Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, David Misime, ameeleza kuwa Jeshi la Polisi limepiga marufuku maandamano yaliyoandaliwa na CHADEMA, ambayo yalikuwa yamepangwa kufanyika Septemba 23 katika jiji kuu la kibiashara, Dar es Salaam. Marufuku hiyo imetolewa kwa lengo la kudumisha amani na usalama wa wananchi.
Your browser is not able to display this video.
Misime aliongeza kwamba hatua hii imechukuliwa kwa sababu baadhi ya viongozi na wafuasi wa CHADEMA wamekuwa wakipanga mikakati ya kuchochea vurugu nchini, hali ambayo inaleta hatari kwa amani ya nchi. Alisema kuwa mara kadhaa serikali imeagiza kufanyika kwa uchunguzi ili kubaini walipo wanachama waliodaiwa kupotea, lakini baadhi ya watu wanaendelea kutoa mipango inayolenga kuharibu amani.
"Kwanini wanataka kututoa kwenye reli hatua za kiupelelezi zinazoendelea baada ya Rais Samia Suluhu kuagiza kufanyika kwa uchunguzi, mara kadhaa viongozi na wafuasi wamekuwa wakipanga na kuratibu mikakati mbalimbali na kutoa mipango yenye lengo la leta vurugu nchini ili kuharibu amani ya nchi yetu kwasababu zao wenyewe, kutokana na taarifa hiyo jeshi la polisi nchini limepiga marufuku kuacha kuendelea kuhamasisha kujihusisha katika uhalifu huo"
Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, David Misime amesema Jeshi hilo limepiga marufuku kufanyika kwa maandamano yaliyopangwa na CHADEMA, Septemba 23 katika jiji kuu la kibiashara, Dar es Salaam kuishinikiza Serikali kueleza walipo wanachama wao waliodaiwa kupotea, akisisitiza kuwa hatua hiyo imechukuliwa kwa ajili ya kudumisha amani na usalama wa wananchi.
Your browser is not able to display this video.
Amesema kuwa, baada ya Rais Samia kuelekeza vyombo vya usalama kuchunguza tukio la kutekwa na kuuawa kwa Ally Kibao, hakuna haja ya maandamano, na vyombo vya dola vinaendelea na uchunguzi kwa kina.
"Kwanini wanataka kututoa kwenye reli hatua za kiupelelezi zinazoendelea baada ya Rais Samia Suluhu kuagiza kufanyika kwa uchunguzi, mara kadhaa viongozi na wafuasi wamekuwa wakipanga na kuratibu mikakati mbalimbali na kutoa mipango yenye lengo la leta vurugu nchini ili kuharibu amani ya nchi yetu kwasababu zao wenyewe, kutokana na taarifa hiyo jeshi la polisi nchini limepiga marufuku kuacha kuendelea kuhamasisha kujihusisha katika uhalifu huo"
Ameonya kuwa hatua kali zitachukuliwa dhidi ya yeyote atakayekiuka agizo hilo.
Tamko la hovyo, warudishe vijana wetu kwanza. Halafu Chadema waje na mkakati mwingine, maandamano hayajawahi kuwa suluhisho kwenye jambo lolote nchi hii,watu wataumia tu na bado mambo yatabaki vile vile.
Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, David Misime amesema Jeshi hilo limepiga marufuku kufanyika kwa maandamano yaliyopangwa na CHADEMA, Septemba 23 katika jiji kuu la kibiashara...
Chadema watulize vishundu kwanza mamlaka zifanye kazi yake. Hata wangeandamana miezi mwisho wa siku ni haohao Polisi watakaotakiwa kutafuta na kukamata watuhumiwa na ni hizohizo Mahakama za Tanzania ambazo wanadai hawaziamini zitakazoshughulikia.
Sidhani kama tanzania ndio nchi ya kwanza au ya mwisho ambayo vyombo vya usalama vinaingilia siasa hii imejitokeza mara kwa mara.
Shida hapa ni upinzani wa hii nchi hauna upinzani wenye mvuto na ubunifu kwa wananchi wengi wanaona ni kama hakunaga upinzani.
Vyama vya upinzania hasa chadema fanyeni utafiti wa kina kwenye nchi nyingine duniani vyama vyao vilifanyaje na vilitumia mbinu gani kujikwamua dhidi ya vyombo vya usalama ambavyo vilikuwa vinaingilia siasa..
Surat An-Nisa (4:58):"Hakika Mwenyezi Mungu anakwamrisheni mzirejeshe amana kwa wenyewe, na mnapohukumu baina ya watu mhukumu kwa uadilifu. Hakika hiyo anayoikuonyeni Mwenyezi Mungu ni bora kabisa. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia (na) Mwenye kuona."Aya hii inaweka wazi wajibu wa watawala na viongozi kurudisha haki na amana kwa watu, na wanapohukumu baina ya watu, lazima wahukumu kwa uadilifu.Pia, kuna aya nyingine zinazoonyesha umuhimu wa uadilifu kwa jamii:
Surat Al-Maida (5:8):"Enyi mlioamini! Kuweni wasimamizi wa uadilifu kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, mtoapo ushahidi, wala chuki ya watu isikufanyeni kutokutenda haki. Tendeni haki; hiyo ndiyo iliyo karibu na uchamungu. Na mcheni Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ana habari za mnayoyatenda."
Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, David Misime, ameeleza kuwa Jeshi la Polisi limepiga marufuku maandamano yaliyoandaliwa na CHADEMA, ambayo yalikuwa yamepangwa kufanyika Septemba 23 katika jiji kuu la kibiashara, Dar es