Polisi wakana tuhuma za kuhusika kifo cha Jacob Elias

Polisi wakana tuhuma za kuhusika kifo cha Jacob Elias

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
Wakati mwili wa Jacob Elias (44) mkazi wa Milanzi Manispaa ya Tabora anayedaiwa kufariki dunia kutokana na kipigo alichokipata akiwa mahabusu ukizikwa jana Februari 16, 2022, Jeshi la Polisi limekana kuhusika na kifo hicho.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Richard Abwao amekana kuhusika kwa kifo hicho na kudai kuwa marehemu alionekana dhaifu kiafya wakati alipofikishwa kituo cha Polisi.

“Wakati upelelezi ukiendelea mtuhumiwa alibainika kuwa mgonjwa kutokana na kutapika huku akionekana kama mtu mwenye tatizo la ugonjwa wa akili, ndipo Polisi wakampeleka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Kitete kwa matibabu,” ilisema taarifa ya Ambwao.

Aliongeza kuwa kwa mujibu wa ripoti ya daktari aliyempokea na kumhudumia, marehemu Jacob alibainika kuwa na tatizo la kisukari kushuka mwilini na baada ya matibabu Februari 10, 2022 alirejea kituo cha polisi.


Pia soma >
INASIKITISHA; Tuhuma nyingine nzito kwa Jeshi la Polisi, watuhumiwa wawili wafariki Morogoro na Tabora
 
Wakati mwili wa Jacob Elias (44) mkazi wa Milanzi Manispaa ya Tabora anayedaiwa kufariki dunia kutokana na kipigo alichokipata akiwa mahabusu ukizikwa jana Februari 16, 2022, Jeshi la Polisi limekana kuhusika na kifo hicho.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Richard Abwao amekana kuhusika kwa kifo hicho na kudai kuwa marehemu alionekana dhaifu kiafya wakati alipofikishwa kituo cha Polisi.

“Wakati upelelezi ukiendelea mtuhumiwa alibainika kuwa mgonjwa kutokana na kutapika huku akionekana kama mtu mwenye tatizo la ugonjwa wa akili, ndipo Polisi wakampeleka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Kitete kwa matibabu,” ilisema taarifa ya Ambwao.

Aliongeza kuwa kwa mujibu wa ripoti ya daktari aliyempokea na kumhudumia, marehemu Jacob alibainika kuwa na tatizo la kisukari kushuka mwilini na baada ya matibabu Februari 10, 2022 alirejea kituo cha polisi.


Pia soma >
INASIKITISHA; Tuhuma nyingine nzito kwa Jeshi la Polisi, watuhumiwa wawili wafariki Morogoro na Tabora
Nani alishuhudia kukamatwa kwake zaidi ya polisi? PGO inaelezeaje kuhusu kukamatwa watuhumiwa? Poleni wa Tabora, lakini kamata na watuhumiwa wanavyo hojiwa nchini ni kinyume na haki za binadamu, na misingi ya PGO yao.
 
Ukifanyika uchunguzi wa kina ni Watanzania wengi wanapata matatizo na wengine kifo huko Polisi kwenye mikoa yote maana unakuta watu wamejaa vituoni kufatilia ndugu zao Jumatatu kwa kesi za ulevi wa gongo mtaani...
 
Tangu lini polisi wakasema ukweli? Rejea kesi ya zombe na wenzie walivyowaua wafanyabiashaa wa madini toka mahenge nayule dereva wa tax wa sinza,juma ndugu.
 
Back
Top Bottom