Polisi yaruhusu maandamano ya Dr Slaa

Polisi yaruhusu maandamano ya Dr Slaa

Bobby,
Usijali sana huyu Mwiba ni mwenzetu katika hii crusade ya mikasa ya nchi yetu. Ila tu matumaini yake makubwa kawayaweka kwa Maalimu Seifu; sasa ukisema kinyume cha huyo yeye demokrasia humtoka!!

SLaa for presidency
 
Wala si jazba Mwiba kwani wewe hupo Bongo? Sorry, but this is very true, miaka ya nyuma nilikuwa niko very proud kutangaza utaifa wangu nikisafiri nje ya nchi lakini sasa nisipoulizwa hata sitaji utaifa wangu naona aibu sana. Nchi inaendeshwa kama nini sijuwi nakosa hata mfano. Can you imagine tuko na sheria za aina 2 sasa, za walalahoi na wenye nacho. Mwenye nacho anaweza kufanya lolote na chochote kisifanyike kwake. Waziri anaweza kufanya lolote hata rushwa iliyothibitishwa na still akaendelea kuwa waziri.Bunge linatoa azimio kwa serikali (Hosea na Mwanyika) hakuna chochote kinafanyika. Do we really have a government au usanii tu? Binafsi ninaona aibu kwelikweli kuwa mtz kwa sasa.

Hayo ni machache tu Mwiba the list goes on and on. So kipi kitamshinda Slaa hapo?

Bravo Bobby, sasa hivi ni aibu sana kwa mtanzania kutaja utaifa wake kwa sababu ya mambo ya aibu yanayoendelea ndani ya nchi. Wana JF tumuunge mkono Dr Slaa kwa sababu ya ujasiri wake wa kupambana na MAFISADI walio ndani ya Serikali na wasio ndani ya Serikali.
 
Mbona Slaa is better than Kikwete ,Mkapa and Mwinyi ,the only problem for him to get to Ikulu ni mwamko mdogo na uelewa mdogo wa wapiga kura hasa wa vijijini !!!

Hawezi kwenda Ikulu kama hajaenda Jela ,wala hajakumbana na vipigo vya Sultani CCM.

hebu tuone Slaa akitumia maneno ya ghadhabu mbele ya vipaza sauti na kusababisha waandishi kutetemeka vidole wanapoandika habari zake, Wakuu jemedari wa Serikali ya Sultani CCM ni Seifu peke yake, bado hajatokea kwa Tanzania ya leo na kama mnataka mkutano unogele basi tumieni karata ya CUF Simba wa Nyika Maalim Seif Sharif Hamadi ,hata akina Slaa wanamjua na kumheshimu sana tu ,sasa nyie magabachori ikiwa mnamwona amepotea na hafai itakuwa ni woga ndio unaowahangaisha.
Mnajua kama mnataka kaseti ya kideo a mkutano wenu ifike Ikulu mpeni nusu saa huyo Mpemba muone itakavyouzika ,na siku hiyo mwambieni asichane nywele hapo itakuwa ni moto tu ,wengine wanasema kama halewi anavuta ila nimuonavyo ni mtu wa dini sana ,ila nimewahi kumuona kwenye mkutano ikiwa ameweka matuta kwenye nywele na kweli macho yameiva na ndipo hapo husema mpaka waandishi huacha kuandika na kushika tama kwa jamaa anavyomwaga mboga na ugali wa Chama tawala.
 
Mwiba,
Tuache ushabiki nani ni nani; lakini kweli Slaa kawasha moto; na sasa hivi kweli ni zamu ya upinzani kukaa chonjo na kuchukua nchi kama mkiacha ubishi kama unaotaka kuuleta. Tangu mwaka 1995 Maalifu Seifu kashindwa kuchukua madaraka; ok; sababu unazo wewe kuwa CCM wana mbinu; ok, Maalimu Seifu angetoa mbinu zake pia. Ameshindwa 1995/2000/2005; unafikiri ataweza lini?

Sasa hivi lazima akubali na mwenzie Lipumba au the like; kuwa; wapangane na kuunda coalition kama ile rainbow ya kenya; pale juu wamweke Slaa, wa pili awe Maalim, labda kidogo mambo yanaweza kubadilika. Halafu kwa sasa hivi coalition imechelewa kwa vijijini kule inabidi wawe na muda wa kuwajua hawa coalition, otherwise huyo Sultani unayesema kila siku atazidi kutawala.
 
Mwiba sorry huenda sijakusoma vizuri hivi kwani JK ana nini cha kumzidi Dr. Slaa? Mbona mimi sikioni na the way nchi inavyoendeshwa kienyeji I even have a feeling kwamba mtu yeyote anaweza kuwa rahisi (rais) wa nchi hii though sikuwahi kufikiri hivyo kabla ya hii awamu ya kisanii.

Mkuu Bob hujamjua Mwiba, huyu Mwiba yeye ni CUF, Seif na Zanzibar tu. Hawezi kumuunga mkono yeyote zaidi ya hao watatu yaani chama CUF pekee, kiongozi Seif pekee na nchi Zanzibar no Muungano. kwa ujumla jamaa ni mbaguzi. Nawaunga mkono wananchi na CHADEMA wa Iringa kwa kuonyesha kwa vitendo support yao kwa Dr. Slaa na kupinga ufisadi na rushwa katika usambazaji na uuzaji wa mbolea. Watanzania wengine tuige na tusambaze ujumbe wa mabadiliko.
 
Mkuu Bob hujamjua Mwiba, huyu Mwiba yeye ni CUF, Seif na Zanzibar tu. Hawezi kumuunga mkono yeyote zaidi ya hao watatu yaani chama CUF pekee, kiongozi Seif pekee na nchi Zanzibar no Muungano. kwa ujumla jamaa ni mbaguzi. Nawaunga mkono wananchi na CHADEMA wa Iringa kwa kuonyesha kwa vitendo support yao kwa Dr. Slaa na kupinga ufisadi na rushwa katika usambazaji na uuzaji wa mbolea. Watanzania wengine tuige na tusambaze ujumbe wa mabadiliko.
NO, NO, MWIBA SI MBAGUZI, NI MAPENZI YAKE TU NA CHAMA CHAKE, KUPENDA KWAKE SI UBAGUZI ILA DEMOKRASIA IMTUMAVYO!!

Slaa for Presidency!
 
Kama sio kuwa mbali na Iringa ningekuwapo katika maandamano hayo tena nikiwa na bango lisemalo NI WAKATI WA KUIZIKA SISI MIJIZI. Watu wa Iringa wamefanya kitu natamani watanzania wote tungefanya kila siku tena hata kama Polisi wanazuia sisi tunaweza kuwaonyesha nguvu ya umma.
Enyi wananchi wa Iringa mmeonyesha njia. Ni wakati wa sisi wengine kuendesha the same thing kwenye mikoa mingine ili kuongeza nguvu kwenye hoja ya shujaa Dr Slaa.
 
All the best Dr. Slaa. I'm sure Iringa residence will never let you down. We're together
 
Watu wa mikoani ndipo hapo huwa wana nipa raha, yaani wao ni vitendo kwa kwenda mbele.
DSM sijui maraha yanatuzidia, ama maisha ni magumu sana? uelewa mwingi taarifa zote za tunavo ibiwa tunazo kuliko hata wa mikoani ila haaa... tupo kama vile hatupo!

BRAVO WAKAZI WOTE WA IRINGA
Hili ni jambo la kuigwa na wazalendo wote wa Tanzania, ina bidi kuunga mkono wapambanaji, hata hao wanao jidai kumzomea Slaa bungeni labda waishi huko huko DODOMA wakirudi mitaani kwetu tunao nasi tuwazomee, Wamerikologa inabidi walinywe wabinafsi wakubwa watetea matumbo yao! badala ya wananchi walio watuma kha!
 
Bobby,
Usijali sana huyu Mwiba ni mwenzetu katika hii crusade ya mikasa ya nchi yetu. Ila tu matumaini yake makubwa kawayaweka kwa Maalimu Seifu; sasa ukisema kinyume cha huyo yeye demokrasia humtoka!!

SLaa for presidency

mzee umechemka sana kwa mwiba. fuatilia posting zake za mwanzo utaona kabisa kuwa huyu ni ccm damu kabisa na ni watu wanaotumiwa kwani ghafla akapiga u turn na kujifanya eti ni cuf ili tu kupenyeza mambo yake. Huyu anajua kabisa kuwa huku bara cuf haina nguvu ila anaitumia kuisaidia chama chake.

kama hauamini tafuta post za mwiba 1-100 za kwanza halafu utaniambia. Watu hawa humu wamo wengi tu wengine utawaona wakija na viabari mbuzi wakidai ni watetezi wa wanyonge kumbe wana ajenda zao. Leo namtaja mmoja tu Gembe na yeye ni kama mwiba tu hakuna tofauti ni watumishi wa mafia wakiongozwa na baba yao anayejuana na viongozi!
 
Kama sio kuwa mbali na Iringa ningekuwapo katika maandamano hayo tena nikiwa na bango lisemalo NI WAKATI WA KUIZIKA SISI MIJIZI. Watu wa Iringa wamefanya kitu natamani watanzania wote tungefanya kila siku tena hata kama Polisi wanazuia sisi tunaweza kuwaonyesha nguvu ya umma.
Enyi wananchi wa Iringa mmeonyesha njia. Ni wakati wa sisi wengine kuendesha the same thing kwenye mikoa mingine ili kuongeza nguvu kwenye hoja ya shujaa Dr Slaa.
Kma itashindikana kuifanya hii iwe ajenda inayojitegemea, Chadema wanaweza kuiingiza kuwa sehemu ya operesheni sangara
 
Wapinzani wangeungana kwa nafasi ya urais asimame lipumba pekee labda itasaidiaaa....si kila kichama...kiwe kinataka kusimamisha rais tuuu
 
Ningekuwa jirani ningebeba bango kabisa!! Wizi hauwezi kuwa siri bana. Dr. Slaa you are our Hero, tunapigana sambamba katika vita hivi hauko peke yako.
 
Tumuunge mkono Mesimiwa Dr. Slaa, maana anachokifanya ni kwa ajili ya watanzania wote kama sio wengi, tusikamane sote kwa pamoja.

Karibu sana shemeji hapa JF ndo penyewe hapa.
Hivi punde nitakutambulisha kwa Masanilo.
Huko Zenji mnatunyima nini lakini.


Big up Dr.Slaa
 
Hawezi kwenda Ikulu kama hajaenda Jela ,wala hajakumbana na vipigo vya Sultani CCM.

hebu tuone Slaa akitumia maneno ya ghadhabu mbele ya vipaza sauti na kusababisha waandishi kutetemeka vidole wanapoandika habari zake, Wakuu jemedari wa Serikali ya Sultani CCM ni Seifu peke yake, bado hajatokea kwa Tanzania ya leo na kama mnataka mkutano unogele basi tumieni karata ya CUF Simba wa Nyika Maalim Seif Sharif Hamadi ,hata akina Slaa wanamjua na kumheshimu sana tu ,sasa nyie magabachori ikiwa mnamwona amepotea na hafai itakuwa ni woga ndio unaowahangaisha....
Mwiba,
Inawezekana Seif ni mzungumzaji mzuri, lakini kama umesoma vizuri ajenda za maandamano kwa " mujibu wa barua ambayo waombaji wameiwasilisha kwa kamanda wa polisi maandamano hayo yanataka mishahara na maslahi ya viongozi wote wa umma wenye nyadhifa za kisiasa yajulikane kwa wananchi kama alivyosema Dr Slaa." Seif ni mmoja wa viongozi hao wanaopokea marupurupu ya uongozi wa kisiasa, ambayo bado ni siri na ndio moja ya sababu za msingi wa maandamano hayo. Hivyo basi pamoja na uzuri wake wa kuzungumza, lakini hilo sio jukwaa lake kwani naye ni mmoja wa watuhumiwa.
 
Kwa wale walioko Iringa mjini, tafadhali je kuna lolote ambalo twaweza lisikia kutoka kwenu kuhusiana na yaliyojiri kwenye maandamanoo na haswa hotuba ya mpiganaji Dr. Slaa?
 
mzee umechemka sana kwa mwiba. fuatilia posting zake za mwanzo utaona kabisa kuwa huyu ni ccm damu kabisa na ni watu wanaotumiwa kwani ghafla akapiga u turn na kujifanya eti ni cuf ili tu kupenyeza mambo yake. Huyu anajua kabisa kuwa huku bara cuf haina nguvu ila anaitumia kuisaidia chama chake.

kama hauamini tafuta post za mwiba 1-100 za kwanza halafu utaniambia. Watu hawa humu wamo wengi tu wengine utawaona wakija na viabari mbuzi wakidai ni watetezi wa wanyonge kumbe wana ajenda zao. Leo namtaja mmoja tu Gembe na yeye ni kama mwiba tu hakuna tofauti ni watumishi wa mafia wakiongozwa na baba yao anayejuana na viongozi!
Ulichosema Shaom ni kweli,especially kuhusu Mwiba,nadhani aliyeifufua ile thread yake ya 2007 kuwa hakuna chama mbadala ndiye amemuumbua zaidi.
 
mzee umechemka sana kwa mwiba. fuatilia posting zake za mwanzo utaona kabisa kuwa huyu ni ccm damu kabisa na ni watu wanaotumiwa kwani ghafla akapiga u turn na kujifanya eti ni cuf ili tu kupenyeza mambo yake. Huyu anajua kabisa kuwa huku bara cuf haina nguvu ila anaitumia kuisaidia chama chake.

kama hauamini tafuta post za mwiba 1-100 za kwanza halafu utaniambia. Watu hawa humu wamo wengi tu wengine utawaona wakija na viabari mbuzi wakidai ni watetezi wa wanyonge kumbe wana ajenda zao. Leo namtaja mmoja tu Gembe na yeye ni kama mwiba tu hakuna tofauti ni watumishi wa mafia wakiongozwa na baba yao anayejuana na viongozi!

Mkuu naona umeamua kuwapa za uso. Safi sana huu ni ufisadi pia
 
Walioko Iringa tunaweza kupata matangazo ya moja kwa moja?
 
Maandamano yalianza saa 4, yalifika uwanjani saa 5. Hotuba zimetolewa mpaka saa 9. sasa wamemaliza. Kwa maelezo zaidi mpigie Mchungaji Msigwa

serayamajimbo
 
Back
Top Bottom