Presha yawa kubwa kwa Luis Miquissone, benchi lamtesa, Simba watajwa, wadau Al Ahly waja juu

Presha yawa kubwa kwa Luis Miquissone, benchi lamtesa, Simba watajwa, wadau Al Ahly waja juu

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
Vigogo wa Afrika, Al Ahly wamepoteza mchezo wa nusu fainali ya Klabu Bingwa Dunia kwa kufungwa mabao 2-0 na Palmeiras ya Brazil, usiku wa kuamkia leo.

Kwa maana hiyo AL Ahly sasa wanasubiri kucheza mechi ya kutafuta mshindi wa tatu dhidi ya Al Hilal ya Saudi Arabia au Chelsea ya England ambazo zitacheza leo katika nusu fainali nyingine ya michuano hiyo.

Katika mchezo huo waliopoteza Al Ahly, winga wao, LUIS MIQUISSONE alikuwa benchi na hakutumika.

Kutotumika kwa staa huyo kumetokana na kutokuwa na mwendelezo mzuri uwanjani tangu amesajiliwa na timu hiyo mwanzoni mwa msimu huu akitokea Simba na inaelezwa kuwa hana furaha kwa kuwa hana uhakika wa kucheza katika kikosi cha kwanza.

Presha imezidi kuwa kubwa kwa MIQUISSONE kutoka kwa wachambuzi, mashabiki na wadau wa klabu yake hiyo wakishutumu kuwa alisajiliwa kwa dau kubwa lakini hajaonyesha kile ambacho kilitegemewa.

Mwenzake, Clatous Chama ambaye awaliodoka Pamoja lakini wakienda timu tofauti, amerejea Simba na ameshaanza kuitumikia timu hiyo ambapo naye hakuwa na wakati mzuri uwanjani alipokuwa amesajiliwa na RS Berkane ya Morocco.

Tayari maoni ya mashabiki hawa wa Tanzania wanaamini kuwa ni bora arejee Simba kwani akiendelea kubaki huko atanenepa kwa ajili ya kukaa benchi.

Luis.JPG
 
Tatizo sio kurejea Simba ila itahitaji akubali pay cut kwanza maana Konde boy anakula takribani million 95 kwa mwezi pale Al Ahly na mkataba wake nadhani ni mpaka 2025.

Swala la kunenepa tu kwa ajili ya kukaa benchi kwa wachezaji wa kiafrika na amerika kusini wanaotokea familia duni au za kawaida kwao sio kesi huwa hawaoni hasara kuzikacha timu kubwa na kwenda hata China au Falme za kiarabu wakiwa bado na viwango vikubwa yote sababu ya pesa.
 
Waarabu ni washenzi sana wana dharau sana mara wamchezeshe kama beki mara akae benchi....Daaah
Sasa dharau ya hao Waarabu iko wapi? Mbona ni kawada sana kwa mchezaji kubadilishiwa majukumu ya kiuchezaji ndani ya uwanja na kocha wake!

Na kama ni huko kukaa benchi, hata wenzake akina Eden Hazard kule Real Madrid wanasugua tu benchi, ingawa walisajiliwa kwa fedha nyingi!

Bidii na maarifa uwanjani ndiyo kila kitu unapo sajiliwa na timu kubwa! Ukiendekeza uvivu, kuruka ruka na kupuyanga tu uwanjani, utawekwa benchi! Na wenzako wata deliver kile kitu ambacho mwalimu anataka.
 
Mwishowe watamuathiri kisaikolojia ashindwe kabisa kucheza.

Naye aombe tu kurudi zake simba kama alivofanya mwenzake chama
 
Mwishowe watamuathiri kisaikolojia ashindwe kabisa kucheza.

Naye aombe tu kurudi zake simba kama alivofanya mwenzake chama
Benchi linaweza kushusha kiwango chake, akipoteza kujiamini atapoteza direction na anaweza kushindwa kurejea katika kiwango chake cha juu.
 
Waarabu ni washenzi sana wana dharau sana mara wamchezeshe kama beki mara akae benchi....Daaah
Waarabu awa mchukii Ila walichotegemea kutoka kwake Kwasasa mchezaji bado haja kifikia. Luis anaitaji muda kuweza kufikia Kiwango walichotarajia tatizo Timu ni kubwa na Ina presha ya Matokeo. Timu kubwa hazina tabia ya kusubiri mchezaji awe Bora, Timu kubwa zinahitaji matokeo.
Luis akirudi Simba bado atakuwa nyota Ila kule Misri badosana kwa level aliyonayo Sasa.
 
Waarabu awa mchukii Ila walichotegemea kutoka kwake Kwasasa mchezaji bado haja kifikia. Luis anaitaji muda kuweza kufikia Kiwango walichotarajia tatizo Timu ni kubwa na Ina presha ya Matokeo. Timu kubwa hazina tabia ya kusubiri mchezaji awe Bora, Timu kubwa zinahitaji matokeo.
Luis akirudi Simba bado atakuwa nyota Ila kule Misri badosana kwa level aliyonayo Sasa.
Akili za kuazima utazijua tu.. (Joke mtani) Ni zako TU.

Ni kweli kabisa huwa inachukua muda kwa mchezaji kuingia kwenye mfumo wa Team labda itokee bahati na hapo ndo team kama inahutaji matokeo uvumilivu unakosekana ila kwa Real Madrid, Hazard ana bahati sana kuvumiliwa.
 
Kocha mwafrica toka South Africa hana sababu kumuweka bench ukiwa uwezo unao kule wenzetu unahukumiwa kwa matokeo uwanjani unasaidia vipi team sio magazetini. South Africa tu hakuweza kwa hiyo sishangai kushindwa Misri. Tuje huku kucheza mpira wetu wa majukwaani ushindani bado hatuwezi.
Waarabu ni washenzi sana wana dharau sana mara wamchezeshe kama beki mara akae benchi....Daaah
 
mpira una levels ,yupo kwnye ligi kubwa baran Afrika n timu anay chezea n kubwa pia so inahtajika akili y mpira iliyokomaa zaid n sio kipaji tu peke'ke!
 
Ningeshangaa sana, eti mchezaji atoke kwenye ligi hii ya Tanzania iliyojaa maamuzi yenye utata aende ang'are kwenye ligi kubwa kama ya Egypt, it's impossible.

Hao ni wachezaji wadogo hawana mpira wa kuchezea timu kubwa kama Al Ahli saizi yao ni huku huku mchangani wanakocheza na majukwaa.
 
Back
Top Bottom