Polisi wabadili gia angani, Wanadai hawajui alipo Mfanyakazi wa LHRC Tito Magoti

Polisi wabadili gia angani, Wanadai hawajui alipo Mfanyakazi wa LHRC Tito Magoti

Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi Kinondoni asema hana taarifa za kukamatwa na kushikiliwa kwa mwanaharakati,Tito Magoti

Awali Kamanda Lazaro Mambosasa aliuthibitisha Umma kwamba Magoti alikamatwa Mwenge wilayani Kinondoni

Zaidi, soma:

View attachment 1301209
View attachment 1301208

Chuki inazidi kukolezwa na wao wenyewe wenye Mamlaka. Kwani kama ana tuhuma au makosa si wangemkamata kwa kufuata utaratibu tu!? Taifa linaendekeza chuki!
 
Mpaka tutekwe wote ndio tutajua umuhimu wa kuungana kama Taifa kupinga huu udhalimu.

Naanza kupata mashaka kama Tito bado tunae na kama tunae,basi sijui atakuwa katika hali gani.

Ukiona hivi, uje kuna mawawili:wamemtanguliza au wamemuumiza na kumjeruhi vibaya kiasi kwamba hawako tayari kuhusishwa/kutuhumiwa na hivyo tutarajie kumuokota akiwa kama Dr.Ulimboka.
Na mimi nahisi hivyo, aidha ndio bai bai au amepigwa sana wanashindwa kumtoa
 
Mpaka tutekwe wote ndio tutajua umuhimu wa kuungana kama Taifa kupinga huu udhalimu.

Naanza kupata mashaka kama Tito bado tunae na kama tunae,basi sijui atakuwa katika hali gani.

Ukiona hivi, uje kuna mawawili:wamemtanguliza au wamemuumiza na kumjeruhi vibaya kiasi kwamba hawako tayari kuhusishwa/kutuhumiwa na hivyo tutarajie kumuokota akiwa kama Dr.Ulimboka.
Hata suala na Ben Saanane inaweza ikawa hivyo hivyo. Wakishakutesa wakaona umetepa au unaweza kuwafia wanakupoteza kabisa.
 
Na makanisani msiwe mnaenda. Chagua kuishi kama mashetani. Tunawaona mtangaza Upendo ,Amani,Mshikamano. Huyo Mungu mnayemwomba alete Amani ndo huyu wa Yakobo Isaka na Ibrahimu ?.Sasa tulipigania uhuru kwa ajili gani kama kama watu wanachukuliwa na kuahawa kila siku?. Tabia hii italipeleka taifa pabaya .Taifa litapasuka kwa tabia hii Tunakemea na kulaani kila siku juu ya tabia hii nyie mnaendelea na vichwa vyenu vigumu.
 
Mpaka tutekwe wote ndio tutajua umuhimu wa kuungana kama Taifa kupinga huu udhalimu.

Naanza kupata mashaka kama Tito bado tunae na kama tunae,basi sijui atakuwa katika hali gani.

Ukiona hivi, uje kuna mawawili:wamemtanguliza au wamemuumiza na kumjeruhi vibaya kiasi kwamba hawako tayari kuhusishwa/kutuhumiwa na hivyo tutarajie kumuokota akiwa kama Dr.Ulimboka.
Hivi hawa watu wafanyao hivi wanafanya kwa niaba ya nani? Jee huyo anayewatuma SIO ADUI WA TAIFA HUYO?
Tuvumilie hiki kitu hadi lini? Hata hawa wenzetu tulio nao hapa JF wanao unga mkono utekaji na mateso kwa nini na sisi tusiwashukie kama mwewe hata kama ni kupigwa ban potelea mbali au tuwaweke wote kwenye ignore list?
Moyo wangu ni mzito sana nikiwaza yakuwa pengine Tito kateswa na kafa au yuko hoi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom