Polisi yawakamata watu 11 kwa kuwatapeli masista wa Kanisa la Katoliki Sh milioni 100

Polisi yawakamata watu 11 kwa kuwatapeli masista wa Kanisa la Katoliki Sh milioni 100

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
Jeshi la Polisi Kanda Maalum la Dar es Salaam limewakamata matapeli sugu wa viwanja kwa tuhuma za kujipatia Tsh. milioni 100 kwa njia ya udanganyifu, wakijifanya wanamiliki na kuuza viwanja vya makazi ambavyo siyo vyao.

Matukio waliyoyafanya yametokea kati ya mwezi Januari na Februari 2022.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salam, Muliro Jumanne amesema watuhumiwa hao 11 akiwemo mwanamke wamekamatwa maeneo ya Goba Kinondoni baada ya kuwatapeli Masista wa Kanisa Katoliki Shirika la Mabinti wa Mtakatifu Maria Kipalapala, Tabora.

Watuhumiwa hawa watafikishwa kwenye vyombo vingine vya kisheria kwa hatua zaidi. “Jeshi la Polisi linawaomba Wananchi waendelee kutoa taarifa mbalimbali ili zifanyiwe kazi na vitendo vya kihalifu viweze kupungua,” amesema Muliro.
 
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salam, Muliro Jumanne amesema watuhumiwa hao 11 akiwemo mwanamke wamekamatwa maeneo ya Goba Kinondoni baada ya kuwatapeli Masista wa Kanisa Katoliki Shirika la Mabinti wa Mtakatifu Maria Kipalapala, Tabora.
Hivi masista pamoja na kutoka kwenye kanisa lenye wasomi wengi walishindwa kwenda ofisi za serikali kuomba ardhi wakaamua kununua viwanja kwa matapeli!!
 
Sadaka jamani Mnaenda Tapeliwa tena. Mngempelekea Mungu jamani
Masista au watawa huwa hawaishi kwa sadaka yeyote. Na tena haziwahusu kabisa. Kila wanachotumia wanazalisha wenyewe.. Na wanapaswa kutoa msaada na huduma kwa maskini, yatima, wazee etc. Ndio Maana wanajikita sana sana kwenye uwekezaji na uzalishaji.
Hata kama sister ni daktari na ameajiriwa Serikalini mshahara wake hapokei yeye... Inaingia shirikani moja kwa moja.
 
Hivi masista pamoja na kutoka kwenye kanisa lenye wasomi wengi walishindwa kwenda ofisi za serikali kuomba ardhi wakaamua kununua viwanja kwa matapeli!!
Mambo ya michongo hupelekwa kimichongomichongo
 
Hivi masista pamoja na kutoka kwenye kanisa lenye wasomi wengi walishindwa kwenda ofisi za serikali kuomba ardhi wakaamua kununua viwanja kwa matapeli!!

Mtawala wa Dubai mwenyewe ametapeliwa juzi kati tu hapa na watu wenye ngozi nyeusi kwa kumuuzia madini feki! Sembuse hao Masista!

Linapokuja suala linalohusu UTAPELI, ngozi nyeusi wako vizuri sana. Kila siku zinagunduliwa mbinu mpya za kuwapiga watu.
 
Back
Top Bottom