Yaani Niffer anaonekana ana kosa zaidi ya mwenye ghorofa lililoanguka kwa uzembe....hovyo kabisaJeshi la Polisi limemsafirisha kwenda jijini Dar es Salaam mfanyabiashara wa mtandaoni, Jenifer Jovin maarufu Niffer baada ya kujisalimisha polisi jana.
Mfanyabiashara huyo alijisalimisha kwa Jeshi la Polisi jana baada ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kuagiza Jeshi hilo kumhoji kwa kosa la kukusanya fedha za michango kwa ajili ya waathirika walioporomokewa na ghorofa Kariakoo jijini Dar es Salaam bila kibali.
Pia, Soma:
- Jeshi la Polisi tayari limempata Niffer kwa kuchangisha michango ya wahanga wa Kariakoo
- Niffer atoa majibu baada ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kutaka akamatwe kwa uchangishaji wa fedha kwa ajali ya maafa Kariakoo
Jengo hilo liliporomoka Jumamosi Novemba 16, 2024 na kusababisha vifo vya watu 16, majeruhi 86 na uharibifu wa mali za mamilioni ya fedha.
Akizungumza leo Jumanne Novemba 19, 2024 jijini Dodoma, Kaimu Kamanda wa Polisi wa mkoa huo, Anania Amo amesema Niffer amekamatwa na polisi baada ya kujisalimisha jana.
βAlijisalimisha jana baada ya kumtafuta, tayari tumemsafirisha kwenda jijini Dar es Salaam,βamesema.
Credit: Mwananchi
Kabisa Ni jasiri naweza sema Ni mwanamke anaeongoza Kwa ujasiri TanzaniaHuyu Binti anafaa kugombea Urais!
Ni jambo la aibu kuona ID ya zamani meaning ni mtu mzima halafu akili imejaa tope, unakua chawa wa binti mdogo mpaka kwenye ujinga.....Hii ni Kiki kwa utawala wamechemka sana.. Tabu hawajui wanaharibu sana kwa wananchi.
Na aliyeshupalia anafurahia sana na gesi. Huku yeye wa Maziwa ya mtoto tangu akue.
Upande wa Niffer ni jambo zuri, litapita hili.
Yaani sijaelewa, kutumia hela isivyo au ni curiosity ya kutaka kujua kama zimetumika kwa njia sahihi?Maji ya mil40 kweli?
Li bhnaYaani sijaelewa, kutumia hela isivyo au ni curiosity ya kutaka kujua kama zimetumika kwa njia sahihi?
Yaani kanidissapoint mnoo jamaaMajaliwa anatuangusha tunaomwamini.
Umenisemea brooHuyu binti nimetafakari alipoanzia nikaona ilikuwa hivi:
1. Aliwaza peke yake "Ngoja nitume mchango kwa ajili ya maafa ya mporomoko wa Ghorofa Kariakoo.
2. Akamshirikisha mwenzi, " Nataka nitume hela kuchangia wenzetu waliobanwa kwenye vifusi Kariakoo. "
3. Mwezie akamuumga mkono.
4. Mwezie naye akamtaarifu jirani yake " jamani tunakusanya hela tuzitume Dar kwa walio athirika na maporomoko ya Ghorofa.
5. Wachangiaji wakaongezeka tena na tena na tena.
6. Awali alikuwa mmoja kwa nia njema baada ya muda wakawa wengi kwa nia njema kabisa.
7. Tatizo ni RUKSA HAWAKUPATA.
8. Bila shaka hela zote walizokwisha zichangisha wanazo wakizitoa zote bila kubakiza senti moja mmuachie hakuwa na nia mbaya.
9. Wakimtia ndani wakamfungulia mashitaka huyu binti watakuwa wamekosea kabisa moyo wa kujitolea utakuwa umefifishwa kwa amri ya serikali.
10. Binti kama alikusudia kuiba angefanya kimya kimya, kakini alijiweka wazi. " Tulipoona anachangisha bila kibali tusione yeye ni Mwizi" Binti asamehewe baada yabkuonywa hakuwa nania mbaya kwa mtazamo wangu.
Kama amehama dini tegemea FaizaFoxy kuingilia katiNi jambo la aibu kuona ID ya zamani meaning ni mtu mzima halafu akili imejaa tope, unakua chawa wa binti mdogo mpaka kwenye ujinga.....
Sio kila mtu anamuonea wivu huyo binti,
Infact kwa watu wenye akili timamu tunamuonea huruma, maana ni mgonjwa wa akili tu.....
Hakuna mtu timamu anachukua picha online kutafuta sympathy...
Mara ahame dini kama dozi ya malaria....
Mara adanganye vipodozi location anayonunua...
Mara apondee biashara za watu then later aje afanye...
Then ukuaji wake wa biashara na maisha binafsi havina uhalisia, hata TRA sio mlipa kodi wa level hizo..
Mtu timamu hawezi fanya hayo na mengine mengi..
Kafanya kosa acha awajibishwe iwe funzo kwake na sisi wengine...
Akitoka hapo atapunguza kiherehere.... maana hana maisha nje ya mtandao
Wewe kama jitu zima jitahidi upate akili kidogo uwe unamshauri vizuri role model wako.
Mafuta yapi si amejisalimisha?ila ni kitu gani hao umbwa waliotumwa plus mafuta etc etc na muda pia wangeongeza nguvu hiyo kweye uokoaji si hata watu wawili wangepona? sisi ni viazi usijitetee.
Toa mfano halisi.........kwenye maafa kama haya ya Kariakoo au kwenye tukio gani? πUmbali siyo tatizo mbona wazungu wanachangisha pesa Ulaya na matatizo yapo Kanyenye Tabora uko.
Trump kamshinda Madam Harry.Why?Mwizi kama wezi wengine tu.
Wenye nia nzuri wapo Kariakoo kwenye tukio...............sasa huyo mwenzako yupo Dodoma anachangisha pesa...kwa maafa ya Kariakoo Dar es salaam.....huo ni utapeliKama amekamatwa kwani asitajwe jina kama hawa waliokuwa na nia nzuri wametajwa majina. Ndio amekosa na hasa kujibu yeye angekaa kimyaa tu.
Aliongeza pesa kupitia michango ya janga la kariakoo ya kufunguo Mall yake Dodoma... π πYaani Niffer anaonekana ana kosa zaidi ya mwenye ghorofa lililoanguka kwa uzembe....hovyo kabisa
Si nasikia huyu kasoma na alipata 1.7 O level?au?Pelekeni watoto shule