Pongezi kwenu Single Mothers
Inapendeza... Kila la kheri...

Hiyo inaitwa usitukane mamba... wakati bado hujavuka mto...


Cc: mahondaw
 
Hujiulizi alivyo kuwa mwepesi kwako hatakuwa na mwepesi kwa wengine. Singe maza wanafaa kama huna uwezo wa kupata wanawake wa kawaida.
 
Habari za saa hizi Wanajamvi.

Leo kuna jambo fulani nataka kushare nanyi, jambo ambalo huenda mnalifahamu au hamlifahamu lakini kwa vyovyote najua kwa mjadala huu mtafahamu zaidi.

Tunatofautiana mitazamo. Kuna mitazamo tofauti tofauti kuelekea swala la kuoa Singo maza (naomba nitohoe najua inapaswa kuwa 'Single mother' ila sipendi kuchanganya lugha).

Kuna watu tumejizatiti hatutaoa singo maza ila hii kitu ni rahisi zaidi kuzungumza kuliko kuweka katika matendo. Kwanini ?

Mara nyingi kumpenda mtu hutokea bila hiari. Bila kuamua na kupatanisha maamuzi yako na mtazamo wako hiyo ndiyo sababu baadhi yetu tumejikuta tukienda kinyume na mitazamo yetu linapokuja swala la kuoa singo maza.

Acha nieleze jinsi nilivyozama kwa Singo Maza na kujikuta napuuza mtazamo wangu.

Mwishoni mwa mwezi wa tisa nilipewa mwaliko wa kuhudhuria sherehe za harusi fulani ya swahiba wangu sana.
Ilikuwa siku ya Jumamos usiku wa hiyo sherehe, wakati sherehe inaendelea na sisi (mimi na kampani fulani ya rafiki yetu) tumekaa kwenye meza ile kwenye meza jirani palikuwa na msichana fulani. Mweupee, mzuri kweli kweli, shape kama la Wema Sepetu. Nilipomuona nikamstua nikampa hi kisha nikakausha maana niliamini sio hadhi yangu ile . Najijua life langu 'dongotee' kula kwa kuunga unga na mishe ziende vizuri ndo nivae. Watoto wazuri kama wale wanataka matunzo.





Basi nikiwa naendelea kushusha bia, nikapaliwa. Bia ikanimwagikia kwenye shati. Shati likachafuka, miongoni mwa watu waliniona hili likitokea ni yule mrembo, rafiki zangu walipoona hili walinicheka sana ila yule mrembo (acha nimwite Asha) aliinuka alipokuwa na kunifata akanipa pole akatoa kitambaa chake akanipa nijifute. Nikakataa akanibembeleza nikaona sooo nikachukua ila sikujifutia chake niliinuka nikaenda msalani. Ila mpaka hapo akawa amenigusa kwa kiasi fulani nikaanza kumuona wife material.

Niliporudi nikamuomba namba akanipa. Niliporudi home nilimpigia simu aiseee! tulizungumza mpaka asubuhi, akanambia anaomba alale nikamuacha ila nikamuomba tukutane siku hiyo hiyo (jumapili) akasema sawa tutakutana jioni. Kweli jioni hiyo tukaweza kukutana maeneo fulani hivi ya ubungo tukaenda Bar fulani hivi. Kwanza kujiamini kuliniisha maana toto zuri vile linakubali appointment na mie tena sehemu km ile ila nikajikaza mpaka nikafanikiwa kumtongoza.

Hakukataa wala hakunambia chochote ila akasema ntakujibu siku nyingine. Nikaona 'Sawa.' mazungumzo yakaendelea ila sasa katika mazungumzo yake alikuwa mwepesi sana kusema maneno fulani yakuonesha kuwa yeye ni mtu wa dini. Lakini pia alikuwa mwenye ushauri chanya sana na kuonesha uzoefu mkubwa wa maisha jambo ambalo lilinifanya nione huyu ni 'wife material.' Istoshe hakuaguza pombe wala soda ila maji tu na akanambia atalipia yeye, nikasema mke si ndo huyu sasa.
Baada ya kama wiki moja hivi toka tuanze kuwasiliana mahusiano yakawa yameanza rasmi na kwakuwa nilishazama na KUDATA kwake sana nikaona sasa ni wasaa rasmi wa kupanga maswala ya harusi maana ni wife material haswa: hana lawama, hana mizinga, ata ukimwambia njoo saa nane usiku anaweza akaja, mshauri mzuri na mzoefu sana wa maisha istoshe ni MZURI MNO wa muonekano mpaka shape yaani kama ya wema.

Waswahili wanasema usione vyaelea vimeundwa, tukiwa katika mazungumzo akanambia kuna kitu nataka nikwambie, nikamwambia niambie, basi nilijua anaomba hela(maana hivyo ndivyo nnavowajua wanawake kwa uzoefu wangu) kumbe na tofauti kabisa na hilo. "Mimi nna mtoto," unasemaje ? niliuliza "Nna mtoto ana miaka mitatu, Nimeona bora nikwambie mapema kabla hatujaingia kwenye ndoa".

Sasa ndo tunarudi kwenye mada hii, unaweza kuwa na mtazamo fulani kuhusu wanawake wenye watoto, kwamba labda hutooa mwanamke mwenye mtoto katika maisha yako lakini mi nakwambia mwanaume mwenzangu unasema hivyo kwa sababu hujawai PENDA mwanamke mwenye mtoto.
Mimi nilikuwa na mtazamo huo huo lakini mpaka kufikia hatua hii ambayo nimependa kiasi hiki, mtazamo wangu nauona wa Kipumbavu sana, najiuliza kwanini nilikuwa naona si vizuri kuoa mwanamke mwenye mtoto ? Hapa saa hizi nawaza namna maisha yatakavyokuwa nitakapokuwa na familia yangu mpya na mtoto wa nyongeza, nna mtazamo mzuri sana kuelekea singo maza wangu na nataka nimpende mwanae kama mwanangu wa kumzaa kwa sababu sasa nimebaini nguvu ya upendo.

Kama hupendi kuoa singo maza sawa huo ni mtazamo wako, ila Mtazamo wako waweza badilika siku moja ukikutana na mwanamke utakaempenda kweli kweli kama mimi ilivonitokea kwahiyo nikushauri usiseme wala kukashifu watu waliooa masingo maza kama hujui nguvu ya upendo, huenda nawe ukajikuta katika njia hii hii.

Singo maza wote jamani nyie watu mna mbinu sana maana leo nimejikuta nakana nilichokishikilia kwa mda mrefu.

Mnisamehe wote niliowakwaza kwa kushea swala hili lililonikuta kwa kweli acha tu nikiri kuwa nimedata, na nimebadili mtazamo wangu.

Ila ushauri kwa wanaume wenzangu, usikashifu wala usiweke itikadi ya SITAOA singo maza, maana utajikuta unakana mtazamo wa kukolea kwa singo maza fulani, hii imenitokea kama mipango itakwenda vizuri basi tutaalikana kwenye harusi.

Mnisamehe kwa kuandika maneno meengi. Karibuni kwa mchango wenu.
Kuna facts ambazo zipo wazi;

1 . Uwepo wa huyo mtoto ni changamoto kwenye uhusiano mpya ( hili hutaliona sasa ) kuna legal and social implications
2. Wewe si Baba Mzazi wa huyo mtoto na kamwe hutakuwa Baba kwa huyo mtoto, haijalishi utatumia muda na pesa kiasi gani kwenye malezi ya huyo mtoto

3. Uhusiano wako na huyo mama automatically utakufanya mtoto akuzoee na kukuchukulia kama baba, hii itajenga bonding kati yako na mtoto ila kumbuka kinachowaunganisha ni mapenzi yako na huyo mama, siku ikitokea uhusiano wenu ukivunjika hutakuwa na namna ya kuwa tena karibu na huyo mtoto haijalishi utakuwa umemzoea na kumpenda kiasi gani , hii itamuathiri sana huyo mtoto kisaikolojia

4. Kama baba mzazi wa huyo mtoto yupo hai itazidisha ugumu kwenye mahusiano unayotaka kuanzisha, kumbuka kisheria huyo baba ana haki zote za kumuona na kumhudumia mtoto kama akiamua kufanya hivyo hutaweza kumzuia kisheria!

5. Utapata wakati mgumu sana kwenye kumlea huyo mtoto haswa kwenye kumuadhibu atakapokosea, ipo siku mama yake atakuambia MWACHE MTOTO WANGU, hutakuwa na la kufanya maana huyo SI MTOTO WAKO

6. Omba / sali sana huyo mtoto akikua na kuanza kujitambua aendelee kukuheshimu, huwa inatokea akishajua wewe si baba yake mzazi atakutamkia hivyo haswa akifika umri wa balehe hutakuwa na mamlaka ya kumuadhibu
 
Ni kweli si neno zuri hata kidogo. Pia tuwe wastaarabu na wenye kujiheshimu kwa kutowazalilisha wanawake wote wenye kulea watoto bila baba wa watoto(bila mzazi mwenzake).
Heshima inaanzia kwa kwako kujitambua na kujiheshimu, kwa mawazo yako, na maneno yako unayoyatamka au kuyaandika, au kuyaongea.
Huko ndiyo kunatwa kuwa na "utu".

Jina au neno "single mother " nashauri lisitumike, Bali jina la mhusika itapendeza zaidi na kuleta heshima kwa kila mmoja wetu.
Sidhani kama single mother ni jina ama tusi. Tena neno hili sio la kibongo na halijaanzia huku, nashauri njia pekee kuliepuka ni kuacha kuza nje ya ndoa.
 
Siku zote mwanzo wa penzi huwa kuna raha sana unaweza jihisi upo peponi. Na hapa kuna baadhi walibadili dini, wengine waligombana mpaka na wazazi wao. Usije ukafiri siku zote ndiyo itakuwa hivyo. Ndoa za siku nyingi zinavunjika sana sababu wengi wanafikiri ndoa ni ngono na kuambiana i love you. kuna single mother wapo wazuri sana na wengine pasua vichwa
HONGERA KWA MKE NA KWA ZAWADI YA MTOTO. BUY ONE, GET ONE FREE
 
Wala usitetereke na comments za humu..

Nimeona watu wanaingia ndoa ya pili au ya tatu na watoto wao,tena watoto wanajua kabisa huyu ni step dad/mom na wana share malezi,hivyo sioni ugumu wa single mothers kuwa na uhusiano,for any relatiship kitu important ni Chemistry ama Compatibility..ukipata mtu ana great personality anakufanya uwe na furaha then kuwa nae, mtoto chukulia kama ndugu tu wa mkeo,kama unaheshimu na kuwajali ndugu wa mkeo then tatizo liko wapi ukimjali mtoto wa mkeo?
 
Mwaya Mungu awalinde mfikie malengo. Wangekuwa wazungu hapa ungepewa hongera Ila kwa kuwa umeleta swala lako kwa wachawi wasiopenda furaha za watu a.k.a wabongo utakatishwa tamaa wee. Kwani single mother Hana K?? Hana ubongo?? Watu daily wanatoa mimba ili wasionekane wamezaa na tunawajua. Sasa hao Ndio bora? Mwaya km unaona umependa oaa
 
Kuna facts ambazo zipo wazi;

1 . Uwepo wa huyo mtoto ni changamoto kwenye uhusiano mpya ( hili hutaliona sasa ) kuna legal and social implications
2. Wewe si Baba Mzazi wa huyo mtoto na kamwe hutakuwa Baba kwa huyo mtoto, haijalishi utatumia muda na pesa kiasi gani kwenye malezi ya huyo mtoto

3. Uhusiano wako na huyo mama automatically utakufanya mtoto akuzoee na kukuchukulia kama baba, hii itajenga bonding kati yako na mtoto ila kumbuka kinachowaunganisha ni mapenzi yako na huyo mama, siku ikitokea uhusiano wenu ukivunjika hutakuwa na namna ya kuwa tena karibu na huyo mtoto haijalishi utakuwa umemzoea na kumpenda kiasi gani , hii itamuathiri sana huyo mtoto kisaikolojia

4. Kama baba mzazi wa huyo mtoto yupo hai itazidisha ugumu kwenye mahusiano unayotaka kuanzisha, kumbuka kisheria huyo baba ana haki zote za kumuona na kumhudumia mtoto kama akiamua kufanya hivyo hutaweza kumzuia kisheria!

5. Utapata wakati mgumu sana kwenye kumlea huyo mtoto haswa kwenye kumuadhibu atakapokosea, ipo siku mama yake atakuambia MWACHE MTOTO WANGU, hutakuwa na la kufanya maana huyo SI MTOTO WAKO

6. Omba / sali sana huyo mtoto akikua na kuanza kujitambua aendelee kukuheshimu, huwa inatokea akishajua wewe si baba yake mzazi atakutamkia hivyo haswa akifika umri wa balehe hutakuwa na mamlaka ya kumuadhibu

Mbona unamtabiria negative?? Why usimtabirie positive??
 
Huyo aliyemzalisha akamwacha ana akili kweli? Kumwacha mdada mzuri hvyo..beautiful with brain
 
Ahsante sana, ila wiki tu unatangaza ndoa? OK all the best
....Hapo ndio nami pamenishitua Mkuu.
Wiki tu baada ya kufahamiana na bibie ndugu yetu anaona aanze kuzungumzia Mambo ya Ndoa??
WIKI??? [emoji15][emoji15][emoji15]
 
Yote hayo ndani ya mwezi.. Karibu mjini mkuu!
 
Back
Top Bottom