Polisi wamsafirisha Niffer hadi Dar kutokea Dodoma baada ya kujisalimisha kufuatia agizo la Waziri Mkuu la kukamatwa

waTz hamjui sheria, na hilo ndio tatizo. Na serikali imezificha kwenye makaratasi badala hata waanzishe kipindi cha mahakama live kama kipindi cha judge Judy channel e, ili watu wa kesi flani ambazo ni za kutoa knowledge kwa wananchi waelewe sheria inasemaje waone live kila kitu, ushahidi, maelezo hadi hukumu.

alichofanya huyo binti amevunja sheria, na sababu alikua hajui sheria hio, ila kutokujua sheria hakukupi kusanehewa kisa hujui sheria. I'm.in law issues, hekima tu is what she need to wish itumike, but ametenda kosa.
 
Bubu....tulia mwizi ni mwizi tu........kwanini akuja Dar kwenye sehemu ya maafa?
 
Sawa sidhani kama nina cha kuendelea kuchangia
 
Uyu dada sio kwamba watu wanamwonea wivu hapana...

Shida ni kwamba ana kiherehere sana na kuishobokea ccm,,mara kumsifia sijui nani anaupiga mwingi..mda wote kujipendekeza kwa serikali tawala..sasa ccm wanamnyoosha ndio maana wengi wanamcheka.

Ajiandae kukaguliwa biashara zake na watoza Kodi 🙂‍↔️🙂‍↔️ na kama tunavojuana wafanyabiashara tunavyofanya bidii kukwepa Kodi za serikali 🤣🤣..

Akitoka uko mwambieni aache uchawa afanye biashara zake kimya..
 
Hii ni Kiki kwa utawala wamechemka sana.. Tabu hawajui wanaharibu sana kwa wananchi.

Na aliyeshupalia anafurahia sana na gesi. Huku yeye wa Maziwa ya mtoto tangu akue.

Upande wa Niffer ni jambo zuri, litapita hili.
Afuate sheria,Niffa ana nia nzuri ila kuna wengine wangetumia mwanya huo huo kutapeli.Serikali ina nia nzuri ,afungue Foundation au apate kibali kama ilivyo sheria.Niffa hata mimi nampenda sana shida nyingine ya Niffa alijibu baada ya waziri mkuu kutoa tamko yeye angenyamaza kimya na watu wangemshauri vizuri yeye akaanza kubishana na mamlaka .Tusitoe visingizio vya kuwa NIFFA ana maadui wengi
 
Kesi ikiisha wata mpatia nauli ya kirudi Dodoma je police wa Dodoma hawawezi kudili na iyo kesi maana kule ndio makao makuu ya nchi. Alafu mbona munapiga picha nusunusu Mimi nataka nione Chura yake maana watu Wana msifia kweli kuwa anamsabwanda.
 
TAARIFA; Jeshi la Polisi limemsafirisha kwenda jijini Dar es salaam Mfanyabiashara wa mtandaoni, Jenifer Jovin, maarufu kama "Niffer" baada ya kujisalimisha Polisi jana jijini Dodoma.

Mfanyabiashara huyo alijisalimisha kwa Jeshi la Polisi jana baada ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kuagiza Jeshi hilo kumhoji kwa kosa la kukusanya fedha za michango kwa ajili ya waathirika walioporomokewa na ghorofa Kariakoo jijini Dar es salaam bila kibali.

"Alijisalimisha jana baada ya kumtafuta, tayari tumeshamsafirisha kwenda jijini Dar es salaam"- Amesema Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma, Anania Amo.
 
Mpuuzi kabisa. Huwezi kufanyia insubordination serekali. Kwamba yenyewe haiwezi kuchanbia au kujipanga lazima uombe kibali
Hakuna sheria inayotukataza kuchangiana wakati wa shida, CCM itueleze zile pesa za tetemeko Kagera na za vifo vya wanafunzi wa Arusha ziko wapi! Mrisho Gambo alisema pesa za Arusha zitajenga hospitali, mpaka sasa hatuioni.
 
Kuchanga na kuchangisha hela yote ni makosa ni km rushwa kutoa na kupokea.

Serikali inachangisha pesa nalo ni kosa coz lipo fungu kwa ajili ya majanga na maafa!
Dah!!?? Sasa inakuwaje? Wa Tz tumezoea kitambo sana kuchangishana au kuchangia linapotokea jambo la Maafa/Janga, Sherehe/Furaha n.k. kwa mwana-Jamii mwenzetu jirani ili kuonesha "Tuko pamoja".
Michango-fedha ipatikanayo hutumika kwa Utaratibu unaoandaliwa ili walau kununua maji ya kunywa au kutayarisha chai kwa wale watakaofika mahali hapo.
Ama kweli Serikali ni siri-kali. Kwanini Serikali imesubiri hadi huyo Niffer afanye kama alivyofanya halafu sasa ndo inajitokeza kwa hasira na kukemea kana kwamba yenyewe ilishatoa Onyo kabla au ilikuwa tayari imeshaanza mchakato huo wa kuwajibika?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…