Power Mabula: Mtu aliyetikisa enzi zake!

Power Mabula: Mtu aliyetikisa enzi zake!

Kabisa hiyo naongelea pale uwanja wa shule Tabora town school 1981 hivi
Uko sahihi ni miaka hiyo nakumbuka ilidondoka ndege ya kivita pale uwanja wa taifa wa zamani Dar, ilikuwa parade sikukuu ya mashujaa,alikuwepo pale...
 
moja ya picha yake akiwa amebeba tofali kwa meno.

97953920_745908609484569_7177558229505461250_n.jpg
 
I knew him personally and I always have a story to tell about him.

You can hit me up whenever is convenient for you and I'll be glad to share it with you.

He is the source of my lifelong passion.
Uncle Juju mbona mimi hujanihadithia kumhusu.
 
Niambie kwanza....mshikaji wangu yupo au hayupo? [emoji3][emoji6]
Mshkaji wako yupo [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] leo nimempa wali maharage kakataa anauliza "mama mbona hakuna mchuzi" nilicheka sana.
 
Nakumbuka enzi hizo kulikuwa na vipindi vya michezo ya kwenye radio, kama vile, Mahoka (Na kicheko chake, mama mbavu zangu x2 eh eh eh eh eheeeeeeeeeeeeeeeeeH AAAH) na Pwagu na Pwaguzi...!

Kuna mchezo mmoja wa Pwagu na Pwaguzi, walianzisha mradi wa zahanati ya kungoa meno huku wakiwa hawana mafunzo yoyote ya udaktari wa meno, nje ya ofisi yao waliweka bango kubwa likionesha kuwa wao ni wataalamu wa kungoa meno.

Mteja akifika anapokewa mapokezi na mwenzake Pwaguzi, baada ya kulipia pesa ya matibabu anakwenda chumbani aliko Pwagu na kuanza kungolewa meno kwa kutumia koleo za mafundi baiskeli, Ah ah ah ah.

Issue inakuja kwenye kuulizia fedha ambazo mteja alitoa, Pwaguzi siku zote alikuwa anamdhurumu mwenzake, uwa anadai kuwa zilishapotea katika purukushani za kukimbia...!

Nakumbuka kuna mradi mwingine, walikuwa wanakusanya damu za mbuzi, na kuzipeleka Hospitali, eti wanadai wanatoa msaada kwenye benki ya damu, ah ah ah ah. Hawa jamaa walikuwa mwisho.

Nawakumbuka magwiji wa michezo ya kuigiza yaani maselebu wa ukweli, kama Marehemu Mzee Hamis Tajiri (Janja au Meneja Mikupuo), Marehemu Bi Tunu Mrisho (Mama Haambiliki), Mwanaheri Ngandu, Justin Kilumbi, Ali Manjunju (Ngosha), Marehemu Mzee Batholomeo Milulu (Masawe) na Marehemu Mzee Ibrahim Raha (Mzee Jongo) Mzee Fundi Said (Kipara) na wenginewe nimewasahau.

Umetaja jina la Manjunju, Kuna mtaa Huku kahama unaitwa “Mzee Maanjunju” kunaweza kukawa na uhusiano wa Jina hilo na huo mtaa ??
 
Aisee huyu jamaa alivuma sana miaka ya 80 but sadly I never got to see him. Kulikuwepo na story kibao kuhusu uwezo wake wa nguvu za misuri, mambo kibao yaliongelewa, mfano:

-- Alikuwa anaweza kunywa kreti nzima ya soda kwa mkupuo...
Power mabula enzi zake. Ila kwa story za waliomwona wanasema alikuwa hadi lori linamkanyaga.

Anavuta trekta kwa nywele zake maana anarasta napia sio tu hivyo hadi magari yeyote yale mazito ogopa fuso imejaa mchanga anaivuta au inamkanyaga naanaamua kuitingisha mara anaiangusha
 
nilimuona mara kadhaa kwenye maonesho wakati nikiwa primary skul. ni kweli alikuwa anafanya hayo yote yaliyotajwa,ilikuwa inaogopesha aisee.mara ya mwisho niliskia habari zake kuwa aliokoka na akatolewa mapepo mengi.

Ilisemekana alikuwa anatumia nguvu za giza na hizo kreti za soda walikuwa wanakunywa majini (sijamuona live baada ya kuokoka).ila naskia aliacha mazingaombwe.umenikumbusha mbali sana
King'ast mpaja wako kwenye avatar unaonyesha wewe si mbibi ni mdada
 
Miaka ya 80 mwishoni niliona shoo yake, aliweka mkono chini gari likapita juu ya mkono
 
Enzi hizo za mazingaombwe kulikua na
Power Mabula-akivuta gari kwa meno
Profesa Eyesu yeye hana ubabe
Weka makaratasi kwenye chungu inageuka dolale🙃😆😆😁
Hawa watu wako wapi?

Wakongwe jazieni hapo
 
Enzi hizo za mazingaombwe kulikua na
Power Mabula-akivuta gari kwa meno
Profesa Eyesu yeye hana ubabe
Weka makaratasi kwenye chungu inageuka dolale🙃😆😆😁
Hawa watu wako wapi?

Wakongwe jazieni hapo

ipo mada yake humu ndani. ngoja nikutafutie
 
Back
Top Bottom