Pongezi: Asante kocha Zoran Maki kwa kuligundua jipu lililokuwa likiisumbua simba kwa muda mrefu, Jonas Mkude.

Pongezi: Asante kocha Zoran Maki kwa kuligundua jipu lililokuwa likiisumbua simba kwa muda mrefu, Jonas Mkude.

Tipstipstor

JF-Expert Member
Joined
Nov 29, 2021
Posts
1,528
Reaction score
3,352
Ahlanbik:

Kongole kwa kocha zoran maki kwa kupata ushindi wake wa kwanza katika ligi kuu ya NBC hapo nchini Tanzania dhidi ya Geita Gold. Pia pongezi nyingi kwake kwa kumtoa nje kabla ya kipindi cha kwanza kumalizika ,the so called "legend" ,Jonas Mkude.

Ni muda mrefu sasa mchezaji huyo mlevi asiyejituma uwanjani amekuwa akijiona kuwa ni untouchable katika kikosi cha simba kitendo kinachompelekea kucheza kifadha uwanjani.

Mkude amekuwa na uchezaji wa kizamani, uchezaji wa kidingi,kupoozesha mpira,kutokukimbia na kukaba kwa macho,vitendo vinavyochangia kuidhohofisha simba na kuifanya isifikie kilele cha mafanikio katika bara la Africa.

Zoran Maki amekuja na falsafa ya mpira wa kasi ambao ni mlima mrefu kwa kiungo mvivu mvivu kama Jonas Mkude. Zoran anahitaji kuona movements za wachezaji wake pindi wakiwa na mpira na wasipokuwa na mpira,kitendo ambacho amekuwa hakioni kwa mtu kama Jonas Mkude. Muda umefika sasa kwa mkude kuachana na simba na kwenda kwenye timu za chini kama Azam au Kmc.

Simba haihitaji aina ya viungo kobe, ambao ni wazito kukimbia wawapo na mpira ama wasipokuwa na mpira. Muda wa mabadiliko ndio huu.

Salamu zimfikie mshambuliaji namba nne wa klabu wa simba, Babu John Bocco na ndugu yake kutoka kigoma, Mzamiru Yasin. Wakati wenu wa kuendelea kuitumikia Simba umekwisha ,simba inahitaji mabadiliko.

Nikiripoti kutoka ktk jiji la Bergamo nchini Italy ni mimi mchambuzi wenu wa masuala ya soka, Tipstiptor.
 
Kocha msaidizi Matola naye VP aende au abaki?
He must go...kama simba wanahitaji mapinduzi ya kisoka basi wanahitaji kuwa na mfumo wa kisasa katika benchi la ufundi. Kikawaida kocha mpya anapopewa kazi ya kuifundisha timu basi yeye ndie huja na benchi lake la ufundi na pindi anapotimuliwa kazi basi benchi lake zima la ufundi hutimuliwa nalo. Kitendo cha simba kubana matumizi na kuamua kumpangia kocha mkuu watu wa kufanya nae kazi ni kosa kubwa na kinyume na uendeshaji wa kisasa wa timu. Ikiwa kama kocha atahitaji kuzungumza kiswahili na wachezaji wasiojua kiswahili basi ni vyema kwa klabu kuajiri mkalimani wa kuwafasiria wachezaji nini kocha anasema na hivi ndivyo inavyofanywa duniani kote.Mfano mzuri ni pale Marcelo Bielsa alipoajiriwa Leeds united, alikuwa hafahamu hata chembe ya kingereza zaidi ya yes na No tu. Ila Leeds iliajiri mkalimani akawa anatafsiri kile ambacho bielsa alikuwa akiwaambia wachezaji na kutokana na ubora wa kocha Bielsa, Leeda ilifanikiwa kupanda daraja na kurejea ligi kuu ya nchini uingereza.

Matola must be sacked kama simba inahitaji mabadiliko.
 
Ww jamaa ni mjinga tu na hujui ball. Ingekua geita wangekua imara kwenye kiungo alaf wakawa vizuri kwenye wings unadhan hapo hiyo sub ingelipa.

Mmeshasahau kilichomtokea Jumamosi. Alifanya hiyo sub ya kutoa kiungo na kilichotokea ikawa ni vilio kila kona.
 
Ahlanbik:

Kongole kwa kocha zoran maki kwa kupata ushindi wake wa kwanza katika ligi kuu ya NBC hapo nchini Tanzania dhidi ya Geita Gold. Pia pongezi nyingi kwake kwa kumtoa nje kabla ya kipindi cha kwanza kumalizika ,the so called "legend" ,Jonas Mkude.

Ni muda mrefu sasa mchezaji huyo mlevi asiyejituma uwanjani amekuwa akijiona kuwa ni untouchable katika kikosi cha simba kitendo kinachompelekea kucheza kifadha uwanjani.

Mkude amekuwa na uchezaji wa kizamani, uchezaji wa kidingi,kupoozesha mpira,kutokukimbia na kukaba kwa macho,vitendo vinavyochangia kuidhohofisha simba na kuifanya isifikie kilele cha mafanikio katika bara la Africa.

Zoran Maki amekuja na falsafa ya mpira wa kasi ambao ni mlima mrefu kwa kiungo mvivu mvivu kama Jonas Mkude. Zoran anahitaji kuona movements za wachezaji wake pindi wakiwa na mpira na wasipokuwa na mpira,kitendo ambacho amekuwa hakioni kwa mtu kama Jonas Mkude. Muda umefika sasa kwa mkude kuachana na simba na kwenda kwenye timu za chini kama Azam au Kmc.

Simba haihitaji aina ya viungo kobe, ambao ni wazito kukimbia wawapo na mpira ama wasipokuwa na mpira. Muda wa mabadiliko ndio huu.

Salamu zimfikie mshambuliaji namba nne wa klabu wa simba, Babu John Bocco na ndugu yake kutoka kigoma, Mzamiru Yasin. Wakati wenu wa kuendelea kuitumikia Simba umekwisha ,simba inahitaji mabadiliko.

Nikiripoti kutoka ktk jiji la Bergamo nchini Italy ni mimi mchambuzi wenu wa masuala ya soka, Tipstiptor.
Ps4 kuna timu inaitwa Bergamo kule italy ni hatari
Kweli mkude na mzamiru ni viungo wa madaraja ya chini
 
Nafikiri wewe ndio mjinga na ujifunze mpira, Mkude leo alikuwa anapoteza pasi tena zile za nyuma,muda mwingi alikuwa anacheza kama inside 10 mpaka chama Kuna muda alikuwa anacheza nyuma ya mkude.Kifupi leo mkude nafikiri alikuwa amelewa.Simba inahitaji kiungo anaejua kukaba na kuiunganisha tm
Ww jamaa ni mjinga tu na hujui ball. Ingekua geita wangekua imara kwenye kiungo alaf wakawa vizuri kwenye wings unadhan hapo hiyo sub ingelipa.

Mmeshasahau kilichomtokea Jumamosi. Alifanya hiyo sub ya kutoa kiungo na kilichotokea ikawa ni vilio kila kona.
 
Ww jamaa ni mjinga tu na hujui ball. Ingekua geita wangekua imara kwenye kiungo alaf wakawa vizuri kwenye wings unadhan hapo hiyo sub ingelipa.

Mmeshasahau kilichomtokea Jumamosi. Alifanya hiyo sub ya kutoa kiungo na kilichotokea ikawa ni vilio kila kona.
Siwezi kubishana na mtu ambae huna hata class F coaching licence, utanambia nini kuhusu football we nyang'au???!!!
 
Mkude, Ajibu, na Ndemla. Ni wachezaji wenye vipaji vikubwa kilicho wadumaza na uvivu wa mazoezi na ufadha.
Mwangalieni Shabalala, ni kizazi kimoja ila yeye anajituma na bidii ya mazoezi.
Muongeze na Chama kwenye hilo kundi la mafadha
 
Kwa upande wangu nakubaliana na wengi hapa kuhusu Mkude kuwa mvivu uwanjani, hana kasi uwanjani, kukaba kwa macho na hawezi hata kupiga "penetration pass" kuvunja ukuta wa viungo wa timu pinzani hata mara moja kwa dakika zote tisini. Lakini kwa Muzamiru sitaona aibu kumtetea kabisa. Muzamiru anajituma muda wote wa mchezo, anapora mipira kwa adui na hachoki kupambania timu lakini mapungufu yake makubwa mawili ni upigaji wa pasi sahihi na kigugumizi miguuni mwake.
 
Kwa upande wangu nakubaliana na wengi hapa kuhusu Mkude kuwa mvivu uwanjani, hana kasi uwanjani, kukaba kwa macho na hawezi hata kupiga "penetration pass" kuvunja ukuta wa viungo wa timu pinzani hata mara moja kwa dakika zote tisini. Lakini kwa Muzamiru sitaona aibu kumtetea kabisa. Muzamiru anajituma muda wote wa mchezo, anapora mipira kwa adui na hachoki kupambania timu lakini mapungufu yake makubwa mawili ni upigaji wa pasi sahihi na kigugumizi miguuni mwake.
Mkude kalewa misifa mingi - ni kweli binafsi namkubali sana Mzamiru.
 
Mi nashangaa watu ndo wanaanza kuona mapungufu ya Mkude leo. Wakati ndo mchezo wake miaka yote. Yaani ukitaka mkude ang'ae ni mpaka umpange na mtu wa kumkabia. Sasa hiyo biashara nani anataka! Yaani yeye ni asimame tu katikati ya uwanja, apige pass huku apige pass kule.. Basi! Tunaweka mtu ambae hana mchango wowote kwenye timu. Mi muda aende sasa
 
Back
Top Bottom