Msemakweli TZ
Member
- Oct 5, 2022
- 7
- 0
Nikiwa mdau wa benki hii natoa pongezi za dhati kwa Uongozi wa benki Dr. Edwin Mhede - Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi na Prof. Ruth Zaipuna (Mrs)- Mkurugenzi Mtendaji kwa kitendo cha kuyapokea maoni na ushauri na hatimaye kufanikisha kumwadabisha Lilian Komwihangiro (Advocate) aliyekuwa katibu wa benki na mkuu wa idara ya sheria.
Sina budi kuwapa pongezi za dhati kwani kitendo cha kusimama katika ukweli na haki bila ya kuficha maovu yake kinazidi kuiweka taasisi katika hali nzuri kuelekea kwenye mafanikio zaidi.
Hivyo basi msiache kufanyia kazi maoni na ushauri mwingine mtakaoupata ili kuendelea kuboresha benki hii imara hapa nchini.
Nashauri kwa uwazi na ukweli kwa kuwa hiyo nafasi ni nyeti na kiungo kati ya wadau, uongozi tendaji na uongozi wa bodi, nafasi hiyo itangazwe ndani ya benki na nje ili apatikane mtu POTENTIAL ambaye ataweza kusimamia maslahi ya kila upande, kwani kitendo cha kuendelea kuiacha wazi kinaweza kudhorotesha na kupunguza ufanisi wa benki kwa ujumla na mapana yake.
Nawasilisha.
Sina budi kuwapa pongezi za dhati kwani kitendo cha kusimama katika ukweli na haki bila ya kuficha maovu yake kinazidi kuiweka taasisi katika hali nzuri kuelekea kwenye mafanikio zaidi.
Hivyo basi msiache kufanyia kazi maoni na ushauri mwingine mtakaoupata ili kuendelea kuboresha benki hii imara hapa nchini.
Nashauri kwa uwazi na ukweli kwa kuwa hiyo nafasi ni nyeti na kiungo kati ya wadau, uongozi tendaji na uongozi wa bodi, nafasi hiyo itangazwe ndani ya benki na nje ili apatikane mtu POTENTIAL ambaye ataweza kusimamia maslahi ya kila upande, kwani kitendo cha kuendelea kuiacha wazi kinaweza kudhorotesha na kupunguza ufanisi wa benki kwa ujumla na mapana yake.
Nawasilisha.