Pompeo to make 1st trip to Africa in a bid to reassert US as a leading partner The secretary of state will visit Senegal, Angola and Ethiopia

Bila shaka Baba wa Taifa huko aliko anaposikia mambo kama haya, anajuta. Wakati wake, hakuna Kiongozi wa dunia ya kwanza angeweza kutembelea hizo nchi asiikanyage Tanzania.

Halafu tuna watu wanajaribu kulinganisha kichuguu na mlima. Pamoja na Mwalimu kupingana nao kwa hoja mbali mbali, walikuwa wanapigana vikumbo kuitembelea Tanzania kisiwa cha amani Afrika.

Siku hizi wanaikwepa Tanzania kama wanavyokwepa coronavirus. Kisiwa cha amani kimegeuka na kuwa uwanja wa fujo wa kutekana, kutesana na kutoana uhai. Hakika Baba wa Taifa anatoa machozi huko aliko!
 

Kwa Tanzania ilivyokuwa 2010 -2015, Pompeo lazima angetembelea Tanzania katika trip yake ya Kwanza Afrika. Lakini kwa sifa tuliyojijengea miaka mitano iliyopita, Tanzania haimo tena miongoni mwa nchi zinazoheshimika Afrika. Tumewekwa kundi moja na rogue nations. Najua kama Kenyatta asingekuwa Washington juzi tu, Pompeo angepita Kenya pia.

Tangu Rais Bill Clinton, George Bush, na Barack Obama, Tanzania ilitembelewa na Marais wote wa Marekani (bila kujali wanatoka R or D) kama progressive African nation.

Baada ya nchi kushikwa na '.........' tumerudishwa nyuma hatua kumi na kupoteza heshima kimataifa tulipokuwa tumefikia. Yaani sasa hata Secretary of State hawezi kukanyaga kwenye nchi yenye 'amani, utulivu na demokrasia?'

Yanayokuja yanatafakarisha.
 
Kumzuia Mmarekani kuja Tanzania ni sawa mtu akazuie wewe Pascal kwenda Kolomije. Sijui utakosa nini kwa kutokwenda!!

Mayalla, unanikumbusha hadithi ya 'sizitaki mbichi hizi'. Hivi Pompeo angekuja kumsifia Magu hapa ungeandika hivi?

FACT is Americans don't buy into the same stupid games we seem to tolerate here. And Magu will soon learn the lessons of good governance, albeit by force.
 

Ukweli mchungu, yaani watakubishia kwa hili ila ndio ukweli hapa Afrika hatuna jeuri ya kumsema Mmarekani.
 
Trump may host African leaders for a U.S.-Africa investment summit in Washington.

Je, inawezekana hata hii U.S.-Africa investment summit tusialikwe na hata tukialikwa tusihudhurie? Je msimamo wetu ni upi kuhusu hili?
 
Trump may host African leaders for a U.S.-Africa investment summit in Washington.

Je, inawezekana hata hii U.S.-Africa investment summit tusialikwe na hata tukialikwa tusihudhurie? Je msimamo wetu ni upi kuhusu hili?

Shida hua inakuja pale tunapokwenda huko then inakuja session ya Rais wa nchi husika kuhojiwa na waandishi wa habari,hapo hua ni majaribu bora tupotezee tu.

Ulishawahi kupata picha mkuu mwenyewe Vs The hard talk(BBC) au Mkuu vs amanpour(CNN)?
 
Baada ya huyu bwana kuizika Tanzania kidiplomasia, atakayefuata atakuwa na kazi kubwa sana kuisuka upya. Vinginevyo nchi ndivyo itakavyokuwa imejiunga kwenye vi-nchi visivyokuwa na 'influence' yoyote duniani.

Hata humu jirani tu, Afrika ya Mashariki, hatuna sauti tena. Ni nini tofauti yetu na Burundi kwa mfano, kimataifa.

Hivi kuna anayejua ni nini kilitokea kuhusu ile safari ya China iliyowahi kutangazwa kuwa inaandaliwa?

Isije ikawa wenyeji wetu waliamua kuiahirisha kwa sababu...mbalimbali, zikiwemo za kimaslahi yao waliyonyang'anywa, tena kwa makelele mengi tu!
 
Mwanzoni kabisa mwa utawala wa Magufuli, zile marufuku alizo tangaza. Jenerali ulimwengu aliweza kuziscan na kufanya hitimisho sahihi kabisa kwamba kwenye demokrasia "tumerudi nyuma miaka 100". Pro Magufuli walimshambulia kweli.....angalia sasa hivi kila kitu kipo wazi kabisa urudiji nyuma kidemokrasia upo wazi mno na kila mwenye akili huru anaona.
 
We twice hosted US president during JK's time. What has been their impact back then and probably now when we face a new challenge?
 
Hujaeleweka, umeandika Kama bata anaehakisha!! Eti china imejenge reli kutoka Pakistan hahahahaaaaah!
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwahiyo umezipima za kwako na Trump ukaona zako nzito? Pole sana!
Mwabie asinuse pua yake hata kidogo kwa jiji letu la dsm..

Note; kutembelewa na watu wenye Akili Kama kina pompeo Ni hatari Sana kwa Taifa lako. Bora utembelewe na watu wenye akili nyepesi Kama Trump. Pompeo kafie mbali aisee usiguse tz.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…