Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Wasalamu wana Jukwaa!
Nianze kwanza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa Rehma zake na kutuvusha katika janga zito.
Sasa nijielekeze moja kwa moja kwenye hoja yangu. Hoja inahusu Moyo wa dhati wa Mh. Rais kuboresha Utumishi wa Umma kwa kuhimiza kutokuwa na TAMAA YA VYEO KWA WATUMISHI WA UMMA.
Mwanzo mwanzo wakati akiliongelea hili niliona Kama Ni utani ukizingatia tuliwahi kuwa na wabunge ambao ni Mkuu wa Wilaya, na Muda huo huo amepewa kukaimu ukuu wa Mkoa. Ilikuwa ni mtu mmoja vyeo 4 hadi vi4.
Leo ameweka bayana kuwa Kama unaenda jimboni basi achia nafasi uliyonayo. Leo amesema wanaoenda jimboni waachie nafasi zao. Na wanaoomba ruhusa nafasi zao zimechukuliwa. HILI NI JIPYA NA KUBWA KATIKA UTUMISHI WA WILAYA
Sasa basi Mawaziri Nao waige jambo hili jema, Mnao wakurugenzi katika maeneo yenu ya Taasisi zenu. Watanzania wako wengi na wanaweza kutimiza majukumu yao. Tuwape nafasi. TENDENI KAMA RAIS MAGUFULI KATIKA NAFASI ZENU.
Wanaoenda majimboni waende, Ofisi wapewe wasio na nia za siasa ili wamsaidie Mh. Rais.
Mashirika ya Umma, Wakala za Serikali, na Mamlaka kadhaa wako watu. Kipindi hiki Cha Uchaguzi kinahitaji utendaji uendeleee.
Pongezi Mh. Rais kuboresha Utumishi wa Umma
Umetumia lugha ya upole sana, sema kabisa imejaa wajinga wengi sana.Ccm imejaza vilaza wengi sana.
Hajaboresha utumishi wa umma bali amechoka kutengua na kuteua sasa anataka kutumia fursa ya kujaza nafasi zitakazoachwa na watumishi wa umma watakaochaguliwa nafasi za kisiasa. Kabla ya uchaguzi atakuwa na kazi nyingi za kuteua MaDC, MaRC, MaDED na wengine kujaza nafasi zitakazoachwa na wenye nafasi hizo sasa watakopoomba kugombea ubunge wa Bunge dhaifu wakiamini litabaki kuwa hivyo maana wanajua Ndugai dhaifu atarudi Bungeni kwa mbinu zilezile za rungu au kali (hengo) zaidi. Watumishi namna hiyo ambao hawatachaguliwa watapewa uteuzi mwingine hawataweza kuachwa tu bila kipato kwa kuwa ni makada wa Chama Tawala. Baada ya uchaguzi hali itakuwa mbaya zaidi kama CCM itabaki madarakani maana kutakuwa na Serkali dhaifu zaidi, Bunge ndiyoooo hata Mahakamà itakuwa Idara ya Serkali mihimili yote mitatu itakuwa kwenye mhula wa lala salama wa kulimbikiza mali na kusifiana.Wasalamu wana Jukwaa!
Nianze kwanza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa Rehma zake na kutuvusha katika janga zito.
Sasa nijielekeze moja kwa moja kwenye hoja yangu. Hoja inahusu Moyo wa dhati wa Mh. Rais kuboresha Utumishi wa Umma kwa kuhimiza kutokuwa na TAMAA YA VYEO KWA WATUMISHI WA UMMA.
Mwanzo mwanzo wakati akiliongelea hili niliona Kama Ni utani ukizingatia tuliwahi kuwa na wabunge ambao ni Mkuu wa Wilaya, na Muda huo huo amepewa kukaimu ukuu wa Mkoa. Ilikuwa ni mtu mmoja vyeo 4 hadi vi4.
Leo ameweka bayana kuwa Kama unaenda jimboni basi achia nafasi uliyonayo. Leo amesema wanaoenda jimboni waachie nafasi zao. Na wanaoomba ruhusa nafasi zao zimechukuliwa. HILI NI JIPYA NA KUBWA KATIKA UTUMISHI WA WILAYA
Sasa basi Mawaziri Nao waige jambo hili jema, Mnao wakurugenzi katika maeneo yenu ya Taasisi zenu. Watanzania wako wengi na wanaweza kutimiza majukumu yao. Tuwape nafasi. TENDENI KAMA RAIS MAGUFULI KATIKA NAFASI ZENU.
Wanaoenda majimboni waende, Ofisi wapewe wasio na nia za siasa ili wamsaidie Mh. Rais.
Mashirika ya Umma, Wakala za Serikali, na Mamlaka kadhaa wako watu. Kipindi hiki Cha Uchaguzi kinahitaji utendaji uendeleee.
Pongezi Mh. Rais kuboresha Utumishi wa Umma
We hujui kusoma trends za siasa nenda kalewe Bar usubiri October utapata majibuUroho safari hii hauna nafasi .Watu walikuwa wakikaa maofisini wanawaza siasa tu na kutia Nia kazi haziendi simu mtu anaongea kutwa na kamati zake za fitna wapambe wake ili ateuliwe ugombea
Sasa ni kusuka au kunyoa kagombee ila ofisi uachie wengine wachukue na usirudi Tena yakikushinda utajijua
Mimi sisomi trend nasikiliza kauli ya Raisi Magufuli ninayemuamini hayo ma trend kayasome mwenyeweWe hujui kusoma trends za siasa nenda kalewe Bar usubiri October utapata majibu
KabisaUroho safari hii hauna nafasi .Watu walikuwa wakikaa maofisini wanawaza siasa tu na kutia Nia kazi haziendi simu mtu anaongea kutwa na kamati zake za fitna wapambe wake ili ateuliwe ugombea
Sasa ni kusuka au kunyoa kagombee ila ofisi uachie wengine wachukue na usirudi Tena yakikushinda utajijua