Naona tunaenda kufanyiwa maigizo tena na kuna mtu anataka kulindwa. Eti uchunguzi umebaini vijana wale hawakutumwa na 'afande na kwamba vijana wale walikuwa kama wavuta bangi tu na yule binti alikuwa kahaba!
Kwani binti mwenyewe anasemaje
 
Tuko bara la giza ambapo kuna watu wapo juu ya sheria,hii kitu sio afya kama taifa sababu matukio kama yale yanaweza kufanywa tena na tena na mhusika akijua atalindwa kama alivyolindwa mwingine,tunatengeneza taifa la kijinga kwa vizazi vyetu vijavyo
Udhaifu wa jeshi letu la polisi ndio sababu ya watu kujichukulia sheria mkononi.

Mabadiliko katika jeshi la polisi yatakuwepo kama mwenye mamlaka ya kuteua mkuu wa mapolisi atachukizwa na utendaji wa polisi.
 
Mie nilisema tangu mwanzo humu jukwaani, hili tukio watu mmelichukulia kihisia tu, ila inawezekana binti na hao jamaa ni wameamua tu kujirekodi lakini hakuna tukio la ubakaji, yawezekana walifanya kwa makubaliano watu mkaja juuu. Haya tazameni sasa
 
FaizaFoxy weka neno hapa dada etu.
 
Muulize kamanda. Kwahiyo kahaba hana haki zake mana no kama vile anahalalisha kana kwamba kahaba kajitakia!
afande akili ndogo mno hapo anajisifu kwamba amemaliza utata wakati upumbavu wa wazi wazi
 
Kwa akili zako mkuu huyo raia atabaki salama kwa ushuhuda atakaoutoa!?
Au unataka kuponza uhai wa watu tu pasi na faida yeyote!?
 
Hhahahaha. Hili jeshi letu la polisi ama kweli kwa usanii limekithiri. Kumbe wakati wanasema wapewe muda wa kufanya uchunguzi wakati ushahidi ulikuwa wazi ndio wakati huo wameutumia kutupikia stori na kubadilisha kibao
 
Ni kama wavuta bangi
Ni kama anajiuza
Naona kuna "kama" mbili hapo.

Ni kama hawana uhakika wanavuta bangi au kama anajiuza.

Kunatakiwa kuziondoa hizo "kama"
Mahakamani.
na hapo kafanya upelelezi na hajui kapeleleza nini

hapo hapo watuhumiwa wamekamatwa na kuhojiwa na wakasema hawajatumwa

ila kitendo hakisemwi inasemwa ni kama wavuta bhangi, kama makahaba

ila ni suala la muda wataumbuka
 
video sijaiona.... ila nachoweza kusema na ambacho kipo sahihi kabisa hapo ni hakuna uchunguzi....wala kutafuta sababu ya kwanini walifanya uhalifu...wahukumiwe kutokana na matendo yao...kwa ushahidi wa video na mtendwa....majuto yao ni kama walilipwa au lah...majuto yaoni kumficha aliyewatuma kama yupo...nae ni muhalifu kama wao...
 
Kwa akili zako mkuu huyo raia atabaki salama kwa ushuhuda atakaoutoa!?
Au unataka kuponza uhai wa watu tu pasi na faida yeyote!?
sasa unababaika n kutia huruma kwanini, na kuna haja gani ya kuendelea kumfedhehesha kijana wa watu kwa kujdaili kwa hisia ambacho hatuwez kukithibitisha kwa vyombo husika vinavyo deal na kutoa haki kulingana na ushahidi?🐒
 
sasa unababaika n kutia huruma kwanini, na kuna haja gani ya kuendelea kumfedhehesha kijana wa watu kwa kujdaili kwa hisia ambacho hatuwez kukithibitisha kwa vyombo husika vinavyo deal na kutoa haki kulingana na ushahidi?🐒
Mkuu mambo yako wazi,ni kipi hakijaweza thibitishwa!??
Yani kaka unakua kama mgeni wa hii nchi.Kuwa kada wa CCM tumeshakukosa kaka,haukuwa hivi wewe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…