Pongezi za Miaka 60 ya Muungano: Twende Kwenye Muungano Kamili wa Ukweli wa Nchi Moja, Serikali Moja na Rais Mmoja? Kero Zote za Muungano Zitayeyuka!

Kwa vile Muungano haukupata ridhaa ya Wananchi ni muda sasa umefika tuuamua kama kweli tunautaka muungano au hatuutaki. Kama tunautaka basi tuamue ni muungano wa aina gani ....!!

Hata huko UK, Wascotland walipozidisha kelele ..... Wananchi wa Scotland walipewa nafasi ya kuaamua kama wanautaka muungano au la ingawa wamekuwa ndani ya muungano kwa zaidi ya miaka 300.
 
Muungano kwani huu wa lazima
 
Great minds...
 
Naunga mkono hoja, kuhusu kuitishwa kwa kura ya maoni, watu waulizwe wanataka muungano wa aina gani, ila sii kweli kuwa muungano haukupata ridhaa ya wananchi, Tanganyika tuliridhia, Bunge letu tulifanya ratification ila Zanzibar ndio haikuridhia, ila Karume alitoa tamko kwa wanabalozi kuwa Zanzibar imeridhia, ila ni kweli mwanzo Zanzibar iliburuzwa kisha ikaridhia nyenyewe. Baada ya tamko la "Muungano kama koti, likikubana unalivua", unajua kilichotokea!, na ile kuchafuka kwa hali ya kisiasa ya Zanzibar, unajua kilichotokea, muungano utalindwa kwa gharama yoyote!.

Muungano ni kama ndoa, Mwanamke kama hakutaki, mwache!. Usimbake!. Muungano wa bila upande mmoja kuridhia ni sawa na ubakaji. Ila aliyebakwa, ameendelea kuishi na mbakaji, akitoa huduma zote, hivyo anahesabika ni kuridhia by performance.

Japo Zanzibar haiku ratified muungano, lakini imetekeleza muungano, hivyo ni imeridhia impliedly. Je, wajua kuwa Zanzibar haikuridhia Muungano? Ina Maana Gani?

Tanzania hatuna sheria ya kura ya maoni, Zanzibar mnayo, pigeni!. Wanzanzibar amueni moja, ama acheni kelele za muungano!, ama pigeni Kura ya Maoni, muamue moja
P.
 

Muungano haipo kisheria

Sikiliza maoni ya Shivji na Jussa


View: https://youtu.be/aEMbKGQ9Bsg?si=_a6e66sL3E5BaW9m
 


View: https://youtu.be/ng0621BM410?si=OQcfcxQ1LaMnpnJU
 
Honorable learned Adv P. I salute you with hereunder challenges to your reactions:
Have you ever heard a United Republic of Tanzania president instructing the president for Zanzibar Isles as does to the VP, PM, Ministers, and other executive subordinates in any union-related matters? If, not why are you persistently claiming that there is one and only one president for the 'United Republic of Tanzania-URT' and that the latter executes his duties on a hanging and vacuum sovereignty bucket knowingly Zanzibar is a state with a constitutionally recognized president?

Why are there two constitutions for the United Republic of Tanzania and the Revolutionary Republic of Zanzibar excluding for Tanganyika to advocate its identity? This kind of union is havoc to endure

The best way to dissolve the outstanding tensions that politicians mostly fuel, is to recall a whitepaper poll from the citizens who determinately would suggest which kind of union they prefer that is tailored to suit the culture, core values, and social affiliations without prejudicing others' rights.
I can assure you that the union is meant for the political leaders only whilst the normal civilians are naturally union-integrated based on social and business historical grounds.

The citizens were not involved in drafting and formalizing the implementation of the current union structure which is why every day Complaints and concerns of citizens regarding the implementation of union affairs are escalating beyond tolerance.

To be precise the following are a nuisance to entertain and confidently continue promoting and advocating that the union is beneficial to both parties. Refer to Prof Shivji on this link:
View: https://www.youtube.com/watch?v=2v6qMQcqx8U
 

Mkuu, kumbuka pia huku bara walioridhia ni Wabunge wa TANU na siyo wananchi. Ni sawa na sasa useme wananchi tumeridhia Mkataba na Waarabu wa DPW wakati ni Tulia na watu wake wametumika.
 
Mkuu, kumbuka pia huku bara walioridhia ni Wabunge wa TANU na siyo wananchi. Ni sawa na sasa useme wananchi tumeridhia Mkataba na Waarabu wa DPW wakati ni Tulia na watu wake wametumika.
Hapa unahitaji kidogo kujua elimu ya uraia, wabunge ndio wawakilishi halali wa wananchi, ridhio la mikataba ya kimataifa, ratification, inafanywa na Bunge na sio wananchi!, hivyo Muungano uliridhiwa rasmi na Bunge la Tanganyika, ila kwa Zanzibar, aliyeridhia ni mtu mmoja, Rais Karume.

Hata mkataba wa DPW, kuridhiwa na Bunge ndio utaratibu, tatizo la mkataba ule, sio mkataba ni makubaliano, Bunge halikutakiwa kuridhia makubaliano hayo. Japo Bunge Limeridhia, DPW Kuendesha Bandari Zetu, ni Makubaliano Tu, Tukithibisha Kuna Matatizo, Tunarekebisha Mkataba wa HGA, Kazi Nzuri Iendelee!
P
 

Umeandika, nakunukuu

ila kwa Zanzibar, aliyeridhia ni mtu mmoja, Rais Karume.

mwisho wa kunukuu


Swali

Una ushahidi wa maandishi kuwa Karume aliridhia ??
 

Elimu hiyo unayonipa ninaifahamu tayari. Labda hujaelewa point yangu.

Ni kweli kwa katiba yetu hii ya CCM Wabunge ndiyo Wawakilishi halali wa Wananchi. Je ni halali Wabunge kuendelea kutuamulia kwenye mambo makubwa kama hayo...!? Tatizo ni kwamba katiba yetu haiwapi wananchi mamlaka ya kujiamulia mambo yao wenyewe. Mamlaka yapo kwenye kikundi cha watu wachache. Worse enough hata kuchaguliwa kwao ni kimangushi tu .... wanapachikana kama wanavyotaka wenyewe.

Mfano mzuri wa kumaliza utata kama Wananchi bado wanaridhia muungano au la ni kufanya kama kile walichokifanya kule Scotland, UK. Tuliona Wananchi wake walikubaliwa kupiga kura kuona kama bado wanataka kuendelea na muungano wa miaka zaidi ya 300. Mfano mwingine ni UK yenyewe. Wananchi wake walipiga kura kuaamua kama bado wanata kuendelea na EU au la .... majibu wote tunayajua.

Swala la DPW nimelitoa tu kama mfano. Kwamba ni mkataba au siyo hilo tulishalijadili sana na kila mtu abaki na anachokiamini.
 
Hivi unaposema Tanzania hatuna Sheria ya kura maoni, Zanzibar mnayo, pigeni UNAMAANA GANI?
Au unamaanisha Tanzania ndiyo Tanganyika au Zanzibar haipo Tanzania?
Kuna mtu mmoja alikuwa mkali na jeuri sana ikitamkwa neno Muungano mbele ya macho yeke..Shelf Khatibu (RIP). Alionekana kama msomi mzuri na mtunzi mzuri wa vitabu ila alikuwa mhafidhina kwelikweli.
 
Elimu hiyo unayonipa ninaifahamu tayari. Labda hujaelewa point yangu.
Kiukweli nakuelewa sana kuliko unavyodhania
Ni kweli kwa katiba yetu hii ya CCM Wabunge ndiyo Wawakilishi halali wa Wananchi. Je ni halali Wabunge kuendelea kutuamulia kwenye mambo makubwa kama hayo...!?
As long as hivyo ndivyo katiba inavyosema, ni halali, hadi ibadilishwe.
Tatizo ni kwamba katiba yetu haiwapi wananchi mamlaka ya kujiamulia mambo yao wenyewe. Mamlaka yapo kwenye kikundi cha watu wachache. Worse enough hata kuchaguliwa kwao ni kimangushi tu .... wanapachikana kama wanavyotaka wenyewe.
Ni kweli, na nakuunga mkono
Kwa vile sisi bado hatuna sheria ya kura ya maoni, hatuwezi kupiga kura kuuliza hilo, lakini kwavile Zanzibar, sheria ya kura ya maoni mnayo, kwanini msipige kura nyinyi na kuamua?. Niliwashauri hapa Wanzanzibar amueni moja, ama acheni kelele za muungano!, ama pigeni Kura ya Maoni, muamue moja

P
 
Hivi unaposema Tanzania hatuna Sheria ya kura maoni, Zanzibar mnayo, pigeni UNAMAANA GANI?
Tanzania hatuna sheria ya kura ya maoni!, serikali yetu ikitaka kufanya jambo lolote inafanya tuu bila kuwauliza wananchi wenye nchi, lakini Zanzibar, wao wanayosheria ya kura ya maoni, wakitaka kufanya jambo kubwa, wanawauliza Wazanzibari.
Au unamaanisha Tanzania ndiyo Tanganyika au Zanzibar haipo Tanzania?
Tanzania ndio nchi, halafu Zanzibar ni nchi ndani ya nchi!. Zanzibar wanaweza kupiga kura ya maoni na wakaamua, tatizo ni uamuzi huo huishia Chumbe, Tanzania hatuutambui, Tanzania hatuitambui katiba ya Zanzibar, wala hatuitambui GNU!.
P.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…