Poverty Elimination in Tanzania is a 'Result Oriented Business'


Chile please
 
Gainjin i think you meant "Chill" or "Chill out"?

Nakubaliana na wewe to some extent, (on lugha), lakini sidhani kama it can be much of the bigger problem that will impact or hinder our ability to achieve sustainable developments.

Nakubaliana na Asha Dii kwa kiasi kikubwa.
 
Unaweza kua result oriented kama umepanga hizo results vizuri. Huku bado tunapangiwa results na donors, bila kuchunguza how SMART the objectives/results are, bila kushirikisha mtanzania wa kawaida (only viongozi are consulted). Lazima ishindikane. Hapa naongelea kipindi hiki cha IMF na world bank, sio wakati ule wa ujamaa.
 

JMushi,

Umewahi kusikia mfano wa kuvunjika kwa madirisha ya nyumba? Ukiwa na nyumba iliyo na dirisha lililovunjika na kuacha kulitengeneza kwa muda mrefu, unaweza kuwavutia watoto na wahuni kutupa mawe na kuvunja madirisha mengine.

Tanzania hatukuanza na matatizo makubwa. Tulianza na matatizo madogomadogo na sasa yamekuwa utamaduni.
 
Tabia hiyo imeanzia chini kwa raia mmoja mmoja, kamwe hatujazowea kudai marekebisho au kukataa huduma isiyofikia viwango. Si migahawani, madukani, wala maofisini

That is expected each individual seeks to maximize his chances naturally under the given circumstances, that is to say most of us will pick battles we think we have greater chances of winning independently. Kwa maana hiyo kama umeenda kwenye mgahawa na huduma aijakuridhisha au hata kama chakula kilikuwa kimeanza kuchacha, unajuwa wazi in most cases hata ukilalama mwenye mgahawa atakwambia anza zako mazee. But then kama kungekuwa na chombo cha kusimamia haya malalamiko na kina nguvu ya kutoa adhabu kwa niaba ya mteja, mwenye mgahawa atafikiria mara mbili kuja na kauli za ajabu au kuweka chakula cha jana. People achieve the maximum when they work as groups ndio maana ya kuanzisha siasa duniani, hili certain groups ziwe represented kihalali katika jamii.

Gaijin,
Haya matatizo yanatokea sehemu mbalimbali. Hili kupunguza matatizo kama haya wenzetu wanazo quality assurance methodologies.

Ni Result Oriented individuals wanaoweza kufuatilia quality assuarance na mikataba ya kisheria.
Obviously vitu vitajirudia kwenye nyanja nyingi za maisha ya watu and the way they make their decisions in everyday lives, were there are no regulatory bodies it becomes a jungle with no guidance, people will only use their past experience to deal with those situations.

Maendeleo yepi yanayoweza kuja bila ya muongozo au njia sahihi za kukuza maendeleo, Baresa/Bakrhesa (or whatever his name is) anapeleka ngano yake mpaka nchi za ulaya sasa. Na mkulima mdogo hataweza vipi hilo bila ya mikopo iliyo sahihi au sera za serikali za kuwatafutia soko huko na wao. Point ni kwamba kuna watu hili waweze fika hatua fulani za mbele kunahitajika watu wengine wawawezeshe na kuhakikisha wanawafikisha hapo.

Hatuwezi kuondokana na umaskini kama hatujui kujieleza. Kama hatujui kujieleza hatuwezi kupata tunachotaka. Hili linaanzia kwenye mtu mmoja mmoja na hatimae serikalini.
Kujielezea nako inataka muda na ukitumia JF na post za watu humu ndani as the basis of your argument unakosea saaana. Kwa sababu kuna wengine uandika wakidhani wengine wana basics za hiyo argument ndio maana anaweka points kadhaa akitegemea wengine wana huwezo wa kuchambua argument yake inatokea au inaanzia wapi. Vinginevyo watu wangekua wanaandika maneno helfu moja kwenye post zao just for the sake of your argument. Nadhani wafuatiliaji wengi wangekua wameshachoka kusoma hiyo thread by the third post.

True, sasa mweleze Gaijin process yote hiyo ilivyo ndefu in practise hili akupate ndio sababu nasema, wakati mwingine it's easier watu wawe na hata basics. Sisemi yeye.


Donors wanapanga results zao kwa maslahi yao na sisi je watanzania? Kuna chombo gani cha kijamii au cha kijumuia kama pressure group kinachoangaika kukagua sera za serikali kuanzia kwa wafanya biashara (maana zinaweza kuwa sera za Mkullo mbovu zinazotokana na ushuru mkubwa na kufanya wafanya biashara waweke bie zao juu na mtanzania kuumia), Kuna chombo gani kinachosema wakulima hawasaidiwi hili waweze jiendeleza kupitia kilimo na kukagua sera za kilimo chetu, maana hata hizo pembejeo kuibiwa tuna subiri mwanakijiji atujuze. Kuna chombo gani wewe binafsi umewahi kusikia ina-check chochote kuhusu sera mbovu na usimamizi wake ulivyo mmbovu kinafanya kazi.

U cant blame individuals on these matters ni poor politics (bad governance and the rest), social ignorance to understand their rights and the social groups responsible to give checks.
 

Hio post ambayo umeni quote I was stressing on kila mmoja kucheza nafasi yake ipasavo... Kwamba it not only about viongozi pekee bali hata wananchi.... Kwamba hata kama we do have a responsible and reliable Leader kama mwananchi hachezi nafasi yake tatizo balo lipo pale pale katika eneo zima la Poverty Elimination. Hili ambalo nime kuqoute is my stand too.... Good thing nime post on the same thing mda sio mrefu in another thread katika nafasi ya Leaders.... na this was it (a paste)

.... It does not matter kua the leader in question kashindwa kufurahisha kila mtu (kwanza itakua vigumu else huyo leader ni mnafiki!). What matters ni kua huyo Leader anaweza dhibiti nafasi yake kiasi kwamba vitu kama ufisadi wa nje nje unakua hamna, matatizo kama mikataba feki inkua hamna, Kwamba aweze kua Mzalendo.... Awe na uchungu na nchi na wananchi.... na juu ya hapo awe na qualities of a Great leader who is not afraid of making major decisions hasa in relation to the Betterment of the Nation. Hapo Mzalendo believe me you..... Leader akiwa hivo ni rahisi hata kufanya kazi; kwamba hata kama ana delegate, atahakikisha kuna jopo za kweli za quality insurance kuhakikisha all inaenda ipasavo na to it's best.


Mzalendo kuwaangalia wananchi sio tu kua wahakikisha umewafanyia kila kitu.... HAIWEZEKANI! Ila kuhakikisha unawawekea wananchi wako mazingira ya kuweza weka wepesi katika maisha yao kwa kungalia yale ambayo yawagusa moja kwa moja. For instance katika nchi nyingi za Kiafrika tegemezi kubwa la majority katika taifa ni Kilimo.... Bahati nzuri nchi zote hizi zina rules, guidelines na principles ambazo in most cases ziko impressive on paper; BUT Unfortunatley hazitelekezwi ipasavo... Hakuna kusema kua Serkali ipo that interested katika soko la mazao, ama quality ya end product, ama Processing machines, ama incentives za kutosha in the sector na sio za ubabaishaji kama ilivo.... That mind you is just one of the ways ya kuweza boresha na kugusa wananchi directly....
 
Reactions: Taz

OK based on your recent point how does uneducated human being in the village somewhere in rural Tanzania supposed to play his part in elevating his life chances (im thinking that is where poverty is the most), if he wasnt provided with the right skills?. Huyu mtu si ataishi kwa mbinu alizozikuta na ufahamu wake ndio hule hule aliopewa hapo hapo kijijini. Wewe leo unaweza lalama kuhusu viongozi wabovu (because you have been informed of your rights through education, working, your socialization process and the rest), what about yeye wa kijijini ambae kanyimwa the right education and skills to understand his rights and the likes, si ndio kesho anakwenda kuwapa kura yake, wale wanaomuumiza now tell me how does this individual suppose to improve his chances?




Hili suala ni la kikatiba zaidi we cant expect people to be patriots we give them the conditions and clear guidance on how they should conduct their bussiness and what is expected of them, again by creating groups that can check on them. That is how everybody else in liberal-societies is doing and it is working well for them, why cant we just copy that.
 

Kipindi cha Ujamaa World Bank, IMF, Donors walitoa pesa nyingi. Na zile alama za maendeleo zilizopatikana zisingekuwepo bila misaada kutoka nje.

Lakini siku zilivyozidi kwenda, hatukuweza kujenga economic model ambayo isingetegemea misaada ya kutoka kwa wahisani au mashirika ya pesa za dunia. Hivyo baada ya kutupa pesa na kutuachia tufanye tunavyotaka, wamehamua kutupa pesa na kutuambia nini tufanye (stick and carrot approach).

Ukiwa unapewa misaada huna sababu ya kuonana na wananchi wako. Hivyo toka enzi ya ujamaa mpaka sasa tunajenga nchi kwa kujaribu tu na kutumaini kuna siku majaribio yatatiki.

Z-10
 
hivi kuna hata nyanja au sekta moja sisi tunaweza kujisifu tupo makini? (hapa siulizii umakini wa asilimia, hasha bali angalau tunaweza kuridhika kuwa hapo tunapiga hatua kwenda mbele?)
 
True but that is not the whole truth, we have seen that in a grand scale such as in Greece recently. You don't have to play their ball completely, if you can give them sound economical plans and ways to repay the debt they can negotiate. Only when you put nothing on the table that is where most of the policies would be direct from them.

Sasa kama kungekuwa na current economical plan tailored to suit current circumstances, that is where the starting point of negotiations between them and us. Au kaka unafikiri, Mkukuta and 'five years plan' ni kwa ajili ya nini? Hule ni usanii wa CCM kuwapelekea na negotiotions zina anzia hapo.

Kwa maana hiyo suala kusema SAP's are entirely on sided is misleading.

Ghana wanatunga baadhi ya policies zao sasa.
 

AshaDii,

Kuna ukweli kuwa ni lazima kila mtu afanye vizuri katika nafasi. Lakini ni nani anayeakikisha kuwa watu wanafanya vizuri katika nafasi hizo?

Tukikazania kuwa ni lazima watu wa chini nao wawajibike kwenye nafasi zao, tutakuwa kwenye catch 22: Huwezi kupata kiongozi anaye wajibika bila kuwa na watu wanaowajibika. Na huwezi kupata watu wanaowajibika mpaka uwe na kiongozi anayewajibika, vicious circle.

Imefika wakati wale wanaopenda nchi yao wajitolee na kuonyesha mfano.
 

Eric Cartman,

Nakubaliana na wewe. Kuna geo-politics. Mfano wa Greece hipo kwenye Euro zone. Hivyo World Bank na IMF itakuwa na mtazamo mwingine.

Russia katika 90s walikuwa na matatizo vilevile. Lakini Nuclear Arsenals zao zilifanya nchi za magharibi kufikiria mara mbili.

Vilevile kuna wheel of fortune. Ghana ameanza kupump mafuta. Hivyo reserve yake ni kubwa. Angola nao wana-pump mafuta.

Nigeria wanajenga reli. World bank alitoa masharti makubwa. Kesho yake mchina bila kukaribishwa akachuka na manoti yake na kutoa offer iliyofanya nchi za magharibi zikae vinywa wazi.

Tukija kwa Tanzania, hatuna nafasi kama zilizopo hapo juu. Hivyo ni lazima tutumie akili na juhudi zetu wenyewe.
 

Hata kama tutapa viongozi wazuri, tusipokuwa na nia ya kupata mafanikio tusahau...hizo zitakuwa ndoto. Naamini umaskini wetu unachangiwa pia na tabia zetu...uvivu na ujinga wa kutotaka kujielimisha vikiongoza.
 
Wahindi wala rushwa hawa watachukua miaka mingi kumaliza hizo project...Na asilimia kubwa ya matatizo yetu ya leo ni "made in India".
 

Zakumi sera zinatendeka na hela kwa hiyo kusema hatuna room to manouver si kweli. Hayo ya nchi zilizo fortunate kuwa na precious marialisili zinaingiza hela na kuweza ku-invest wisely ni kweli. Hila na sisi hatuna priorities simple as that si 'IMF' wala 'WD' wakulaumiwa kwa yote ni siasa zetu tu.

Hela ya marupupu, per diems, VX's ni policy tayari ya kuweza kuinua maisha ya wengi, kama ulivyogusia hawali amna performace based bonuses watu wanalipwa tu. Hapo bado ujazingatia hela ambazo zimetengwa kufaniskisha policy kadhaa nazo zinavyopotea, bila ya the right mechanism to police the policies.

To put simply we need a new constitution first that considers accountability and the next phase is politics. That is where creativity can begin.
 

Sasa nani anawapa uhuru huo donors?
 

Eric,

Vitu vinafanyika na ndio maana nikaanzisha hii thread. Watanzania tuna matatizo katika kupanga na ku-execute. Hivyo kusema kuwa tunaweza kwa kuangalia mifano ya wenzetu bila sisi wenye kujenga capabilities zetu itakuwa kujidanganya.

Kwa kuangalia mazingira yetu, inabidi tuwe na political will na nidhamu ya juu kwa sababu ya idadi ya watu wetu. Ukubwa wa nchi yetu na resources zilizokuwepo.

Kwa sasa hivi political will na nidhamu hipo kwenye short supply. Na athari za kutokuwa na nidhamu tunaziona hata kwa nchi zilizoendelea. Mfano mzuri ni nchi za Euro Zone. Nchi ambazo hazina nidhamu katika sera zake zipo kwenye matatizo makubwa kuliko zile zenye nidhamu.
 
Hata kama tutapa viongozi wazuri, tusipokuwa na nia ya kupata mafanikio tusahau...hizo zitakuwa ndoto. Naamini umaskini wetu unachangiwa pia na tabia zetu...uvivu na ujinga wa kutotaka kujielimisha vikiongoza.

Ndahani,

Wakati mwingine uvivu wa watanzania na mazingira ya kazi. Chukua kima cha chini ambacho analipwa mfanyakazi wa serikali. Siwezi kumlaumu mfanyakazi yoyote anayepokea kima hiki kufanya kazi kwa uvivu. Je katika sekta ya umma wapo watu wangapi wenye kupokea mishahara hii? Wengi.
 
hivi kuna hata nyanja au sekta moja sisi tunaweza kujisifu tupo makini? (hapa siulizii umakini wa asilimia, hasha bali angalau tunaweza kuridhika kuwa hapo tunapiga hatua kwenda mbele?)

Nyanja kubwa ya kujivunia ilikuwa kuzungumza siasa za dunia na Afrika wakati ndani hatufanyi chochote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…