Pongezi Rais Magufuli na Awamu Yake ya Tano, Wafanya Maajabu Vita Dhidi ya Umasikini, Tanzania Yaongoza Dunia Kupunguza Umasikini Uliotopea-WB.

Pongezi Rais Magufuli na Awamu Yake ya Tano, Wafanya Maajabu Vita Dhidi ya Umasikini, Tanzania Yaongoza Dunia Kupunguza Umasikini Uliotopea-WB.

Paschal, waandishi wa habari wenzako wanatekwa na kubambikiwa kesi za utakatishaji fedha na uhujumu uchumi.Wewe umeona uje kivyako ili kunusuru maisha yako. Hatakama ni woga, wako umevuka mipaka. Ulicho andika huku mitaani tunakiita: Sifa za kijinga.
 
Labda kama ulitumia tamathali za sema kufikisha ujumbe tofauti na huo uliotuwekea hapa. Chapisho ni la mwaka 2019, lakini takwimu ni miaka kabla ya 2015. Maana yake, hii ni taarifa ya mwaka huu inayoelezea mafanikio ya kipindi hicho (2011-2015) ambacho kilikuwa chini ya JK kuwa Tanzania iliongoza kupunguza umasikini. Ripoti itakayokuja ndio itakayoipima serikali ya JPM.
Kiukweli kunahitajika elimu kwa Watanzania kusoma ripoti. Mwaka 2000-2011 was the data collection period, unaweza kukuta kwa data hizo, kwa mwaka huo, wala Tanzania haikuongoza. Date of publication ndio hii ya Dec, 2019. Hii maana yake Tanzania ndio inayoongoza sasa kwa ripoti ya mwaka huu.

Mimi nina watoto 10!. Tukifanya research ya members wa jf wenye watoto wengi kwa mwaka huu wa 2019, naweza kuongoza. Ikichapishwa Ripoti ya "Wana JF Wenye Watoto Wengi 2019", jina langu likaongoza. Ukiangalia niliwapa lini, huwezi kuja na hoja kuwa tangu 2015 tayari nilikuwa na watoto 10, hivyo hiyo rekodi ni 2015!. Ripoti ikitoka mwaka huu, mimi nikaongoza kuwa na watoto wengi, haijalishi walizaliwa lini, bingwa wenu nitakuwa ni mimi, unless aje mwenye watoto 11!.

Sasa katika ripoti ya mwaka huu ya WB kuhusu kiwango cha kupungua umasikini duniani, Tanzania ndio tumeongoza sio kwa nchi za East Africa, Sio kwa nchi za Bara la Africa, bali tumeongoza kwa dunia nzima!. Haijalisi data zilikuwa collected lini, bali ripoti ndio imechapishwa sasa na ni ripoti ya mwaka huu!.
P
 
Paschal, waandishi wa habari wenzako wanatekwa na kubambikiwa kesi za utakatishaji fedha na uhujumu uchumi.Wewe umeona uje kivyako ili kunusuru maisha yako. Hatakama ni woga, wako umevuka mipaka. Ulicho andika huku mitaani tunakiita: Sifa za kijinga.
Waandishi hao ni wangapi tanzania?
Usiseme waandishi bali tuambie ukweli kwamba wale ni mamluki na wanakumbana na madhara ya umamluki tu!

Mao ze dong kule china ali akiwa anaijenga China,alikuwa akiwatandika shabaekeza hadharani wasaliti na mamluki wote na ndio matokeo ya china hii tuionayo sasa!

Nyinyi hapa mnaendekeza mitandao ya kusaka madaraka na kujipanga kuturudisha kulekule kwenye wizi.

The truth ni kwamba JPM NDIE MKOMBOZI WA WATANZANIA 2025 [emoji1241][emoji818]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanabodi,
Naendelea kusisitiza kwenye mazuri, tupongeze, kwenye mabaya tukosoe,kwenye maovu tulaani, kwenye mapungufu tushauri na kutoa mapendekezo.

Leo nilikuwa napitia ripoti ya Benki ya Dunia(WB) kuhusu hatua ambazo zimechukuliwa na nchi mbalimbali kupunguza umasikini uliotopea, I was surprised kukuta Tanzania ndio nchi ya kwanza inayoongoza duniani kwa kupiga hatua kubwa zaidi kuondoa umasikini uliotopea, hivyo japo data ni miaka iliyopita, lakini ripoti ni mwaka huu!, hapa tunajadili ripoti ya 2019 na sio data ni za lini, hivyo Rais Magufuli na serikali yake ya Awamu ya Tano, wanastahili pongezi za dhati kwa kufanya maajabu makubwa kabisa katika vita dhidi ya umasikini uliotopea kwa kupiga hatua kubwa zaidi kupunguza idadi ya familia zilizokuwa zinaishi chini ya kipato cha dola moja kwa siku.

Ripoti hiyo ni hii
View attachment 1304778

Hata Hivyo, Ripoti ambayo ni ya mwaka huu 2019 imeonyesha data za Tanzania kuongoza kwa kupungunguza umasikini uliotopea, zilikusanywa katika kipindi cha miaka 10 tangu 2000 hadi 2011 ila haikusema in details, Tanzania imefanya nini katika kupunguza umasikini huo, naomba tuisome ripoti hii kwa kanuni ya "the end justify the means, kwasababu kwa sasa Tanzania ni Tanzania ya Magufuli, na Tanzania ndio inayoongoza kwa kupunguza umasikini, regardless ni kipindi cha nani umasikini huo ulipungua, as long as ripoti ndio imetoka sasa na Tanzania tunaongoza, then ni haki na halali kabisa pongezi hizi ziende kwa Magufuli na awamu yake ya tano, ila pia kwa vile najua kuna kazi nzuri inayofanywa na TASAF, kwenye ule mpango wa kunusuru kaya masikini, huku MKURABITA, ukirasimisha rasilimali na biashara za wanyonge, na hatua nyingine mbalimbali zinazochukuliwa na serikali ya awamu ya tano katika kupunguza umasikini na kuinua kipato.

Wajameni, taarifa hii ni kwa mujibu wa datas za kuaminini za WB, maana humu jf kumezuka mtindo wa kubeza tuu kila kizuri kinachofanywa na awamu hii. Kwa vile mimi sio mchumi, hata ule ukuaji wa uchumi wa taifa wa zaidi ya asilimia 7% kwa mwaka, ulikuwa unanitatiza kwa sababu nikiangalia hali halisi huku mitaani mambo yanakuwa ni magumu sana, na kujiuliza huo ukuaji wa uchumi wa zaidi asilimia 7% unamfaidia nani, ni mpaka mchumi wetu Number 1 aliponifafanulia ndipo nikaelewa.

Hivyo hata bandiko hili, kama familia yako sii miongoni mwa kaya zinazoishi kwa kipato cha chini ya dola 1 kwa siku, unaweza usielewe kuwa Rais Magufuli na awamu yake ya tano, wanafanya mambo makubwa mazuri ya kuleta maendeleo kwa taifa letu.

Hongera rana rais Magufuli na kikosi kazi chako cha awamu ya 5, inawezekana kabisa sisi Watanzania, tusione, lakini kama World Bank wameona, dunia imeona, wasioona sasa wataonyeshwa.

Na kwa vile mwaka ujao ni mwaka wa uchaguzi mkuu, kuna wanasiasa ambao watapanda jukwaani na kujinadi kuwamkituchagua tutafanya hiki na hiki na hiki, lakini kuna wengine, watapanda jukwaani sio tuu kusema, bali kuonyesha walichofanya, hivyo naomba kuwaandaa watu kisaikolojia, usije kufika muda huo, watu ambao hawana chochote cha kuonyesha kuwa wamefanya, watakatakiwa kupanda kilingeni na watu wenye good track records za waliyoyafanya, kisha wasio na kitu wakaamua kuweka tena mpira kwapani, nashauri tuu, lets save time, money and resources, kama Watanzania tunachotaka ni maendeleo, na maendeleo hayo yanapatikana, yanaonekanika, then kwa nini tusiwaache tuu tuendelee tuu bila kufanya ....
naomba nisimalizie watu wasije kuniparura bure humu.

Nawatakia maandalizi mema ya kuingia 2020!.
Paskali
mayalla. Wewe ni msomi na watu wengi wanakuheshimu. Hizo Data zinaonesha ni za mwaka 2000 hadi 2011 . Unajua hakika kua wakati huo JP Magufuli alikuwa hajakuwa Raisi. Inakuwaje hizo Pongezi huzipeeki kwa wanaohusika? Au tuseme ni Propaganda au ni upotoshaji a maksudi?
 
Hapana kwenye hili umepotosha mkuu. Ni sawa kumsifia Magufuli kwa kile alichofanya kwa kipindi cha miaka mi-nne yaani 2015 Nov -2019 Nov. Lakini kwa taarifa uliyoleta yenye jedwali linalohusu utafiti wa mwaka 2000-2011, jedwali hilo haliwezi kuhuishwa na uongozi wa 2015-2019. Sifa hizo zinakwendwa kwa Rais mstaafu Mh. Jakaya Mrisho Kikwete.
Kwanini tusiwe wakweli tu jamani. Kwanini usikubali tu kwamba data ni za kipindi cha 2000-2011 ila taarifa imetoka mwaka 2019 na haihusu watu ambao waliozaliwa mwaka 2012 na kuendelea.
Tunawapenda ma-Rais wetu na serikali zetu zote zilizopita na hii iliyopo, ila kuna WATU MNAJIPENDEKEZA SANA kwa serikali ya sasa na kusahau serikali zilizopita. Nadhani mnasababu tusizozijua za kujipendekeza kwenu.
PEACE BE UPON YOU!
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu Tirampulaizesheni, kiukweli issues za data analysis ni moja ya maeneo magumu sana kwa sisi Watanzania, na sio data analysis tuu bali hata news analysis.
Kwenye data collection, kuna kitu kinaitwa comparative analysis, japo hizo data kwa Tanzania zmekuwa collected 2000-2011, data hizo zingechakatwa kwa mwaka huo, ungekuta labda wala Tanzania haikuongoza, lakini kwa data hizo hizo kwa ripoti ya 2019 sasa ndio Tanzania inaongoza dunia!. The report ni ya mwaka huu 2019.
P
 
Huyu jamaa hajatembea mikoani aangalie watoto wakiokota ukoko majalalan ili nafsi imsute aje kufuta uzi wake huu kuna watanzania wenzetu wanaishi maisha ambayo hayaelezeki jamani acheni kusifia kila jambo jamani Daaah
Namuheshimu sana mleta Uzi.......ila kwa hili hapana.....kama upo dasalama tu sawa ila jaribu kutoka eneo na ufike interior of Tz utaona hali halisi ya WaTz

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kiukweli kunahitajika elimu kwa Watanzania kusoma ripoti. Mwaka 2000-2011 was the data collection period, unaweza kukuta kwa data hizo, kwa mwaka huo, wala Tanzania haikuongoza. Date of publication ndio hii ya Dec, 2019. Hii maana yake Tanzania ndio inayoongoza sasa kwa ripoti ya mwaka huu.
Kaka P. Ni sawa date of publication ni 2019 na ni sawa pia data ni ya 2000-2011. Tatizo linakuja pale unaposema au unapojaribu kusema huo ndio ukweli kwa mwaka huu wa 2019. Ili iwe kweli basi lazima kuwe na njia ya kufanya prediction kutumia hiyo data kutoka data collection time to the current time. Wewe kama mleta uzi ulitakiwa ujiridhishe kwamba kitu kama hicho kimefanyika vinginevyo ulitakiwa uwatahadharishe wasomaji wako kuhusu ukweli huo. Sasa wewe ulivyoiweka inaonyesha kama mambo hayo ni kweli kwa 2019 na bahati mbaya hata kama ni kweli hiyo haikuwa awamu ya Magufuli. Hapo ndio umejipalia mkaa.

Ningekuwa wewe badala ya kuwalaumu watanzania nige reflect, na kama wako sawa basi hakuna ubaya kujisahihisha au kukubali umekosea. Ukishupaza shingo hii itakula kwako kama mtu mwenye heshima zake hapa JF. Wish you all the best in this.
 
Watanzania tujifunze kusoma ni ripoti ya lini!. Ripoti hii ni Ripoti ya mwaka 2019 regardless data zilikuwa collected lini, validity ya ripoti yoyote ni the date of publication of the report na sio dates of data collection, hivyo as of now, Tanzania ndio inaongoza kwa kupunguza umasikini uliotopea kwa mwaka huu 2019!.
P
aisee HUNA AKILI WEWE! pumbavu kabisa!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom