Posho mbili, Spika Sitta, Takukuru na Maadili yake!

Hii inaonyesha kwamba Hosea hana jipya anatumiwa na mafisadi tu kuwatisha Wabunge ili wasiiweke kwenye kiti moto kuhusiana na sakata la Richmond. Hosea wacha uhuni kazi imekushinda bora tu ujiuzulu.
 

mungu alishatusaidia na ujinga wetu,kwani nchi hii haina jeshi la kujenga nchi,maana hawa wote jeuri yao inatokana na ahadi za wahindi za kuwapa maisha, na ndiyo maana viongozi wetu hawatuheshimu maana walishalewa,nani alijuwa kama mkapa angetugeuka. sasa mambo anayofanya kikwete tuliyemuamini kwa asilimia 80 yako sawa? je ni haki kwetu afanyayo?
 
There is life after PCCB! What does it mean?
 

Aibu tupu. Watu wazima wanashabikia wizi!!!
 
Dkt Hoseah ameongea na waandishi wa habari leo na miongoni mwa mambo aliyoyaelezea ni kwamba ahukumiwe kwa haki na sio kwa hisia. Pia alisema kwamba haonei mtu na anafanya kazi kwa mujibu wa sheria. Alidai pia kwamba tuhuma dhidi ya wabunge kulipwa posho mbili kwa kazi moja zimetoka Bungeni! Hoseah alisema ombi la kufanywa uchunguzi huo ni la Bunge lenyewe kupitia barua ya Februari 26, 2008, ambayo ilimtaja yeye kwa jina ikimtaka afanye uchunguzi huo na kuhoji: "Kwa hiyo Bunge lenyewe linaweza kuandika barua kutaka kuwalenga watu fulani?"

Dk Hoseah alifafanua kwamba, tayari suala hilo la kuwajibishwa liko mamlaka ya juu (rais), hivyo ni vema wakasubiri maamuzi na kusisitiza kwamba, "uchunguzi huo utaendelea kwa hiyo waheshimiwa wabunge, wazee wangu toeni ushirikiano ili suala hili lisije kutufikisha pabaya, nchi hii ni ya amani".
Mkuu huyo alitumia mkutano huo kufafanua pia kwamba, uchunguzi huo haukumlenga mtu yeyote ambaye ni mjumbe wa kamati iliyochunguza kashfa ya Richmond, akisema: "Kwanini, mbona Mheshimiwa Zitto (Kabwe) tumemhoji, yeye alikuwa kamati ya Richmond?"

Kumbukumbu za Bunge (Hansard), kuhusu Taarifa ya Kamati ya Nishati na Madini ya Agosti mosi, kujibu taarifa ya serikali iliyotolewa Julai 25, inasema: "Mheshimiwa Spika, Azimio Na. 20, Serikali iendeshe uchunguzi maalum ili kubaini ukweli kama taarifa rasmi ya Takukuru iliyotoa matokeo ya uchunguzi kuhusu mchakato wa Richmond ilikataliwa na kuharibiwa na kutolewa nyingine.

"Na kama jalada halisi linalohusu kampuni ya Richmond lililokuwa BRELA liliharibiwa na kuwekwa jingine kwa lengo la kuficha ukweli. Mheshimiwa Spika, Utekelezaji wa Serikali: Kamati ya Vyombo vya Dola imekamilisha uchunguzi wake kuhusiana na suala hili.

"Na imebainika kuwa, si kweli kuwa taarifa rasmi ya Takukuru iliyotoa matokea ya uchunguzi kuhusu mchakato wa suala la Richmond ilikataliwa na kuharibiwa na kutolewa nyingine kwa lengo la kuficha ukweli.

"Vile vile, taarifa ya kamati ya vyombo vya dola inaonyesha baada ya upelelezi na uchunguzi wa kina kufanyika wameridhika kuwa jalada halisi la Richmond lililokuwa BRELA halikuharibiwa na wala hakukuwa na jalada lingine lililowekwa kuficha ukweli wa jambo hili."

"...Maoni ya Kamati; Kamati inaridhika na taarifa hiyo."
Hoseah akitumia azimio hilo, alisema alibahatika kusoma kwa makini taarifa zote za kamati kuanzia ya kwanza na hiyo ya pili na kuhoji : "Sasa nijiuzulu kwa kosa lipi, watu mnihukumu kwa haki, au unataka kuchukua nafasi yangu (alimuuliza mwandishi wa gazeti hili)?"
(Source: http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=15735).
 
kosa lako ni kushindwa kuishauri serikali kwamba kesi ya posho mara mbili etc ni jukumu la polisi na kiutawala zaidi kuliko kuwa la rushwa. hivyo ungewarudishia faili lao na barua zao ziende kunako husika.
na zaidi ya hapo hata sisi takukuru hua tunalipa hiyo posho kwa waandishi wa habari na wabunge na wadau wengine wanapo hudhuria warasha/kongamano /na semina zetu bila kusahau mikutano yetu iwe ya ndani au ya nje.
zaidi ya hapo tunatuhumiwa na wabunge kwa kuisafisha richomond, sasa wakati huu huh tukiwachunguza haita onekana tunatenda haki.
 
hosea maji shingoni tena ole sendeka alisema takukuru walifanya semina na wao wakagawa posho hizo hizo kwa wabunge walioshiriki, leo hii wanachunguza posho hiyohiyo waliotoa
 
kosa lako ni kushindwa kuishauri serikali kwamba kesi ya posho mara mbili etc ni jukumu la polisi na kiutawala zaidi kuliko kuwa la rushwa. hivyo ungewarudishia faili lao na barua zao ziende kunako husika

Nafikiri kosa alilozungumzia ni linalohusiana na Richmond! Chungulia post #1 tena utaelewa!
 
hosea maji shingoni tena ole sendeka alisema takukuru walifanya semina na wao wakagawa posho hizo hizo kwa wabunge walioshiriki, leo hii wanachunguza posho hiyohiyo waliotoa

Kosa la wabunge waliokwapua posho mbili kwa kazi moja kinyume na sheria ni kutokutoa taarifa kwa TAKUKURU kwamba tayari walishapokea posho kwa hiyo wasingestahili kulipwa tena!
 
Kesho itakapotolewa ripoti ya serikali katika kutekeleza maazimio yaliyotolewa na Kamati Teule ya Richmond kitaeleweka kwamba sakata hili lina mweleko gani!
 


Hawa watu nadhani wanatuchezea akili. Kwani baada ya kutolewa maazimio yale 23 ya bunge, serikali ilitakiwa kufanya uchunguzi tena au kuyatekeleza?

Kwa mfano kama azimio lilisema Hosea awajibishwe, serikali ilikuwa tena na nafasi ya kuchunguza upya kuhusu kosa la Hosea au ilitakiwa kumpa haki yake ya kumwachisha wadhifa wake?

Na kama Hosea hakukosea, pia Mwanyika au mdendaji yeyote serikali hakufanya kosa, basi nani alifanya makosa yote kuhusu Richmond? Na kwa nini EL na wenzake walisusa na kuachia nafasi zao na kusababisha baraza zima la mawaziri kufa kifo cha mende?

Naona ni usanii tu ndo unaendelea.
 
Nasikia mh. huyu kaitwa Dodoma jana,nadhani leo kuna jambo litatokea-tungoje na tusubiri.leteni data zaidi ya safari yake huko Dodoma.
 
hosea maji shingoni tena ole sendeka alisema takukuru walifanya semina na wao wakagawa posho hizo hizo kwa wabunge walioshiriki, leo hii wanachunguza posho hiyohiyo waliotoa

Nadhani hukusikiliza press conference ya Dr. Hosea. Kwa kweli katoa maelezo mazuri sana ya kujibu hoja zote walizotoa wabunge. Imeonyesha wazi kuwa Spika na Wabunge ni wapotoshaji wakubwa. Tatizo ni wabunge kulipwa posho mbili na sio kulipwa posho moja.

Ufafanuzi alioutowa:-

1. Posho walizotoa Takukuru kwa wabunge hazi kutolewa mara mbili. Ofisi ya Bunge haikuwalipa posho wabunge ku attend seminar hiyo. Kwa hiyo ni Takukuru tu ndio iliyowalipa.

2. Posho zinazochunguzwa na Takukuru ni zile zinazolipwa kwa Kamati za Bunge ambazo kwanza hulipwa na Bunge na baadae Kamati zikienda kufanya uchunguzi na mahojiano na wizara na mashirika hudai tena posho hizo hizo. Hii si takrima bali ni makosa.

3. Kwa sheria za Takukuru, kupokea pesa bila kuzitolea jasho ni rushwa.

4. Wabunge hawana kinga katika makosa ya rushwa. Wanayo kinga katika mambo yanayohusu shughuli zao za Bunge na matamshi wanayotowa Bungeni.

5. Ni Bunge ndio lilimuonba Hosea kufanya uchunguzi huo.

6. Yeye hanyimwi usingizi kama wabunge watampigia kura ya kutokuwa na imani naye. Yeye yuko pale kuwahudumia watanzania kwa kufanya kazi yake kwa uadilifu.

7. Wabunge waiachie Takukuru ifanye kazi yake.

8. Takukuru haikuwadhalilisha wabunge kwani yenyewe haikutangaza wabunge iliyowahoji bali ni wabunge wenyewe ndio walikimbilia kutangaza katika vyombo vya habari.

9. Hakuna Mtanzania yeyote aliye juu ya sheria.

Mimi personally nampongeza sana Dr. Hosea kwa ujasiri wake wa kuwa na msimamo. I am sure wabunge wamepata shock, walidhani wangeweza kumtingisha kwa kumtisha na sakata la Richmond lakini kumbe jamaa hatetereki. Kwa vipimo vyangu amefanikiwa kuvunja hoja zote za Sitta na wabunge.
 
Lakini kupokea posho na rushwa wapi na wapi? Mimi nina wasiwasi ilikuwa ni jitihada za kuwa-discredit akina mwakyembe kabla ya kujadiliwa kwa ropiti ya Richmond. Labda kama "rushwa" imepewa maana pana zaidi.
 

"Nani hajui kama wewe pesa za mafisadi zimekufikia?.Suala la kupokea posho mara 2 limeanza leo?.Basi wachunguze tangia bunge limeanza. Na je yale maazimio 23 akiwemo Osea kujihuzulu imekuaje kugongona na ilo la posho za wabunge, kwani osea amekuwa mkuu wa takukuru leo, alikuwa wapi siku zote?.Wewe ni mmojawapo wa mafisadi.
 
naunga mkono hatua za TAKUKURU kuwachunguza wanaopokea posho mara mbili..hakuna ubabaishaji hapa kama umepokea posho mara mbili na ukijua kwa dhati umekwisha pokea posho mara ya kwanza huo ni wizi...haina definition nyingine zaidi ya hiyo...huo ni wizi tu..simple mwakyembe na wenzako kubalini kuhojiwa acheni makelele hayatawasaidia otherwise no sooner we will clasify you all as wafa maji.
 

mawazo ya kizamani sana haya...
 


Mimi pia abiria wa basi lako... Wabunge wamechemsha big time!
 

Ni kwa taratibu gani ya kisheria TAkukuru wanatakiwa kutoa posho kwa wabunge?
2. Posho zinazochunguzwa na Takukuru ni zile zinazolipwa kwa Kamati za Bunge ambazo kwanza hulipwa na Bunge na baadae Kamati zikienda kufanya uchunguzi na mahojiano na wizara na mashirika hudai tena posho hizo hizo. Hii si takrima bali ni makosa.

hawa wanaotoa hizi posho kwa wabunge ni kina nani? wanazitoa wapi na katika fungu gani? Na kwanini wakidaiwa na wabunge wasigome?

3. Kwa sheria za Takukuru, kupokea pesa bila kuzitolea jasho ni rushwa.

Hiyo sheria imepitwa na wakati, mtu akikupa zawadi atakuwa amekupa rushwa? Basi wengi wetu humu tuna hatia ya kupokea zawadi!


4. Wabunge hawana kinga katika makosa ya rushwa. Wanayo kinga katika mambo yanayohusu shughuli zao za Bunge na matamshi wanayotowa Bungeni.

Wabunge wakiwa bungeni hakuna mahakama inayoruhusiwa kuwachunguza au kufanya uchunguzi wowote bila idhini ya Spika. Siyo kuombwa na Katibu wa Bunge. Bunge likikaa hakuna chombo cha dola kinachoweza kuleta hata summons ya kumuita mbunge yoyote. Sasa TAKUKURU wamepata wapi nguvu ya kuwaita wabunge kutoka kwenye kikao cha bunge kwenda kufanya uchunguzi wao? Soma sheria ya Haki, Madaraka na Kinga ya Bunge Ibara 5 na ya 11!


5. Ni Bunge ndio lilimuonba Hosea kufanya uchunguzi huo.

Hata kama hilo ni kweli, wanapoanza uchunguzi wao wanatakiwa watoe taarifa kwa Spika. Sheria inasema hilo haliwezekani "without Speaker's leave"!

6. Yeye hanyimwi usingizi kama wabunge watampigia kura ya kutokuwa na imani naye. Yeye yuko pale kuwahudumia watanzania kwa kufanya kazi yake kwa uadilifu.

Wabunge hawahitaji kumpigia kura yeye kwani hawamthibitishi uteuzi wake. WAbunge wataipigia kura serikali! Yaani, kutokuwa na imani na waziri mkuu. Sasa JK itabidi achague kumtosa Hosea au serikali yake iporomoke tena sababu ya kiburi cha watu wanaofikiri wako juu ya sheria.

7. Wabunge waiachie Takukuru ifanye kazi yake.

Hilo ni kweli, lakini ifanye kazi yake kisheria. Na hilo ni kusitisha uchunguzi wao sasa hivi, kuomba kibali kwa Spika wanapomtaka mbunge yoyote kutoa ushirikiano wakati kikao cha bunge kinaendelea. Nje ya hapo, wao ndio wamejinyanyua juu ya sheria.


8. Takukuru haikuwadhalilisha wabunge kwani yenyewe haikutangaza wabunge iliyowahoji bali ni wabunge wenyewe ndio walikimbilia kutangaza katika vyombo vya habari.

Imewadhalilisha wabunge kwa kufanya uchunguzi wakati kikao cha bunge kinaendelea bila ruhusa ya Spika.


9. Hakuna Mtanzania yeyote aliye juu ya sheria.

Na hilo linamjumuisha Hosea na Pinda. Kama ingekuwa kweli wanatawala kwa sheria Pinda alitakiwa kujiuzulu siku ile alipotoa ruhusa ya watu kujichukulia sheria mkononi utadhani hiyo sheria ni mapendekezo ya aina fulani.

Mimi personally nampongeza sana Dr. Hosea kwa ujasiri wake wa kuwa na msimamo.

Misimamo mingine siyo ya kupongeza ni ya kubeza. Msimamo wa kudai ana madaraka ambayo hana siyo msimamo wa kupongezwa.

I am sure wabunge wamepata shock, walidhani wangeweza kumtingisha kwa kumtisha na sakata la Richmond lakini kumbe jamaa hatetereki. Kwa vipimo vyangu amefanikiwa kuvunja hoja zote za Sitta na wabunge.

Wabunge wakikubali kushindwa mbele ya TAKUKURU na wakapigishwa magoti then the parliament has officially become irrelevant!. Hosea hawezi kutunishia misuli bunge akabakia alivyo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…