Pongezi kwa Mkenya aliyemwandikia Raila hotuba hii

Hiyo sio makala (documentary) hiyo ni hotuba (speech) pia insha (dictation) inafundishwa elementary schools nyie mpaka chuo mnajifunza insha?
 

nilitumia jina lako ili kuchangamsha mjadala.najua sie wewe uliyeandika.

vyovyote iwavyo,aliyeandika kama ni mkenya,basi anahitaji pongezi,hakika kajitahidi sana.

kuhusu wakenya kupata ajira ya kufundisha kiswahili nje ya kenya,nisemehe tu kwamba wanaopata au waliopata,haijawa hivyo kwa kuwa wanajuwa sana kiswahili, la hasha.ni kwasababu ya kuchangamkia fursa.bado watanzania wanajua sana kiswahili(cha kitaaluma,cha kuandika na cha kuzungumza) zaidi yenu.

fahamu tu kwamba wapo watanzania wanaofundisha kiswahili katika vyuo mbalimbali ughaibuni.
 
Hiyo sio makala (documentary) hiyo ni hotuba (speech) pia insha (dictation) inafundishwa elementary schools nyie mpaka chuo mnajifunza insha?

Kajifunze Kiswahili halafu uje upya
makala
Kiswahili[hariri]
Nomino[hariri]
makala
  1. maandishi katika gazeti
Tafsiri[hariri]
Halafu Insha (utungaji) inafundishwa hadi chuo kikuu japo kuanzia sekondari huwa inabadilishwa na kuitwa fasihi.
 
Nakuona katika ubora wako, japo hii post yako inataka kutuhamishia mada kidogo!

Hao wakenya wanaofundisha ughaibuni wamepata hiyo kazi kwa kuwa kiswahili ni ni lugha ya eneo la maziwa makuu! Ndo maana hata watanzania wapo wengi sana kwenye vyuo na redio au taasisi nyingine za kiswahili ughaibuni!


Lakini yote hayo ni tisa, kumi kama unataka kiswahili fasaha lazima uje tz, kama ambavyo ukitaka kiingereza fasaha Africa unaenda uganda!
 

Kaka ili uajiriwe kwenye kazi yoyote ile, huwa kuna mahojiano ili kubaini uwezo na ujuzi wako wa kuifanya ile kazi, asili ya unakotoka huwa haijalishi sana, hata kama nchi yako inatumia lugha ya Kiswahili muda wote, sio kigezo au kiashirio tosha kwamba nyote mko sawa kwenye Kiswahili cha uandishi.
Kwanza humu JF ukiingia na kupitipitia bango zenu, nyingi huwa majanga kiuandishi.
 
Nimesema kuhusu eneo kinakoongelewa kiswahili sio kama kigezo cha ajira bali kama fursa!

Kama alivyosema kadoda, uwepo wa wakenya kule kwa kipindi cha mwanzoni sio kwa sababu ya kuongea kiswahili fasaha, ni kwa sababu ya kuchangamkia fursa.

Kuhusu uandishi wa humu JF ni kuwa content kama hizo zinaonekana kwenye nyuzi ambazo watu huchangia kimzaha mzaha!

Mtu anapofanya mambo kimzaha ni dhahili hajikiti kwenye ubora wa kile anachokiandika ila anataka tu kufikisha maana ya kile anachokusudia!
 
kweli uyu aliyeandika ni MTZ kabisaaa hakuna mkenya anaandika ivi wana words zao zinazowatofautisha na sisi hata maprofesa wa kiswahili Kenya haandiki ivi
 
Kadoda11 na MK254,
MK254 ina mpasa kuishukuru sana Jamiiforums kwa kumpiga ''msasa'' jinsi ya kuwasiliana nasi kwa kutumia Kiswahili safi kiasi cha RAO Raila Amolo Odinga a.k.a Baba kuweza ''kumtumia'' kwa imani kubwa ili kuwasiliana na Wana-Kenya katika kampeni za kuelekea uchaguzi mkuu Agosti 8, 2017.
 
MK254 anakula tu pesa ya mzee raila kimya kimya bila hata kuwakumbuka wabongo walimfunza kiswahili.

maisha haya usije ukamdharau mtu aisee.sitoshangaa akikabidhiwa kitengo cha mawasiliano kwa umma cha ikulu ya kenya endapo baba akishinda urais.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…