Pongezi za Halima Mdee, Zitto na ACT Wazalendo, namuona Mdee aliibukia ACT 2025

Hata hawo kina Lissu na mbowe wote washaramba asali, chadema imepwaya sana hatuoni tena commitment ya chama nimeshangaa sana mtu kama mbowe sasa hatoki Ikulu akimsema maalim seif sana
Chawa tulia huna ulijualo zaidi ya uchawa Ili mkono uende kinywani
 
Aende tu wote WASALITI
 
Vipi wewe SIO ASSET?Halima ANGEKUWA ASSET Angeenda CCM Chama tawala lakini kwa kuwa MSALITI ameona Ampongeze MSALITI MWENZAKE
 
Hapo umefeli ACT ni kama EFF ya South Africa ila Chadema ni kama DA ya sauzi au ODM ya Kenya yaani chama mbadala chenye mizizi nchi nzima ambayo kuing'oa ni ngumu.

Kumbuka ACT Ina wapiga kura laki 1 pekee 2015 na 2020 licha ya uwepo wa Maalim mgombea wao Urais hakufika hata kura laki 1!!! Ila Chadema licha ya kwamba walipewa Jimbo Moja ila kura za wagombea ubunge zilifika million 3 ikimaanisha tayari wagombea wake Wana mtaji mkubwa.

So Mdee aligombea kawe atakua na mtaji wa kura elfu 10 hivi huku mgombea wa Chadema atakua na kura sio chini ya elfu 50 za kuanzia. Kilichompa ubunge Mdee sio umaarufu wake Bali umaarufu wa Chadema.

Huyo Zitto mwenyewe huko kigoma alizidiwa kura na Chadema Sasa kama tu Hana political base huko kwake Nini kinakupa assurance kuwa atawasaidia Hawa wasaliti wapate ubunge?!

Poor analysis!! Uliwajaza hivi hivi wale wamama wa viti maalum waliokumbilia Nccr ila sidhani hata unajua wako wapi Leo!!
 
Karibu pande hizi The Doctrine ya Mwanasiasa Kuwa Maarufu Kuliko Chama!-Ni "Utumishi wa Watu VS Utumishi wa Chama
P
 
Huyu anakula fedha za umma akijua fika hajachaguliwa na Chadema! sasa huyu malaya wa kisiasa anashauri nini? Malaya ni malaya tu, malaya wa kisiasa lakini.
Mke wa Benson Kigaila ni viti maalum, pamoja na michepuko kadhaa ya viongozi, mchepuko wa Lissu uliporukwa, ndipo zogo likaanza, akawa anatishia kujitoa chadema
 
Vyama mbadala kwa sasa Tsnzania hakuna. Kuna vyama vya upinzani tu.
 
Nafikiri hii superiority attitude ndo itawamaliza CHADEMA, yani wanadhani CHADEMA milele ndo itakuwa mbadala, Tanzania mpaka sasa vyama vitatu vilishabadilishana kuongoza upinzani. Zitto unaemtaja alikuwa sehemu ya mafanikio ya CHADEMA ambayo kwasasa imepoteza brain power na kubaki kuwa watu wa dogma, watu wa likes/retweet mitandaoni na kujigamba kuongoza upinzani hivyo huwezi kulinganisha na DA ambao wanamizizi na wanaungwa mkono na watu wenye fedha hasa walowezi;
1. CHADEMA na ukubwa wake umeletwa na Akili na juhudi za kina Slaa, Zitto, Safari, Baregu, Kitila, Mbowe, Lissu hivi sasa wana watu hawa au wamebaki na wapiga ramli, dogma na watu wakutafuta sifa za mitandao bila kujali wanapost uwongo au ukweli
2. Nchi hii ni very diverse haswa kwenye swala la dini ndo maana Zitto alikuwa muhimu sana kubalance that with CHADEMA ila mihemko ikamuondoa sasa angalia ACT inaungwa mkono wapi utajua the factor nyuma yake and with that push na uwezo wa viongozi wa ACT muda kwa muda wataendelea kula wafuasi wa CHADEMA
3.Cha muhimu zaidi CHADEMA wamepoteza uwezo wa kutengeneza sera na kuvutia tabaka la wasomi na wenye uelewa ACT is winning that na ukiamau kufanya uchambuzi huru utaona jinsi ACT walivyowabunifu, wanatafiti, wanajipanga, wanatoa mbadala tena kwa kipindi hichi ambacho firebrand politics hazifaii maana Samia sio mtu wa hivyo.
4.ACT kuwapokea wafuasi wa maalim kumekifanya kuwa chama chenye resource kuanzia ya ki weledi, uzoefu na ujuzi kuliko CHADEMA hivyo CDM ajiangalie na kikubwa wanachozidiwa CDM na ACT ni kuwa ACT viongozi wake wanaaminika na Dola na Taasisi zake wake CDM labda Mbowe/Mwalim/Mnyika wanaweza na dola kwasababu ni predictable wapo rational wengine wanaona sifa kuchukiwa na dola na taasisi zake sasa sijui serikali wataipata vipi labd kama wana mpango wakupindua

Kiukweli CHADEMA wakilalia sie ndo tunaongoza upinzania ni rahisi zaidi kupotea Tanzania maana kuna factor nyingi sana zinasaidia wapinzani wao na hasa hawa wapinzani wakiwa na weledi kama wa ACT
 
Chawa tulia huna ulijualo zaidi ya uchawa Ili mkono uende kinywani
Sasa utabaki kumsikiliza Tundu Lissu kwa youtube yeye anavaa makoti akipiga mishemishe zake Belgium., poor chadema
 

Mkuu nimependa analysis Yako unfortunately siasa za Afrika be it Sauzi au Kenya au Uganda sio za sera Bali umaarufu!! Ni mara ngapi tuliambiwa Odinga amechokwa au Maalim amechokwa ila wamekua waki maintain political base Yao bila hata sera kivile ila LOYALTY tu ya wafuasi wake waliogeuka cult.

2. Chadema imevuka level ya chama imekua cult Kwa members wake. Mfano Mimi Kuna mengi tu yananikera Chadema ila no matter what ntaipigia kura tu Kila chaguzi sababu nliipenda tokea 2004 so Sina kingine zaidi ya LOYALTY tu (Which is sad of course).

2. Nikiri ACT Wana sera nzuri na wapo organized kuliko vyama vyote vya upinzani Tanzania ila kama nilivyosema siasa zetu sio za issues ni ushabiki. So usitegemee Kuna mtu anasubiri kusikia sera za ACt Bali wanataka kuona amesha amsha tu ya kichama (Hii wanayo Chadema na CUF ya enzi zile) na sio makaratasi.

3. Niliwahi sema humu Chadema hata ikikosa wabunge wa kuchaguliwa Bado itakua KUB sababu Ina mtaji wa kura million 2 kabla uchaguzi haujafanyika so hata wakikosa majimbo yote wana assurance ya viti maalum walau 30!! Namba ambayo ACT hawawezi ifikia hata wakishinda majimbo yote ya pemba!!.

4. Kuhusu Zitto ni kweli alikua ana balance ila Chadema imeshavuka hiyo stage ya udini maana imetapakaa nchi nzima na hata chaguzi zilifika huwa Wana Pata back up ya Maalim so Wana balance kura za bara na Pwani. Dr Slaa, Lissu, na Lowassa waliweza Pata kura nyingi za Urais hata maeneo ya uislam kuliko mgombea yoyote yule wa upinzani. Hata hapo Ujiji Lissu alizoa kura za Urais kuliko mgombea wa ACT licha ya kwamba sio muislam au Muha!!

Trust me 2025 usishangae Chadema ikapata wabunge wengi Lindi na Mtwara kuliko ACT!! Mark my words...... Chama ni mtandao na ni Chadema pekee Wana mtandao huo. ACT haiwezi pata jimbo Kanda ya ziwa ila Chadema ipo assured na kura za Mara, Bukoba, Ukerewe, Shinyanga, Geita, na Mwanza hizo pekee ni nyingi kuliko ACT wakishinda majimbo yote ya Pwani na Zanzibar!!

So siasa ni numbers sio sera and Chadema have the numbers like DA and ODM!!
 
Wabunge wa maslahi binafsi. Kwanini asitoke sasa hivi wakati Chadema hawamtaki? Ni kwasababu ya marupurupu na pesa😂 Yaani unapenda chama lakini unasubiri miaka miwili na zaidi kuamia🤔🤔 ujinga wa TZ huu
 
Leo ndio siku yenyewe ya wanawake duniani, hongera sana kwa wanawake wote duniani akiwemo Mwanamke huyu!.
P
 
Rubish
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…