na I'd ya member maarufu mkosoaji wa Jf...Cha ajabu watu waliohusishwa naye bado wapo wanapost tu...Leo wanasema hawajui alipo ili baadaye wakamtelekeze sehemu kama walivyofanya kwa Mo baada ya kumsainisha nyaraka muhimu kwa nguvu.
 
Duh....

Hii ni hatari sana......

Wanawezaje hivi sasa kukanusha, wakati hapo nyuma waliikiri kuwa wao ndiyo wanaomshikilia huyo Tito Magoti?

Huu ni ushahidi wa mazingira kuwa wao Polisi, kumbe ndiyo wale watu WASIOJULIKANA!
ndo mnajua leo, halafu bado akipotea mtu mnasema amechukuliwa na watu wasiojulikana,
 
[emoji44][emoji44][emoji44][emoji44][emoji44][emoji44][emoji125][emoji125][emoji125]
Kamanda wa Polisi Kinondoni, Mussa Taibu amesisitiza hana taarifa za kukamatwa kwa Tito Magoti wa LHRC kwenye himaya yake licha ya Kamanda Lazaro Mambosasa kuthibitisha alikamatwa Mwenge wilayani Kinondoni #MwananchiUpdates

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom