Pongezi za Miaka 60 ya Muungano: Twende Kwenye Muungano Kamili wa Ukweli wa Nchi Moja, Serikali Moja na Rais Mmoja? Kero Zote za Muungano Zitayeyuka!

The best way ni kuiexpose Tanganyika kutoka kwenye koti la muungano, yaan tuunde federation.

Swala la kuunda Union kwa sasa ni ngumu. Huwezi kuunda Union wakati majority ya wazanzibar wanasema wanataka Zanzibar yenye mamlaka kamili, yaani hii kitu ya Zanzibar kuwa mamlaka kamili ni very sensitive Sana, kuna wazanzibar hata ndani ya ccm wanaamini kwenye Zanzibar yenye mamlaka Ila wanaogopa tu kusema hadharani, unless kama tunataka kuwaburuza watu ili iundwe hiyo Union, mwisho wa siku watu wataishi kwa chuki kwenye mioyo kwa kuwalazimisha kitu ambacho hawakitaki.

Muungano unatakiwa uwe na Win Win situation , watu waridhiane na siyo kulazimisha Mambo.
 
tuwape tu uhuru wazanzibar wachague, wakitaka kusepa waende tena asubuhi kabisa.
 
tuwape tu uhuru wazanzibar wachague, wakitaka kusepa waende tena asubuhi kabisa.
Mkuu Yesu Anakuja , umewahi kupendwa usipopenda, ukaamua kumhurumia mpendaji, ukamkubalia kumuoa ili kumsitiri, na baada ya ndoa, ukajikuta na wewe sasa unapenda, ikitokea sasa mpendaji mara anasema hakutaki tena, ungekuwa wewe, talaka utatoa?. Niliwahi kuuliza Tangu lini Mke Ndani Ya Ndoa Akaomba Uhuru ili Kutoka Nje Ya Ndoa? Aruhusiwe?

Aliyeomba muungano ni Zanzibar,
Ili Tanganyika imsitiri
Tanganyika ikakubali
Tukaungana
Tanganyika ikapenda kufa, ikafa ikaoza, ikajifuta hadi jina la Tanganyika ikalifuta.
Kuna kumwacha tena huyu mwali?!.
Ni kufa na kuzikana!.
Muungano wetu adimu na adhimu, tutaulinda kwa gharama yoyote, milele na milele.
P
 

Ushahidi upi kuwa Zanzibar iliomba Muungano ? Au ni hadithi Za vikao vya mbege hizo ?
 

Kama Zanzibar hamuitambui Katiba ya Zanzibar , huyo Lissu na Chadema yake wanalalamika kitu gani kutawaliwa na Mzanzibari ?
 
Kama Zanzibar hamuitambui Katiba ya Zanzibar , huyo Lissu na Chadema yake wanalalamika kitu gani kutawaliwa na Mzanzibari ?
Sio kama Zanzibar hawaitambui katiba ya Zanzibar, ni katiba ya JMT ndio haitambui katiba ya Zanzibar lakini inawatambua Wazanzibari kama Watanzania wengine wote na wana haki zote sawa sawa ikiwemo kuwa rais wa JMT.
P
 
Kama Zanzibar hamuitambui Katiba ya Zanzibar , huyo Lissu na Chadema yake wanalalamika kitu gani kutawaliwa na Mzanzibari ?
kwa bahati mbaya au nzuri, kile amesema Lisu ndio kipi moyoni mwa Watanganyika wengi, ila wanaogopa tu, ila wangekuwa huru kuongea, ungeshangaa sana. hakuna mtu wa Bara anajua faida tunapata kuungana na zanzibar, given the treatement we receive from zanzibaris na faida wanazozipata wao kwetu wakati sisi kwao hatupati kitu. ni unahudumia mchepuko
 

Kwani Wazanzibari wanapata faida kwa kuuliwa ndugu na jamaa zetu kila uchaguzi kulazimisha kuweka vibaraka vyenu?
 
Siungi mkono hoja maana Mwl Nyerere alikwishalitolea ufafanuzi. Popote pale duniani nchi ndogo kwa ardhi na idadi ya watu inapoungana na nchi kubwa kijiografia na idadi ya watu nchi ndogo huwa na hofu ya kumezwa. Wakati tunaungana Zanzibar ilikuwa na watu 360,000 huku Tanganyika ikiwa na watu 12milioni. Lkn Zanzibar ilikuwa ni nchi kamili. Kutaka Serikali moja na Rais mmoja ni kuidogosha Zanzibar na kuifanya kuwa Mkoa sawa na Mwanza. Tunaweza kuondosha kero za Muungano bila kuidogosha Zanzibar. Kutoka kero 22 Hadi kubakia 4 ni mafanikio makubwa mno.
 
Kwani Wazanzibari wanapata faida kwa kuuliwa ndugu na jamaa zetu kila uchaguzi kulazimisha kuweka vibaraka vyenu?
kwanza mnapata exposure ya alimu,

pili, mnaajiriwa bara ili kulisha watoto wenu.

mnaruhusiwa kumiliki ardhi yeyote mpendayo.

mnateuliwa vyeo serikalini huku bara.

mnakopa ila sisi tunawalipia wakati mna TRA yenu.

vipi,niendeleee?
 
kwanza mnapata exposure ya alimu,

pili, mnaajiriwa bara ili kulisha watoto wenu.

mnaruhusiwa kumiliki ardhi yeyote mpendayo.

mnateuliwa vyeo serikalini huku bara.

mnakopa ila sisi tunawalipia wakati mna TRA yenu.

vipi,niendeleee?

kupata hayo ndiyo mje kuwauwa ndugu na wazee wetu kila ufikapo uchaguzi na kuwaweka vibaraka wenu ??
 
kupata hayo ndiyo mje kuwauwa ndugu nz wazee wetu kila ufikapo uchaguzi na kuwaweka vibaraka wenu ??
ndio tunataka muondoke ili mkaishi peke yenu huko zanji. muondoke kigamboni na DSM na mikoani, mrudi tu kwenu, manake hakuna usawa. kwanza iweje kamkoa kenye watu 2m kajifanye kako sawa na nchi yenye watu 58m. haiji akilini. mmelishwa kila kitu lakini hamridhiki, ajira, ardhi everything hadi ulinzi ila hamridhiki.

 
Huu ndio ukweli, tena ukweli mtupu
 

Sasa jibu swali
kupata hayo ndiyo mje kuwauwa ndugu na wazee wetu kila ufikapo uchaguzi na kuwaweka vibaraka wenu ??
 
Sasa jibu swali
kupata hayo ndiyo mje kuwauwa ndugu nz wazee wetu kila ufikapo uchaguzi na kuwaweka vibaraka wenu ??
nani ameuwa ndugu zako aisee mbona unaongea makorombwezo? haueleweki. tukisema muondoke unarukia kuwa tunauwa ndugu zako, wepi? na ninyi mbona mnatubagua tukija huko na mnaturushia mabom ya petroli?
 
nani ameuwa ndugu zako aisee mbona unaongea makorombwezo? haueleweki. tukisema muondoke unarukia kuwa tunauwa ndugu zako, wepi? na ninyi mbona mnatubagua tukija huko na mnaturushia mabom ya petroli?

Unajifanya kama huelewi namna jeshi linavyomwagwa wakati wa uchaguzi pamoja na Polisi na Usalama wa taifa wenu

Yule Mkuu wenu wa usalama Diwani alipiga kambi pale Government press .

nakuonyesha namna tunavyoteswa kila uchaguzi na vyombo vyenu vya ulinzi ili kuwaweka madarakani vibaraka wenu


View: https://www.youtube.com/watch?v=gmxrblkDnbc&t=19s
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…